Watu 7 (Wawili wana asili ya #Asia) wanashikiliwa baada ya Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ya Tanzania (DCEA) kukamata Kilogramu 3,182 za dawa za kulevya aina ya #heroin (Kg. 2,180.29) na #methamphetamine (Kg. 1001.71) katika Mikoa ya #Dar na #Iringa (Wilaya za #Kigamboni, #Ubungo #Kinondoni na #Iringa) kati ya Desemba 5 na 23, 2023.
Taarifa ya #DCEA imeeleza kuwa Ukamataji huo umehusisha kiasi kikubwa cha #DawaZaKulevya ambacho hakijawahi kukamatwa katika historia ya #Tanzania tangu kuanza kwa shughuli za udhibiti wa dawa za kulevya
Taarifa hiyo imefafanua zaidi kuwa dawa hizo zilizokuwa kwenye vifungashio vya bidhaa zenye chapa mbalimbali za #Kahawa na Majani ya Chai, endapo zingefanikiwa kuingia Mtaani zingeweza kuathiri zaidi ya watu 76,368,000 kwa siku.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.