Vitambulisho vya Taifa vyakataliwa Benki

Vitambulisho vya Taifa vyakataliwa Benki

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,267
DSC02503.jpg
mwenye habari za kina/ gazeti hili atujuze
 
Hii nchi inachezea hela zetu za kodi;
- Kitambulisho cha kupigia kura cha zamani eti hakitumiki tena;
- Kitambulisho cha taifa, sijui nacho ni feki;
- Kitambulisho kipya cha kupigia kura.

Hivi nyie wanasheria mliobobea mnawezaje kukaa kimya
na kuangalia upotevu mkubwa kama huu wa pesa
za walipa kodi.
 
Hii nchi inachezea hela zetu za kodi;
- Kitambulisho cha kupigia kura cha zamani eti hakitumiki tena;
- Kitambulisho cha taifa, sijui nacho ni feki;
- Kitambulisho kipya cha kupigia kura.

Hivi nyie wanasheria mliobobea mnawezaje kukaa kimya
na kuangalia upotevu mkubwa kama huu wa pesa
za walipa kodi.

Mamdenyi nakupa heko, leo umeongea ukweli na uwazi. Naunga mkono hoja yako kwa wanasheria bobezi.
 
Ufeki wake ni kuwa havina saini ya mtumiaji. Huwezi kutambulika benki bila ya kitambulisho chenye saini yako.Na wale jamaa walioshinda tenda walifanya kusudi ili tuwarudie kuwapam ingine kwa ajili ya kutuuzia scanners maalum kwa ajili ya ukamilisho wa utambuzi wake.

DSC07923.JPG
 
Serikali wanachukua fedha then hawarudishi,mafisadi wanakopa kwenye mifuko nao hawarudishi unategemea itaendelea? Kila mwaka ma DG na officers wanalipana bonus za 200m hadi 400m unategemea nini? Saccos wanakopeshwa watu wanakula hawarudishi ni kama mabillioni ya jk.
 
Wanasheria wa bongo ni njaa tu!! Heeee mimi hata hicho kitambulisho cha taifa sina, itabidi nikivizie Mwanza.

Usiombe ukutane na viongozi warafi na wazinzi kama hawa wa CCM na wakurungezi wao, wanapenda sana anasa, magari yao V8, BMW, yanakula mafuta hatari liter 1 km 4-5, ni lazima wafirisi mifuko.
Starehe na uzinzi ni gharama je wanatoa wapi pesa?? Mbona wengine tunazisaka masaa 16 hatupati kitu?
 
wamesema saini imefichwa ki elektroniki
Ufeki wake ni kuwa havina saini ya mtumiaji. Huwezi kutambulika benki bila ya kitambulisho chenye saini yako.Na wale jamaa walioshinda tenda walifanya kusudi ili tuwarudie kuwapam ingine kwa ajili ya kutuuzia scanners maalum kwa ajili ya ukamilisho wa utambuzi wake.

DSC07923.JPG
 
Serikali wanachukua fedha then hawarudishi,mafisadi wanakopa kwenye mifuko nao hawarudishi unategemea itaendelea? Kila mwaka ma DG na officers wanalipana bonus za 200m hadi 400m unategemea nini? Saccos wanakopeshwa watu wanakula hawarudishi ni kama mabillioni ya jk.
nini kifanyike sasa>>>
 
nini kifanyike sasa>>>

Serikali ijitoe kabisa kwenye mifuko ya hifadhi hapo tutatua mengi,rais ndio anamteua dg unategemea dg ataenda kinyume na rais? Ahadi za rais na chama zinatekelezwa na mifuko no returns!! Mifuko ijikite kwa madumino yaliyokusudia na si kukopesha watu binafsi na ketekeleza ilani za chama.
 
Ni kweli kabisa hiki ni feki, kile cha kupiga kura kilikuwa kinafaa sana, kwa sababu kilikuwa kinamfanya mtu atambulike mpaka anapoishi kirahisi unaweza kumpata hata muhalifu. Ni sawa kabisa Bank na taasisi nyingine kukikataa.
 
ndio maana mimi sijajiandikisha, halafu tuone kama watanifuta utaifa wangu, hata details zilizomo ni za kawaida za kila siku, kwanza kitambulisho cha utaifa kina expire date kama leseni? wakati wewe ni mtu wa taifa hili moja kwa moja, na ili kitambulisho kikamilike lazima kiwe na saini yako ambayo inathibitisha kuwa chako. tusubiri vya kura vipya, tutaanza kutembea na pochi rasmi ya vitambulisho na kadi za bank.
 
yashushe hapa King

Kitendo cha kukataliwa bank kwanza kimeonyesha udhaifu mmoja wapo maana hakina sign pili tuliambiwa hivi vitambulisho vitakuwa ni smart ambavyo vitaunganisha kwenye mifumo yote ya utambuzi zikiwemo bank chuo etc lakini ukikiangalia hicho kitambulisho hakina kitu chochote cha utambulisho wa smart hata wakisema na hiyo imefichwa ki-electrinically nayo ni uongo na wizi mtupu tatu hologram waliyoweka ni ya kitoto sana ni rahisi sana kuwa faked,kina expire date,hakielezi utambulsiho wa makazi.
 
Lengo kubwa ni kuuweka utambulisho wa utaifa baadala ya Utanganyika na Uzanzibar.....................


Serikali mbili kuelekea serikali moja.......
 
Back
Top Bottom