Vipi nimkatalie?

Vipi nimkatalie?

mahirtwahir

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2013
Posts
614
Reaction score
322
Vikuba vya asumini,kaniletea tamasha
Mapenzi ya utotoni,leo kaja yakumbusha
Yanamwenda midomoni,kwa furaha na bashasha
Kaja omba samahani,vipi nimkatalie?

Hakosi kunahibika,yuko kwangu mikononi
Uso ameuvubika,yuko kwangu kifuani
Kama mwana amefika,kwa mama mwenye imani
Kaja omba samahani vipi nimkatalie

Naipenda sura yake,mzuri hana maringo
Mchesh hulka yake,atembea kwa mikongo
Apendeza kwa mwanya wake,tabasamu la maringo
Kaja omba samahani,vipi nimkatalie

Tatizo wazazi wake,ndio wanotuhasimu
Hawataki awabanduke,awe kwao dama dawamu
Asema ni mboni yake,kuichocha hajatimu
Kaja omba samahani,vipi nimkatalie?
 
::
Mkatalie kwa kusamehe,usiumize moyo wako.
Wazazi wana maisha yao,usiumize moyo wako.
Mkatalie kwa kuishi nae,usiumize moyo wako.
Mkamatilie usimwache,usiumize moyo wako.
Bahati hairudi kinyume,usiumize moyo wako.
Hai Hati Hai Hati ee,
Hadi kwa mola awe wako.
=
 
sijitie jitimai,kukosa kilo moyoni
tamasha yu kifuani,lipi jibu watakani
wabusu kwake pajini,kututega tujibu nini
jipe raha ya moyoni,tamasha nawe penzini

situtie kashdani ,lawama ukatutwika
mlopendana ni ninyi,utotoni mlikoweka
wenu wa kwenu ubani,moyoni ukabebeka
jipe raha ya moyoni ,tamasha nawe penzini
 
sijitie jitimai,kukosa kilo moyoni
tamasha yu kifuani,lipi jibu watakani
wabusu kwake pajini,kututega tujibu nini
jipe raha ya moyoni,tamasha nawe penzini

situtie kashdani ,lawama ukatutwika
mlopendana ni ninyi,utotoni mlikoweka
wenu wa kwenu ubani,moyoni ukabebeka
jipe raha ya moyoni ,tamasha nawe penzini
snowhite kwa hili shairi mwanafunzi anaruhusiwa kumletea mwalimu wake zawadi ya kikuba?
 
Last edited by a moderator:
Kama anataka kukumbushia, wewe gegedana
Huwezi kujua, labda amekukumbuka
Kabla hujaendelea, unaweza kuniambia
Muda gani hamjaonana, hebu funguka

Kama wewe kweli unampenda, usilaze damu kumbushia
Haina haja ya kuumia, huku tunda unalitaka
Kitu gani bana, maisha mafupi kula bata
Eti Wewe ulimtoa bikira, haina haja ya kumkatalia

Wazazi kawaida, msamehe kwa yaliyotokea
Maisha ni kusameheana, huwezi jua
Pengine mama mtarajiwa, watoto atakuletea
Tena narudia, usithubutu kumkatalia

Hebu malizia, anajua kupika
Jiko limejileta, chukua jumla
Kabla wakware kummendea, utakuja jijutia
Nakutakia mafanikio mema, endelea kula raha za dunia
 
Kama anataka kukumbushia, wewe gegedana
Huwezi kujua, labda amekukumbuka
Kabla hujaendelea, unaweza kuniambia
Muda gani hamjaonana, hebu funguka

Kama wewe kweli unampenda, usilaze damu kumbushia
Haina haja ya kuumia, huku tunda unalitaka
Kitu gani bana, maisha mafupi kula bata
Eti Wewe ulimtoa bikira, haina haja ya kumkatalia

Wazazi kawaida, msamehe kwa yaliyotokea
Maisha ni kusameheana, huwezi jua
Pengine mama mtarajiwa, watoto atakuletea
Tena narudia, usithubutu kumkatalia

Hebu malizia, anajua kupika
Jiko limejileta, chukua jumla
Kabla wakware kummendea, utakuja jijutia
Nakutakia mafanikio mema, endelea kula raha za dunia

Mkuu HARUFU mbona mizani inagongana? Au ndio ushairi mambo leo? Btw big up sana!
 
Last edited by a moderator:
mkatalie moyoni ,zama zake zimepita
jiwekee tumaini,mwingine utampata
mwenye uzuri wa shani,huyo anatapatapa
usilambe matapishi,ving'aavyo vingalipo











anaomba samahani,jua amekosa soko
akuona wa thamani, aache vyake vituko
suraye haina soni,kawa kama mbwa koko
usilambe matapishi,ving'aavyo vingalipo


kama wataka tulizo,niko hapa nibaini
njoo nikupe liwazo, achana na huyo haini
kwangu hakuna mizozo, wazazi wala jirani
usilambe matapishi, ving'aavyo vingalipo
 
mkatalie moyoni ,zama zake zimepita
jiwekee tumaini,mwingine utampata
mwenye uzuri wa shani,huyo anatapatapa
usilambe matapishi,ving'aavyo vingalipo











anaomba samahani,jua amekosa soko
akuona wa thamani, aache vyake vituko
suraye haina soni,kawa kama mbwa koko
usilambe matapishi,ving'aavyo vingalipo


kama wataka tulizo,niko hapa nibaini
njoo nikupe liwazo, achana na huyo haini
kwangu hakuna mizozo, wazazi wala jirani
usilambe matapishi, ving'aavyo vingalipo



Ulionena ni kweli,inangia akilini
Kua alikua ghali,ila sasa hana soni
atafuta afadhali,japo kwa kichochoeoni
Hata anambie nini,sirejei matapishi

Mwanzo nembembeleza,kwa wangu umasikini
Hampa nisivyoweza,ili asinighaini
ndipo alipo nibeza,kuona sina thamani

Nafasi ulionipa,ninaitamani kweli
Ni vipi nitakupata,unipoze yangu hali
 
Ulionena ni kweli,inangia akilini
Kua alikua ghali,ila sasa hana soni
atafuta afadhali,japo kwa kichochoeoni
Hata anambie nini,sirejei matapishi

Mwanzo nembembeleza,kwa wangu umasikini
Hampa nisivyoweza,ili asinighaini
ndipo alipo nibeza,kuona sina thamani

Nafasi ulionipa,ninaitamani kweli
Ni vipi nitakupata,unipoze yangu hali
nafasi hii i wazi, japo ina washindani
wengi wataka mizizi, wakailie gizani
njoo ulijaze zizi, ubebe jiko nyumbani
usinifanye kipozeo, kama yule wa zamani
 
nakuna kichwa nawaza, nikujibu jibu gani
ninajaribu kujikaza, jibu haliji kichwani
hili ni beti la kwanza,sijui nijibu nini
kama kweli wa mpenda, kwa nini umkatalie?

beti la pili naanza,nashikwa na bumbuwazi
kuna jibu limejibanza, nataka niweke wazi
tamasha alikuwa wa kwanza,kabla kujua wazazi
kama kweli unampenda, kwa nini umkatalie?

mapenzi kama kiatu, tamasha anakutosha
sije sikiza ya watu, tamasha hutomkosha
mimi ntakuona fyatu, tamasha ukimrusha
kama kweli unampenda, kwa nini umkatalie?
 
Mahir Twahir tafadhali acknowledge kwamba hilo shairi si la kwako.

Watunzi wenyewe ni Ikhwan Safaa (Malindi)

Muimbaji ni marehemu Maulidi Machaprala.
 
mkatalie moyoni ,zama zake zimepita
jiwekee tumaini,mwingine utampata
mwenye uzuri wa shani,huyo anatapatapa
usilambe matapishi,ving'aavyo vingalipo



kama wataka tulizo,niko hapa nibaini
njoo nikupe liwazo, achana na huyo haini
kwangu hakuna mizozo, wazazi wala jirani
usilambe matapishi, ving'aavyo vingalipo

Hapo dada umetisha jamaa ashindwe mwnyewe, Big up to you
 
Nipite kistaarabu,nisiharibu majibu
Mbona watugea tabu,AMA Una tujaribu
AMA wataka sababu, jibu baya tukujibu
Za bibi AMA za babu,ndo kumbukumbu mujarabu

Yupo kwako mikononi, Mara yupo kifuani
Si ajabu Yu chumbani,mnagegedana ka zamani
Sass watuuliza nini, wakati unaye ndani
Ka si Shari kitu gani,kumchokonoa pweza puani

Hitimisho namaliza, waonekana wampenda
Katu usije jikawiza,mbali nawe ataenda
ILA ya wazazi sikiliza,japokua wampenda
Usije kupata viza,waliokuusia kutoyatenda....
 
Ulionena ni kweli,inangia akilini
Kua alikua ghali,ila sasa hana soni
atafuta afadhali,japo kwa kichochoeoni
Hata anambie nini,sirejei matapishi

Mwanzo nembembeleza,kwa wangu umasikini
Hampa nisivyoweza,ili asinighaini
ndipo alipo nibeza,kuona sina thamani

Nafasi ulionipa,ninaitamani kweli
Ni vipi nitakupata,unipoze yangu hali
Mkuu shukurani ya punda?, umepewa ushauri
Badala ya kuuchukua, au kuufanyia kazi
Wewe unakamata fursa, acha ubazazi
Jaribu kuzingatia, mpongeze miss neddy
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom