vipi utaamini mwanaume anakupenda?

vipi utaamini mwanaume anakupenda?

bidodo

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2013
Posts
217
Reaction score
90
ni msichana wa 22 ila akili yangu bado ya kitoto kuna mtu kasema ananipenda ni 2 month sasa na kasema haridhiki mpaka niende kwake hivi kweli ananipenda miii naogopa kwenda mnanishaurije??kasema kama sijenda simpendi wala hatonifanya kitu kibaya.
 
hamna kitu hapo binti...kama unaenda kwake ujue kuwa unampelekea 'nanii' yako! kumbuka kuna masuala ya mimba zisizotarajiwa na magonjwa ya zinaa kama baba lao linaloitwa 'ukimwi' a.k.a 'ngoma' au 'umeme'! take care...na kama unatafuna vya kwake juwa umejiweka kuwa kama kuku wa krismas..anytime unaliwa...
 
Usitudanganye binti yangu. We sema unapima kina cha maji. Kwa vile umeishajiingiza nenda kwake utajua huko huko kama anakupenda au anakutaka. Badala ya ukae na ufanye utafiti unakilimbilia JF.
ni msichana wa 22 ila akili yangu bado ya kitoto kuna mtu kasema ananipenda ni 2 month sasa na kasema haridhiki mpaka niende kwake hivi kweli ananipenda miii naogopa kwenda mnanishaurije??kasema kama sijenda simpendi wala hatonifanya kitu kibaya.
 
Siku hizi watu hawaendagi kwa watu tena mdogo wangu. Muambie mkutane bar kwenye mbuzi choma, ama kama anamudu mkutane karambezi. Ukienda kwake atakuomba umsaidie kuosha vyombo na kufua nguo.

Anyways, kuimbishwa miezi miwili ni muda mrefu sana eh?
 
Hahahahahahaha lohhh.

Anyway mama huyo jamaa anataka kitu kitam taaam. Kama we huko tayari usiende kwake .

Na kama anataka ukutane nae kwa maongezi mwambie lunch time tukutane kwenye restaurant hii au mama ntililie hii..

Just a suggestion:- kama humuamini sana huyo jamaa usiende dinner au activities zozote zile during the night.

Kama kipimo cha upendo wake ni we kwenda kwake eeehhhh hapo kuna kazi..

Take care & be careful.....
 
heeee km amekwambia usipoenda kwake hakupendi, ujue na ukifika kwake atakuomba umpozee dushelele lake, ukikataa atasema tena humpendi, utampa ili uonyeshe unampendaje, then utapata mimba, ukipata mimba atasema utoe, ukikataa kutoa atasema humpendi so utatoa kuonyesha unampenda. Ukitoa ndo kashakuharibu ivyoooo so atakutumia km ndala za chooni zenye thaman bafuni tu hata sebuleni haziruhusiwi sembuse ukumbini?
Be careful mdogo wangu funguka akili.
 
Nenda mdogo wangu usiogope, cku hizi kuna ushndani wa wanawake hivyo ukizubaa atakuacha kweli. We nenda tena uende umejiandaa kabisa kunaniliu, na ukiona anachelewa kukuomba anza kumtega kwa kumkalia vibaya na kumrembulia hayo macho yako mazuri. Fanyia kazi huu ushauri, wengine wanakupotosha ili ukose bwana!
 
Wewe umesema bado una akili ya kitoto acha mambo ya kikubwa.
 
usiende kwake kama ni mazungumzo mwaweza kutana lunch time kuwa mwangalifu dinner usiikubali katu kama anakupenda kweli sio lazima kwenda kwake
 
bidodo, yani kwanza em jipende wewe na kujali hisia zako first,maana smtyms kuwa selfish ni kitu kizuri sana,kujithamin mwenyew kwanza.
Coz unaonekana unajali hisia zake kwanza,kiasi kwamba ukijiingiza kwenye mapenzi(kama bado),utateseka sana kihisia.
Yeeye kasema anakupenda,uende kwake..ok,ujiulize je wewe unampenda?upo tayari kuwa na mahusiano kwa sasa?upo tayari kuwa nae?kwanin mkutane kwake,what so special?kwanin msimeet kwingine kama hakuna shida yoyote?!!
Kumbuka shetani na kamati yake,wameshashona sare,na huyo jamaa washamuandaa wanakusubiri wewe bi harusi,mkafunge ndoa gizani..kuwa private ,gizani, na mtu wa jinsia tofauti ni risk kubwa sana....(mama yangu aliniambia hili)..:tafakari Chukua hatua mdogo wangu..


Nb: usijali wanaokunanga hapa,ni chuya ktk mchele,we pepeta usonge mbele. Ushauri ni mwingi,maamuzi ni yako dear.
Goodlucky.
 
Last edited by a moderator:
ni msichana wa 22 ila akili yangu bado ya kitoto kuna mtu kasema ananipenda ni 2 month sasa na kasema haridhiki mpaka niende kwake hivi kweli ananipenda miii naogopa kwenda mnanishaurije??kasema kama sijenda simpendi wala hatonifanya kitu kibaya.
Wahenga wanasem ("fimbo ya mbali.........................") we jipeleke then ukavimbishwe, mbaya zaidi ukapate tiketi ya dozi ya milele.
 
ni msichana wa 22 ila akili yangu bado ya kitoto kuna mtu kasema ananipenda ni 2 month sasa na kasema haridhiki mpaka niende kwake hivi kweli ananipenda miii naogopa kwenda mnanishaurije??kasema kama sijenda simpendi wala hatonifanya kitu kibaya.
Kwanza unastahili pongezi kwa kuleta swala lako hapa jf ili upate ushauri makini.pili ushauri ni kuwa usiende kwake kwani utakuwa umefuata maangamizi yako wewe mwenyewe,kwani ukienda akakuomba mapenzi ukimkatalia akaamua kutumia nguvu,utapiga kelele kuomba msaada au utanyamaza?na ukipiga kelele utaeleweka ilhali uliingia humo ndani kwa miguu yako mwenyewe?
Na ili kujua ikiwa anakupenda au la,mweleze sababu za msingi za wewe kutoenda kwake usikie ataitikiaje,ikiwa atakuelewa nakutokukulazimisha kwa vitisho kuwa humpendi,basi ujue wazi kuwa huyo anakupenda na anajali hisia zako na yuko tayari kukusikiliza.Lakini ukimweleza sababu zako za msingi na bado asikuelwe na aanze kukutisha kuwa humpendi,washa taa nyekundu kichwani hiyo ni dalili mbaya huyo hakupendi na anajali hisia zake tu anataka kukutumia vibaya.Ukipata jibu maamuzi yatabaki kwako sasa kusuka au kunyoa si wengine ni watoa nasaha tu.
 
22 wewe si mtoto,hata katiba ya jmt imeweka wazi.
NENDA TU,kisha uje utuelezee YALIYOJIRI :mimba::dance:
 
We mdada apo kuna mambo unatakiwa kufanya chagua moja kati ya haya
1. Nenda ukiwa na msimamo wa kutofanya chochote nae
2. Nenda ukiwa na mwanaume wa kweli a.k.a (dume) kwa kinga zaidi
3. Mwambie mkutane sehemu ambayo ata weza kukupiga dushelele
UAMUZI NI WAKO
 
Hivi karambezi kuna mtori?

Siku hizi watu hawaendagi kwa watu tena mdogo wangu. Muambie mkutane bar kwenye mbuzi choma, ama kama anamudu mkutane karambezi. Ukienda kwake atakuomba umsaidie kuosha vyombo na kufua nguo.

Anyways, kuimbishwa miezi miwili ni muda mrefu sana eh?
 
Back
Top Bottom