Vita ijayo mashariki ya kati

Niseme kwa ufupi sana kwa sababu maalum. Nimewahi kushiriki kwenye technology panel ya Pentagon ambapo tulishirikiana kwa karibu sana na IDF. Inabidi tukubali kuwa wenzetu wako mbali sana; uwezekano wa Hizbollah au Iran kupata Technolgy ya Drone au long range missiles ni mambo waliyokwisha yaona zamani na kazi iliyokuwa mbele yao ni namna ya kuwadhibi; yaani walikuwa wanatafuta namna ya kuwadhibiti wairani na hizbollah kabla hata hao mahasidi wao hawajafikia uwezo huo. Nina wasiwasi sana na kila sababu ya kuamini kuwa iwapo Irani au nchi yoyote eneo la mashariki ya Kati itajipatia silaha hizo za nyukulia na ikajulikana kuwa ziko wapi basi silaha hizo "zitawalipukia" wenyewe ! Inabidi wawe makini sana na namna wanavyopata teknologia hatari za namna hiyo

Hapa unazungumza kitu kinachowezekana sana. Kwa kweli Wairan pia wanajua uwezo mkubwa wa Waisraeli na nyuma yake Wamarekani. Isipokuwa falsafa ya Iran juu ya ulinzi ni ya kujitegemea kwa kutengeneza zana zao wenyewe. Ingawaje itawachukua muda mrefu kufikia kiwango cha nchi hizo mbili, isipokuwa kujitegemea katika kuunda silaha kwenyewe ni 'deterrence' kwa vile itakuwa vigumu kwa nchi nyingine ku 'decipher' mali yao. Wairan hawa waamini Warusi. Urusi pia ipo chini ya influence ya Wayahudi (fuatilia majina ya wale walio katika shirika la Rosoboronexport), vile vile natumaini wajua Urusi imekataa kuiuzia Iran makombora ya S-300 ingawaje Iran ilikwishayalipia, kutokan na shinikizo za Israel na Marekani.
I am sure, Wairan nao they don't leave anything to chance. Labda hii ndiyo sababu hasa, kwa nini Israeli na Marekani haijaishambulia Iran hadi sasa. Ni kwa vile wanaogopa kupata surprises!
 
LALA LALA LELE LE II LOLO mziki una chorus safi safi huu hebu nisikilize nicheke, then niangalie serious thread nijenge afya mie
 
Please ongea ukweli, nikwamba hiyo UAV au SAI ilionekana mapema wakati inakaribia southern border ya Israel nawao walikuwa tayari washajua na hawakutaka kuitungua mapema vile sababu ya makazi ya watu, wenzetu wanajali utu, hivyo walisubiri mpaka eneo lisilo na makazi ya watu ndipo waitungue.

vita ya hizbullah na Israel, Hizbullah wanajichanganya kwenye makazi ya watu-walebanoni, raia, kwahiyo ulitaka IDF iue raia??

Unajua nini juu ya DEMONA REACTOR?? angekuwepo Rais ambaye marehemu, Rais Kennedy angekueleza na kwanini hadi leo rais anayeingia madarakani wa marekani lazima aiheshimu Israel??

Tusiwe washabiki wa upande wowote!

Si miaka mingi imepita tangu Israel ilipowashambulia raia wasio na silaha kwa kutumia mabomu ya sumu yenye kutoa moshi mweupe (phospharus). Kama sasa wanajali raia basi tumshukuru mungu.
 
Pole mr. Sijali kwa kutukanwa. sijaona ulichokosea ila ulichotakiwa ni kuweka links za hizi taarifa. Japo JF ni jamvi la watu makini hawakosekani wenye matusi. Edelea kuleta taarifa japo wengine watachukia.
Imebidi niandike makala hii baada ya tukio la kihistoria la siku tatu zilizopita juu ya anga ya Israel, na kuona kuwa huenda wengi hapa hawatakuwa na nyenzo au taarifa zitakazowasaidia kuli-analyse ipasavyo tukio hilo. Ni dhahiri kuwa SAI iliyoweza kupenya mazindiko ya anga (radar) ya Israel yasiyo na mfano popote duniani, na kusafiri kwa zaidi ya saa tatu hadi kwenye ncha ya vituo vya nuklia vya Israel....hii si hatua ndogo hasa ukiangalia uwezo mkubwa wa Israel na Marekani.
Ni dhahiri, baada ya bw Nasrallah kukiri kuwa ni Hizbullah kwa msaada wa Iran ndio waliotuma UAV, au SAI (Unmanned Aerial Vehicle- Safina ya Angani Ijiendeshayo = SAI), hakuna mtu atakayetia shaka sasa juu ya uwezo mkubwa wa Kiteknolojia walio nao Waajemi (Wa-Irani). Kwani kwa anayefuatia mambo, ni mara nyingi sasa Iran imetuonjesha weledi wake wa kiteknolojia. Chukua kwa mfano vita ya 2006 ya Hizbullah na Israel, ambapo kwa kweli Hizb ilimwendesha puta Mwisraeli kwa kuvunja vifaru maarufu vya Merkava (Kitanda cha Mungu:kutokana na wanavyoamini kuwa kina amani), na pia kuishambulia na kuichoma kwa kombora Meli ya kisasa zaidi Saur kwenye mwambao wa Lebanon, ambayo Waisrel waliamini hakuna yeyeto angeweza kuigusa na ndiyo maana wakaiegesha kando ya Lebanon.
Pili ni hekaya mashuhuri ya Iran kuitungua 5-generation SAI ya Marekani, Sentinel RQ-170 (the beast of Kandahar: mnyama wa Kandahar) ambayo haigunduliwi na Radar (kiasi iliposhiriki katika mauaji ya Osama huko Pakistan, Wapakistan hawakuwa na habari yeyote)--ambayo Wairan waliitungua kwa teknolojia bila ya kufyatua kombora na kuweza kuishusha ikiwa na mikwaruzo midogo dogo tu, jambo lililowatia aibu kubwa Wamarekani.
Tatu ni uwezo wa Wairan kupigana na kushinda virusi vikali vya Komputa (tarakilishi) viitwavyo Stuxnet na Flame bila ya msaada wa yeyote.
Nne kutuma kwao, kwa kulipiza kisasi, virusi vilivyofuta kumbukumbu zote za mashirika mawili makuu ya petroli katika Saudi Arabia na Qatar na kuambukiza komputa zaidi ya elfu 40 za mashirika hayo na hadi leo si Wamarekani wala Waarabu wameweza kuviondoa virusi hivyo, kiasi Leon Panetta, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Alhamisi ilibidi awaite wafanyibiashara wakuu wa Marekani na kuwaonya juu ya vita ya kibemasa (tafsiri yangu ya cyberwarfare, kama mchezo wa kibemasa)!
Yote haya yananionesha kuwa Iran, katika baadhi ya nyanja za Teknolojia, iko mbele hata ya Marekani (Jambo hili si rahisi kulichuuza maana watu wengi bado twawaangalia wazungu kama miungu watu, hawashindwi!).
Natija ninayotoka nayo ni kuwa vita ijayo itageuza kabisa sura ya Mashariki ya Kati, ikiwa si dunia nzima. Kwa kweli kuna nchi zitafutika kabisa katika uso wa dunia zizaliwe nyingine mpya- yaani haidhuru eneo litakuwepo lakini mfumo mzima kama tunavyoujua sasa hautakuwepo. Mithili ya yaliyotokea baada ya vita kuu za dunia ya kwanza na ya pili na vita vya hivi karibuni vya Balkani, ambapo nchi mpya zilizuka. Jambo muhimu zaidi, mfumo wa dunia 'world sytem' kama tunavyoujua hivi sasa, nao pia utatoweka.
Jee, una idea nchi gani zitatoweka na zipi zitabakia?
 
Alaa, wewe ni katika waleee waliokuwa wakikimbia somo la Jiografia shule? Waona sasa, matokeo yake wadhani Iran ni nchi ya Kiarabu!

Haafu hata hao Waarabu wenyewe, unajua uwezo wao wa kijeshi au wasikia tu? Usione kwa vile wameshindwa na Israel mara kadhaa kwa hiyo wako nyuma. Israel ina nguvu kubwa za kijeshi (inapata silaha za bure kutoka Marekani kila mwaka za thamani ya dola bilioni 3.5) hata ina uwezo wa kuzishinda nchi nyingi za Ulaya kijeshi- nchi kama Greece, Norway, Italy, Spain, Portugal...na wengine wanasema hata nchi kubwa kama India, Turkey, Canada nk.
Nchi za Kiarabu nazo, naamini Egypt, Syria, Algeria, Morocco.... zina uwezo wa kuzinyuka 97% ya nchi za Sub-Saharan Africa. Kwa hiyo ondoa mentality ya Uarabu, Uislamu n.k. na tafuta facts. Cha muhimu, soma na jielimishe!

Kweli, naona unaijua jiografia ya kiushabiki tu. Iran ni oldest civilizations ambayo kutokana na matamaduni yasioeleweka bado wanabaki nyuma ya mataifa mengi hasa ya Ulaya, Marekani Japan, China nk. Pia hiyo missada toka Marekani inatoka kwa Waisraeli wenyewe. Hujui kama matajiri wakubwa wa dunia, wanasayansi wakubwa ni Waisraeli? Haijalishi wapo Ujerumani, Marekani au EU. Wanajijua na wanadhamini sana nchi yao ingwa ipo uhamishoni. Sasa hao wenye maitikadi yao wanaotegemea kamisheni ya mafuta ili wale tende na kukaa kivuvi kwenye majamvi, na kujitapa na magari yanayotoka hukohuko, wakati huohuo utaalamu wa kuyachimba mafuta hayo lazima utoka EU, Marekani, Japan au China.
Sasa somo lako ni la kitoto, kama yale mambo ya kitoto yalioamsha uma wa watu wasikuwa na akili kughadhibika na kuchukua hatua za kishetani. Pole
 
Si miaka mingi imepita tangu Israel ilipowashambulia raia wasio na silaha kwa kutumia mabomu ya sumu yenye kutoa moshi mweupe (phospharus). Kama sasa wanajali raia basi tumshukuru mungu.

iliwashambulia magaidi !
 
Kweli, naona unaijua jiografia ya kiushabiki tu. Iran ni oldest civilizations ambayo kutokana na matamaduni yasioeleweka bado wanabaki nyuma ya mataifa mengi hasa ya Ulaya, Marekani Japan, China nk. Pia hiyo missada toka Marekani inatoka kwa Waisraeli wenyewe. Hujui kama matajiri wakubwa wa dunia, wanasayansi wakubwa ni Waisraeli? Haijalishi wapo Ujerumani, Marekani au EU. Wanajijua na wanadhamini sana nchi yao ingwa ipo uhamishoni. Sasa hao wenye maitikadi yao wanaotegemea kamisheni ya mafuta ili wale tende na kukaa kivuvi kwenye majamvi, na kujitapa na magari yanayotoka hukohuko, wakati huohuo utaalamu wa kuyachimba mafuta hayo lazima utoka EU, Marekani, Japan au China.
Sasa somo lako ni la kitoto, kama yale mambo ya kitoto yalioamsha uma wa watu wasikuwa na akili kughadhibika na kuchukua hatua za kishetani. Pole


Asante. Saa nyingine watu kama ninyi inabidi kuwanyamazia tu. Kama mpaka sasa wadhani Iran inategemea wengine kuchimba mafuta, au wanakaa jamvini kula tende tu....sidhani unaishi nyumba yenye umeme.
 
Asante. Saa nyingine watu kama ninyi inabidi kuwanyamazia tu. Kama mpaka sasa wadhani Iran inategemea wengine kuchimba mafuta, au wanakaa jamvini kula tende tu....sidhani unaishi nyumba yenye umeme.

Asante, kumbe wale Warusi baada ya USSR kusambaratika walipewe uraia? Kazi njema
 
Imebidi niandike makala hii baada ya tukio la kihistoria la siku tatu zilizopita juu ya anga ya Israel, na kuona kuwa huenda wengi hapa hawatakuwa na nyenzo au taarifa zitakazowasaidia kuli-analyse ipasavyo tukio hilo. Ni dhahiri kuwa SAI iliyoweza kupenya mazindiko ya anga (radar) ya Israel yasiyo na mfano popote duniani, na kusafiri kwa zaidi ya saa tatu hadi kwenye ncha ya vituo vya nuklia vya Israel....hii si hatua ndogo hasa ukiangalia uwezo mkubwa wa Israel na Marekani.
Ni dhahiri, baada ya bw Nasrallah kukiri kuwa ni Hizbullah kwa msaada wa Iran ndio waliotuma UAV, au SAI (Unmanned Aerial Vehicle- Safina ya Angani Ijiendeshayo = SAI), hakuna mtu atakayetia shaka sasa juu ya uwezo mkubwa wa Kiteknolojia walio nao Waajemi (Wa-Irani). Kwani kwa anayefuatia mambo, ni mara nyingi sasa Iran imetuonjesha weledi wake wa kiteknolojia. Chukua kwa mfano vita ya 2006 ya Hizbullah na Israel, ambapo kwa kweli Hizb ilimwendesha puta Mwisraeli kwa kuvunja vifaru maarufu vya Merkava (Kitanda cha Mungu:kutokana na wanavyoamini kuwa kina amani), na pia kuishambulia na kuichoma kwa kombora Meli ya kisasa zaidi Saur kwenye mwambao wa Lebanon, ambayo Waisrel waliamini hakuna yeyeto angeweza kuigusa na ndiyo maana wakaiegesha kando ya Lebanon.
Pili ni hekaya mashuhuri ya Iran kuitungua 5-generation SAI ya Marekani, Sentinel RQ-170 (the beast of Kandahar: mnyama wa Kandahar) ambayo haigunduliwi na Radar (kiasi iliposhiriki katika mauaji ya Osama huko Pakistan, Wapakistan hawakuwa na habari yeyote)--ambayo Wairan waliitungua kwa teknolojia bila ya kufyatua kombora na kuweza kuishusha ikiwa na mikwaruzo midogo dogo tu, jambo lililowatia aibu kubwa Wamarekani.
Tatu ni uwezo wa Wairan kupigana na kushinda virusi vikali vya Komputa (tarakilishi) viitwavyo Stuxnet na Flame bila ya msaada wa yeyote.
Nne kutuma kwao, kwa kulipiza kisasi, virusi vilivyofuta kumbukumbu zote za mashirika mawili makuu ya petroli katika Saudi Arabia na Qatar na kuambukiza komputa zaidi ya elfu 40 za mashirika hayo na hadi leo si Wamarekani wala Waarabu wameweza kuviondoa virusi hivyo, kiasi Leon Panetta, Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Alhamisi ilibidi awaite wafanyibiashara wakuu wa Marekani na kuwaonya juu ya vita ya kibemasa (tafsiri yangu ya cyberwarfare, kama mchezo wa kibemasa)!
Yote haya yananionesha kuwa Iran, katika baadhi ya nyanja za Teknolojia, iko mbele hata ya Marekani (Jambo hili si rahisi kulichuuza maana watu wengi bado twawaangalia wazungu kama miungu watu, hawashindwi!).
Natija ninayotoka nayo ni kuwa vita ijayo itageuza kabisa sura ya Mashariki ya Kati, ikiwa si dunia nzima. Kwa kweli kuna nchi zitafutika kabisa katika uso wa dunia zizaliwe nyingine mpya- yaani haidhuru eneo litakuwepo lakini mfumo mzima kama tunavyoujua sasa hautakuwepo. Mithili ya yaliyotokea baada ya vita kuu za dunia ya kwanza na ya pili na vita vya hivi karibuni vya Balkani, ambapo nchi mpya zilizuka. Jambo muhimu zaidi, mfumo wa dunia 'world sytem' kama tunavyoujua hivi sasa, nao pia utatoweka.
Jee, una idea nchi gani zitatoweka na zipi zitabakia?



[h=1]Report: Hezbollah drone made in Germany[/h] Lebanese newspaper claims downed drone's equipment purchased from German companies via dummy Iranian corporation





Lebanese newspaper Al-Jumhuriyah reported Wednesday that the equipment onboard the Hezbollah drone that infiltrated Israeli airspace was manufactured in Germany.

It was reportedly purchased by a dummy Iranian corporation which arms the Revolutionary Guards.

The Lebanese newspaper named Germany's Siemens and Bockstiegel as the companies from which the equipment was acquired.

According to the report, Hezbollah owns many drones similar to the one infiltrated Israel which are used for spy missions only. "The aircraft can carry 3 kg of explosives only," sources told the paper.

Previous reports suggested the drone was able to carry dozens of kilograms of explosives.

Meanwhile, a State Department source denied that Iran had extracted information from the US drone that crashed in its territory earlier this year.
 
iliwashambulia magaidi !

Kama hata watoto wenye umri wa siku chache na vikongwe waliouawa ni magaidi basi ni wazi kuwa kuna taifa lenye uoga wa ajabu linawaogopa hata vitoto njiti.
 
Ktk Top 10 ya majeshi yenye nguvu duniani,israel ipo na cha kushangaza ina wanajeshi wachache kupindukia,kombora dogo kuliko yote duniani limevumbuliwa na israel mwaka huu na wamemuuzia teknolojia mrusi kombora lenyewe lina uzito wa kilo nne na ni dogo kama rula na effect zake ni kama kombora linalobebwa na magari makubwa ya kijeshi...toa udini wako hv ufikirii kwa middle east nchi zinazoizunguka israel zikiweka silaha chini amani itakuja,ila israel akiweka silaha chini kifo kitamjia,for years wamemshindwa,sasa subiri soon uone iran itakavyobamizwa baada ya hapo mataifa ya kiarabu pamoja na urusi watakapovamia israel na kuharibiwa kabla ya kuingia mpinga kristo
Naona taifa teule halina raha
 
uSIWASIFIE HISBOLLAH KWA SABABU HISBOLLAH wao hawavai uniform za jeshina kama wanavaa uniform basi wasingekuwepo duniani! Wao huvaa kiraia na huja kama raia wema huku wameficha siraha, sasa Israel ni Taifa huru na linaloheshimu utu wa mtu, hivyo hawawezi kumlenga mtu asiye na nguo za kijeshi wakati wanapigana.

Halafu nawashukuru sana watanzania wanaounga mkono Israel. CCM na serikali yake walitulazimisha sana kuichukia Israel wakati wa ukomunisti. Leo hii watanzania tunajua ukweli kuwa hiyo yote ilikuwa ni chuki ya bure ili kuwaliwaza waarabu na azama zao za kutaka kuiteketeza israel.

Mungu ibariki Israel! shemaa alehemu alehemu adonai! maranataaa maranataaa!
Muda sio mrefu itadhalilika, jitaarishe kisaikologia
 
Ktk Top 10 ya majeshi yenye nguvu duniani,israel ipo na cha kushangaza ina wanajeshi wachache kupindukia,kombora dogo kuliko yote duniani limevumbuliwa na israel mwaka huu na wamemuuzia teknolojia mrusi kombora lenyewe lina uzito wa kilo nne na ni dogo kama rula na effect zake ni kama kombora linalobebwa na magari makubwa ya kijeshi...toa udini wako hv ufikirii kwa middle east nchi zinazoizunguka israel zikiweka silaha chini amani itakuja,ila israel akiweka silaha chini kifo kitamjia,for years wamemshindwa,sasa subiri soon uone iran itakavyobamizwa baada ya hapo mataifa ya kiarabu pamoja na urusi watakapovamia israel na kuharibiwa kabla ya kuingia mpinga kristo
daaaah
 
Back
Top Bottom