Vipepeo Weusi: Mkakati Namba 0034 (Simulizi)

Mbona una sound kama shoga? Upo sawa kweli mkuu?
Si kosa lako mkuu nimegundua hata miezi 6 humu hujatimiza,
Usijali karibu kwenye jukwaa la great thinkers tutakuelewesha na utaelewa jinsi ya kuishi na watu
8aeea45279a5665f453fe33b3ade98c9.jpg
 
Hii kazi anayofanya ndugu yetu The bold kwa kushirikiana na Nifah ni ngumu sana. Na ugumu wake unakuja pale unaowafanyia hii kazi ni Watanzania. Ndio asilimia 99 tunaosoma hii story ni Watanzania.

Em jiweke kwenye nafasi ya mwandishi hata kwa dakika moja tu. Fikiria umepatwa na dharula ukashindwa kuleta story mezani na kwa moyo mkunjufu ukaona sio vizuri wanabodi wasubiri tu bila kujua kinachoendelea. Unaamua kumtuma mtu awape taarifa, baadae ukiwa na mategemeo ya kufungua uzi na kukutana na posts za 'pole mkuu kwa dharula' unakutana na kashfa. UTAJISIKIAJE labda?

Kuna mwandishi anaitwa George Mosenya yeye sometime huwa anakatisha story na kuamua kuziuza inbox kutoka na upuuzi kama huu.

Kama kitu hulipii kashfa za nini? Hii sio oxygen kusema usipoivuta unakufa.

Tubadilike ndugu zangu, Mbona wenzetu hawapo hivi?
 
Wakuu,

Mu wazima natumai..

Kwanza mniwie radhi kwa kuwakatisha uhondo kwa siku ya leo.. Nilikuwa na changamoto fulani hivi iliyokuwa inanilazima niwe na utulivu na concentration ili kuiweka sawa!

Nashukuru kwa wale wote ambao mmeelewa na kunitakie heri changamoto ikae sawa.! Asanteni sana..

Pia, ingawa hakuna umuhimu lakini naomba pia niwajibu wale ambao walikuwa "negative" juu ya taarifa iliyoletwa na roho yangu, Nifah

Mkuu, TUJITEGEMEE, naona hii mara ya pili unatoa comment kama hii mara ya kwanza ilikuwa ni siku nilichelewa kuweka episode kwa takribani dakika 40 nje ya muda na ukakosa uvumilivu na kusema kitu kinachofanana na ulichokisema leo.. Mimi niwe wa kwanza kupingana na wazo lako kwamba nisitishe simulizi kwa wiki tatu niandike kisha nianze kutupia episode! Wazo lako haliko sawa.. Tafakari utaelewa kwanini haliko sawa..

Mkuu wise-comedian, nilitaka kuanzisha mtiti huo ugomvi wake ungetafuta pa kujificha, ila baada ya kuona comment yako ya pili, nimecheka tu nimeelewa kwanini unajiita "wise-comedian"... No hard feelings

Mkuu Fasir, aisee naomba uwe na adabu na acha kutuchafulia uzi.. Mimi huwa mvumilivu sana lakini upuuzi kama huu wako hautakiwi kuachwa bila kukemewa..
Kuwa na adabu na jitahidi kuficha upumbavu wako.. Nifah ameleta taarifa kwa nia njema tu na actually ni mimi ndiye nimemuomba alete taarifa hii.. Unapomvunjia heshima yeye unanivunjia heshima na mimi.. Tuko kwenye huu uzi kwa ajili ya burudani na labda kujifunza mawili matatu.. Huu sio uzi wa mipasho hivyo narudia tena jitahidi kuficha upumbavu wako..
Unafahamu nini kimenipata?? Nilikuwa sitaki kusema hili ila wacha nikuulize, unafahamu nani aliyeniamuru nibadili majina ya characters??
Huyo Nifah unaye mkejeli unafahamu amesimama na mimi kiasi gani katika katika masuala yangu yote katika maisha halisi huku mtaani?? Narudia tena na tena, ficha upumbavu wako na jiheshimu..

Mwisho,

Niwashukuru wote mlioelewa na kuvumilia... Na nimshukuru "cheupe wangu" Nifah kwa role kubwa anayoplay kila mahali.! Yeye ndiye aliyenishawishi niwaletee simulizi hii, sikuwa na mpango wa kuiweka humu..
She is the most awosome woman I have never seen.. Tunalia pamoja, tunacheka pamoja, na tunafanikiwa pamoja.. I'm the luckiest man on earth..

Nawashukuru sana wakuu..

Kesho jumapili mchana Episode 6 inakuwa hewani..


The Bold.
The Bold and ze Nifah :)
Haya wakuu.. tuonane kesho na poleni sana kwa yalowakuta.
 
The bold ananikumbusha riwaya za marehemu Elvis Musiba na Ben Mtobwa.
Ila kwa zama hizi yupo mkongwe Hussein Issa Tuwa, yeye anajiita bingwa wa riwaya za taharuki, yaani hapo msomaji unabaki na taharuki zisizosemeka. Mkipata nafasi tafuteni na msome riwaya zake kadhaa hamtajuta asee, nina dedicate kwenu vitabu hivi ambavyo nimeshavisoma tayari
1. Usiku wa 9/12 ( 1&2)
2. Mkimbizi
3. Mdunguaji
4. Mtuhumiwa.

Na pia story hizi sijui kama ameshatoa vitabu vyake
1. Miss Tanzania
2. Mtafiti
3. Bondia

Na sasa nipo mkao wa kula nasubiria kitabu kingine (kipo jikoni) kinaitwa "Kilio cha gaidi"
Ni hatari sana aisee.
Ni wimbo Wa gaidi na sio kilio cha gaidi
Na kwa taarifa hicho kitabu kishatoka ni kikali kweli
 
Ilipoishi Episode 5

Ray anapelekwa katika nyumba inayomilikiwa na Idara ya Usalama wa Taifa iliyopo Mbezi Beach.
Akiwa hapo anapewa maelezo kutoka kwa Waziri wa mambo ya Ndani Mhe. Charles Wangwe kuhusu shughuli na mikakati ya The Board.
Waziri Wangwe anampa mifano ya mikakati michache ya The Board na hatimaye wanafikia katika mkakati namba 0034 ambao ndio hasa lengo lao la kumuita hapo na ili waweze kumuomba asaidie juhudi za kusambaratisha umoja wa The Board.


Tuendelee….



EPISODE 6


Mhe. Wangwe akaweka faili mbele yangu na kuanza kunipa maelezo.

"Kwa taarifa ambazo tumeweza kuzikusanya mpaka sasa tuna kila sababu ya kuamini kuwa mkakati namba 0034 unalenga kuhakikisha wanachama wa The Board wana asilimia kubwa katika umiliki wa vitalu vya gesi na mafuta"

Akaacha kuongea na kutulia kidogo.

"What? Sidhani kama mko sahihi kwa kadiri ninavyo fahamu vitalu vyote vya gesi viko chini ya makampuni ya kigeni na msimamo wa Waziri wa nishati unajulikana kuwa hataki watu wa ndani ya nchi wahusike katika utafutaji na kuchimba gesi na mafuta" nikamuuliza Waziri kwa mshangao.

"Yes, Ray! That's exactly why wakaja na mkakati namba 0034"

"Mheshimiwa, ili kuepuka yote haya sioni sababu kwanini msiwaruhusu wazawa kuhusika katika kutafuta na kuchimba gesi na mafuta, sioni kama kuna ubaya wowote" nikamuuliza tena kwa mshangao.

"Of course, uko sahihi kabisa Ray! Tunapaswa kuruhusu wazawa kuhusika katika sekta ya gesi na mafuta.. But hatutaki kuwaruhusu The Board! Sijui unanielewa, tunataka kuwaruhusu wazawa lakini hatutaki kuruhusu The Board! Hawa watu hatuna imani nao, kila jambo na kila mkakati walioutekeleza umekuwa na manufaa kwao binafsi lakini hakuna manufaa kwa nchi! Kama nilivyokueleza awali hawa watu lengo lao ni kushika uchumi wa nchi na kujiongezea ushawishi katika mwenendo wa nchi! So, no Ray hatuwezi kuruhusu The Board watushinde tena akili kwenye hili." Waziri Wangwe akaongea huku ananiangalia usoni akiwa serious haswa.

"Ok! So, mnahisi mpango wao ni upi ukizingatia karibia vitalu vyote viko chini ya makampuni ya nje" nikamuuliza Waziri.

"Nitakupa mfano mmoja kukuwezesha kuelewa kuelewa angalau kiasi wanachokipanga kwenye mkakati huu 0034" Waziri Wangwe akaongea huku akikaa sawa kwenye sofa na kuinama mezani kwenye lile faili aliloliweka na kuanza kunipa maelezo.

"Nitakupa mfano wa kampuni ya Quebec Energy inayofanya utafutaji mafuta kwenye bonde la ufa kilosa na kilombero mkoani Morogoro. Kampuni hii imepewa zaidi ya hekari 440 katika sehemu ya bonde la ufa lililopita Morogoro. Walipewa licence na serikali toka mwaka 2008 na mwaka 2009 wakaanza rasmi shughuli za utafutaji mafuta. Mwaka 2013 wakapata mafanikio makubwa ya shughuli zao" Waziri Wangwe akanyamaza akatoa ukurasa mmoja kutoka kwenye faili, ukurasa huu ulikuwa unaonyesha michoro na picha za miamba.

"Hizi ni 2D sesmic data inaonyesha kwamba katika sehemu ya chini kabisa pembezoni mwa miamba ya bonde kuna vitu viko deposited" Waziri akaongea na kuweka karatasi ile chini na kuchukua nyingine.

"Hii nyingine inaonyesha data za sesmic stacking velocities kutokana na tafiti katika bonde la kilombero na kilosa data hizi zinahakikisha kuwa chini ya bonde umbali wa mita elfu tatu kwenda chini kuna miamba ya kale ya kipindi kijografia kinachoitwa Neogene-age.! Characteristics hizi ziko sawa kabisa na eneo la bonde la ufa lilipopita katika Ziwa Albert nchini Uganga ambako kumegundulowa kuwa na deposit ya karibia mapipa bilioni nne pia characteristics hizo hizo ziko sawa sawa kabisa na eneo la Lockchar nchini kenya ambako pia kimepita bonde la Ufa na kiwango kikubwa cja mafuta kimegunduliwa.! Kwahiyo tuna hakika Vitalu hivi vya Kilombero na Pangani vilivyo chini ya Quebec Energy vina kiwango kikubwa pia cha mafuta ardhini." Akaeleza Waziri Wangwe na kuendelea.

"Sasa basi, katika mikataba mingi ya utafutaji mafuta na gesi, kitalu kinakabidhiwa kwa kampuni moja lakini ndani yake kunakuwa na na makampni mawili, matatu au zaidi! Kwa maana ya kwamba kwenye kitalu kinakuwa na kampuni ambayo tunaita kuwa ni Operator, huyu ndiye anayekabidhiwa kitalu. Lakini huyu Operator anakuwa na financers! Huyu Operator yeye ndiye anayeendesha shughuli za kila siku za utafutaji kwenye kitalu na ndiye mwenye mitambo. Hawa financers wao ndio wanahakikisha kuwa kuna rasilimali fedha kwa ajili ya kuendesha zoezi zima la utafutaji mafuta"

"Sasa hawa Quebec Energy wao ndio operators wa eneo la utafutaji wa mafuta katika bonde la ufa eneo la kilombero na Pangani lakini financiers wao ni kampuni inayoitwa Matas Associates ambayo imesajiliwa katika visiwa vya Canyon Islands."
Waziri wangwe akatulia kidogo na kuniangalia.

"Tuko pamoja Ray?" Akaniuliza.

"Tuko pamoja Mheshimiwa" nikamjibu, nilikuwa niko makini kweli kweli nikisikiliza neno kwa neno, sentensi kwa sentensi.

"Ok, vizuri" akanijibu waziri huku akikaa vizuri tena kwenye sofa aendelee kunipa maelezo.
"Ray, unapaswa kufahamu kuwa katika sekta hii ya mafuta na gesi kuna ujanja mwingi sana na moja wapo ya wajanja wa kubwa ni hawa financers, ndio maana wengi wanaenda kusajili kampuni zao katika nchi ambazo zinaficha taarifa za kifedha za watu kama nchi ya Canyon Islands. Kwa taarifa tulizo nazo hawa Matas Associates ni 'shell company'! Ni kampuni ambayo iko kwenye makaratasi tu.. Tunaamini kuwa kuna mzungu mmoja mjanja akaianzisha kwa mtaji wa dola milioni moja ili aweze kuingia mkataba na Quebec Energy. Tunaamini kuwa mwaka mmoja uliopita Khalid Mohammed mmoja wa wanachama wa The Board aliinunua kampuni ya Matas Associates lakini hakununua yeye direct, alitumia mlolongo wa majina ya kampuni anazoziliki huko Oman. Na ndipo hapa mchezo mzima unaponoga." Waziri Wangwe akatulia tena kuniangalia kama tuko pamoja kisha akaendelea.

"Tunafahamu kuwa huyu aliyeanzisha Matas Associates katika mkataba wake na Quebec Energy alikubali apewe asilimia ndogo sana za ubia katika mkataba wao ndio maana hata ikawa rahisi kwa Quebec Energy kumchagua yeye kama financier na kuwaacha wengine. Lakini tunaamini kuwa lengo la mmliki wa Matas Associates ilikuwa ni kiuza kampuni yake kwa faida mara tu ikigundukika kuwa kuna deposits za mafuta huko kilombero na pangani na lengo lake hili limetimia mara baada ya Khalid Mohammed kununua kampuni yake ya Matas. Sasa usidhani kwamba Khalid na The Board ni wajinga walikuwa wanajua wanachokifanya kuwa wananunua kampuni ya kwenye makaratasi na mtaba wa kampuni hiyo na Quebec Energy unawapa asilimia chache katika ubia. Licha ya hayo yote lakini walikuwa bado na nguvu moja muhimu! Wao ndio financiers wenye jukumu la kutoa fedha shughuli ziende. Hapo ndipo walipoanza kuhujumu Quebec Energy." Waziri akachukua faili lingine na kuliweka mbele yangu.

"Nikukumbushe kitu, Quebec Energy walipewa licence mwaka 2008 na licence ilikuwa inaisha mwezi january 2016. Lakini mpaka kufika january mwaka huu 2016 walikuwa bado hawajafanikiwa kufanya drilling ya kisima ili kuhakikisha kuwa kuna mafuta kama jinsi data zilivyokuwa zinaonyesha… Ndipo hapa serikalo ikaamua kuwaongeza muda na kuwapa extension ya mwaka mmoja hadi january 2017. Lakini Miezi miwili baada ya Matas associates kununuliwa na Khalid Mohammed wakafungua kesi mahakama kuu kumshitaki mbia wao Quebec Energy. Wakatumia hoja za kipuuzi tu zilizoandikwa kwa lugha tamu za kisheria na walichokuwa wanadai ni kuwa Quebec Energy imefanya uzembe kwa kushindwa kufanya drilling ndani ya kipindi rasmi cha licence hivyo kuongeza mwaka mkoja mwingine ili kufanya drilling hii itasababisha gharama za uendeshaji kuongezeka tofauti na ilivyopangwa awali, hivyo basi katika shauri lao hilo wakawa wanaitaka Quebec Energy itoe asilimia kadhaa za ubia wake na kukabidhi kwa kampuni nyingine ili ije kuwa operator katika kipindi hicho cha extension ya mwaka mmoja ulioongezwa na serikali!" Waziri Wangwe akanichambulia kwa makini kisha akatulia kidogo kuniangalia.

"Bado tuko pamoja Ray?"

"Tuko pamoja Muheshimiwa" nikamjibu.

"OK, sasa…" Waziri akaendelea "lengo la The Board na Khalid Mohammed kupitia Matas Associates kufungua kesi ni kuinyima fedha Quebec Energy wao wakiwa kama financiers ili hatimae hatua ya drilling isifanyike na shughuli zote zikwame na Quebec Energy ipokonywe licence au isipiwe extension nyingine mara baada ya extension ya kwanza ikiisha 2017, January" Waziri akanyamaza tena kidogo nadhani alihisi kuwa nina swali.

"Whaaat?? Quebec wakipokonywa licence hii inamaanisha kuwa na Matas hawana chao tena katika utafutaji huo wa mafuta kilombero na Pangani!" Niakamuuliza kwa mshangao.

"Yes ndio maana yake" Waziri naye akanijibu kwa kifupi.

"Siku zote hizi mimi nilikuwa nahisi labda The Board wanafanya manipulation ya taarifa za utafutaji mafuta huko kilombero ili kuongeza thamani ya hisa za Quebec katika masoko duniani" nikauliza tena kwa mshangao.

"Hapana wanacholenga ni Quebec wapokonywe licence au ikifika January mwakani 2017 wasipewe extension nyingine" akanijibu Waziri Wangwe.

"Wao wananufaikaje na hili" nikauliza kwa mshangao mkubwa.

"Swali zuri sana ray!" Waziri akaanza kunijibu.

"Kumbuka nimekueleza kuwa mkakati namba 0034 tunaamini unalenga sekta ya gesi na mafuta, pia kumbuka kuwa kampuni Matas Associates iloyonunuliwa na Khalid Mohammed kwa niaba ya The Board ilikuwa na asilimia chache sana kwenye ubia wake na Quebec Energy hivyo basi tunaamini kuwa lengo kuu la The Board lillikuwa ni kufanya sabotage ili Quebec wapoteze vitalu hivi vya Kilombero na pangani ili baadae vije virudi mikononi mwa The Board kwa kutumia kampuni nyingine! Hii inawezekanaje?" Waziri akanyamaza kidogo na kukaa vyema kwenye sofa aendelee na maelezo.

"Katika nchi yetu tunaamini kuwa kuna deposits za mafuta baharini lakini ni Kilombero na Pangani pekee ndiko tunaimani kwa asilimia kubwa kuwa kuna mafuta na tunaamini hiyo ndio sababu kwanini The Board wameamua kuanza nako. Sasa nini kitafuata baada ya wao kufanya hii sabotage kwa Quebec? Duniani kuna system mbili za kutoa licence kwa kampuni za kutafuta mafuta na gesi. Kuna Bid System na kuna Grant System. Bid system inatumika hasa na nchi za ulaya ambapo kampuni zinashindana kuomba licence katika kitalu specific na kwa muda specific! Lakini sisi hapa nchini tumefuata mtindo wa nchi za kiarabu ambao ni Grant system, ambapo serikali inakuwa na orodha yake ya vitalu na makampuni yanaomba tu serikalini kuwa yanataka kufanya utafutaji mafuta na gesi kisha serikali wao ndio wanavigawanya vitalu kwa makampuni vile ambavyo serikali wao wanaona kampuni gani ikae kitalu gani na kwa muda gani!! Hii ni grant system.. Sasa endapo Quebec watapokonywa licence january 2017 maana yake viatalu vya Kilombero na Pangani vitaingizwa katika mkupuo ujao wa ugawaji vitalu.. Sasa ingesaidia kama tungekuwa na Bid System coz tungeweza tu kuyamonitor makampuni yatakayoomba vitalu vya Kilombero na Pangani na tungegundua kampuni gani nyuma yake kuna The Board! Lakini ubaya hii grant sustem ni serikali ndiyo inayopangia kampuni gani ikae kitalu gani.! Na bahati mbaya taarifa zetu za intelijensia hatujaweza kufahamu The Board wamepanga kutumia mbinu gani ili kuwachanganya serikali wagawe Kitalu cha Kilombero na Pangani kampuni wenye masilahi nayo!! Ndipo hapa sasa tunahitaji kujua mkakati 0034 kinaga ubaga.. Inabidi Tuupate kabisa wote mkononi tuusome! Na ndio sababu ya kukuita wewe hapa!" Waziri Wangwe akamaliza kunipa maelezo na kuniangalia.

"Wooooooww! Aiseeeee" nikajikuta nashindwa kupata neno la kuongea. Nikashusha pumzi na kuinamisha kichwa sekunde kadhaa nikifikiri, kisha nikainua kichwa na kumuuliza waziri;

"Kwanini msiwakamate hao wanachama wa The Board ambao mmeshawatambua na kuwahoji kwa kutumia 'mbinu' zenu ninazozisikiaga" nikamuliza waziri.

Waziri Wangwe akatabasamu, "Ray, usiamini kila unachosoma kwenye magazeti na mitandao, sisi sio watesaji! Unajua ubaya wa torture? Ukimtesa mtu kama ni muoga atakupa taarifa unayoitaka haraka tu. Lakini mwingine utamtesa mpaka anakufa hakwambii chochote! Sasa hebu imagine watu mashuhuri kama wanachama wa The Board ije kujulikana amefia mikononi mwetu hiyo skendo itakuwaje?? Si itatutafuna mpaka tuishe?? Lakini usisahau pia ukimtesa mtu anaweza kukwambia hata kile ambacho hakijui, ataropoka tu chochote ili mradi uache kumtesa! Kwa hiyo taarifa inayo patikana kwa kutesa mtu hainaga uhakika na thamani. Tunachokifanya sasa ni sawa sawa na ukimuona panya ana randa randa chumbani kwako, usifanye haraka ya kumuua! Mfatilie taratibu tu, muda si mrefu atakupeleka mpaka kwenye shimo lake na humo ndimo utawakuta mama zake, watoto zake, babu zake na ukoo wote! Hicho ndicho tunachokifanya Ray." Akaongea Waziri huku anatabasamu.

"Na Mhandisi Jaffar Kumbea anahusikaje kwenye hill?" Nikamuuliza huku nimemkazia macho.

"Hiyo ni taarifa ya ndani sana ila wacha nikupe ili tujengeane uaminifu zaidi" akaongea Waziri Wangwe huku anatabasamu zaidi.
"Mda mchache kabla ya Waziri Japhet Kipanju Kuuwawa alitoka nyumbani kwake Masaki majira ya Saa mbili usiku akaelekea moja kwa moja Mawasiliano Tower, hatujui alienda kuonana na nani ila waliomuona wanadai alifika hapo mikono nitupu ila dakika kadhaa baadae alipokuwa anapanda gari kuondoka alikuwa ameshika begi dogo la mkononi linaloonekana lilokuwa na makaratasi. Baada ya kutoka hapo akaelekea Land Mark Hotel karibu na River side ubungo. Akiwa hapo akaongea kwa takribani lisaa lizima na Mwandisi Kumbea na alipotoka hapo na kufika Ubungo akisubiri taa kumruhusu ndipo akapigwa risasi na kufariki. Like begi alilokuwa amepewa Mawasiliamo Tower, halikukutwa kwenye gari. Hivyo tunamshikiria Muhandisi kwa kuwa tunahisi anahusika na kifo hiki, au anahusika na kupotea kwa hizo nyaraka, au labda anajua kilichopo kwenye hizo nyaraka au yote matatu! Kitu pekee kitakachosaidia kuachiliwa kwake ni endapo tutazipata hizo nyaraka na kuoanisha na kile anachotuambia, tukiona kuna ukweli nasi hatutakuwa na budi kumuachia!"

"Ni kitu gani alichowaambia?" Nikamuuliza waziri haraka haraka.

"Samahani Ray hiyo taarifa siwezi kukwambia" akanijibu Waziri Wangwe huku anatabasamu.

"Ok! Nadhani tumeongea kila tulichopaswa kuongea, ni vizuri niende sasa sidhani kama kuna la ziada" nikawaeleza huku nikianza kusimama.
Nukaona wameangaliana na kupeana ishara fulani hivi kisha Baba bite akaongea.

"Hakuna shaka Ray, unaweza kwenda najua ni kiasi gani Cheupe yuko kwenye wakati mgumu kutokana na mzee wake kukamatwa kwa kesi ya mauaji na najua ni kwa kiasi gani hii inakuathiri hata wewe hivyo naomba ukumbuke kuwa kupatikana kwa haraka kwa taarifa kuhusu mkakati mzima namba 0034, au kupatikana kwa nyaraka zilizopotea kutoka kwenye gari la Marehemu Waziri Kipanju, au taarifa yoyote muhimu kuhusu The Board ndivyo itakavyo harakisha kuachiwa kwa Muhandisi Kumbea! Hivyo basi ukipata taarifa yoyote muhimu naomba tuwasiliane haraka iwezekanavyo" aliongea Baba bite huku ananipa mkono.

"Tunawasiliana vipi wakati mmesema hamtaki ijulikane kuwa nashirikiana na nyinyo" nikauliza huku tukipeana mikono na baba bite na wengine.

"Ni rahisi sana Ray, ukiwa na taarifa muhimu na unataka tuonane, nenda mpaka Mlimani City duka la Skolastika bookshop, chagua kitabu chochote cha bei ghari kisha ukienda kulipia kaunta mpe hela ndogo kama elfu tano hivi mfano na akikwambia hela haitoshi mjibibu "kuna hela yangu huku" kisha atakuacha uende.! Baada ya hapo nenda jizungushe zungushe kama nusu saa rudi umwambie akubadilishie kitabu akupe kingine kwa sababu kile labda kina kurasa zimechanika au mpe sababu yoyote ile then atakubadilishia kitabu na kukupa kitabu kingine ambacho ndani yake utakuta maelezo ni namna gani tuonane" akaniekeza Baba Bite

"Oooohh Ok.!" Nikaitikia tu kwa kifupi.

Nikaagana nao. Wakanikabidhi funguo yangu ya gari, nikatoma nje na kuwasha gari na kuondoka.



**********************


Nilikuwa nimepaki gari maeneo ya pembeni kidogo ya kituo cha fire karibu na shule ya sekondari ya jangwani. Nilikuwa hapa namsubiri Isack aje akitokea kwao pale pale karibu tu, Upanga mtaa wa Mindu. Pia nilikuwa nimempigia simu Cheupe atoke kwao Tegeta anisubiri Ubungo kwasababu inabidi turudi Morogoro! Alilalamika kweli kweli lakini uzuri Cheupe wangu anajua kunisikiliza na kilichomtuliza zaidi ni nilivyo muambia kwa kifupi tu "I have a plan".

Kichwani nilikuwa nawaza jambo moja tu ni namna gani tutamnusuru Mhandisi Jaffar Kumbea na kesi nzito iliyoko mbele yake kuhusishwa na mauaji ya Waziri mwandamizi wa serikali.
Hilo tu ndio lilisumbua akili yangu na kuninyima raha. Hata njaa nilikuwa sisikii. Akili ilikuwa imevurugika. Huo ugomvi wao wa viatalu vya mafuta haunihusu! Its a dog fight..

Niliumia sana jinsi Cheupe wangu nilipokuwa namuona akiwa kwenye maumivu mazito kutokana na jambo hili. Na si hivyo tu Mhandisi Kumbea licha ya kuwa baba mkwe wangu mtarajiwa, bali pia alikuwa ni rafiki yangu, baba yangu na mtu aliyenisaidia vitu vingi sana kwenye maisha. Sikuwa tayari Mhandisi Kumbea apokwe uhuru wake kirahisi hivi, sikuwa tayari Cheupe wangu aishi na maumivu na simanzi maisha yake yote, sikuwa tayari mimi mwenyewe kuishi na maumivu kama ninayoyasikia sasa kwa maisha yangu yote yaliyobaki. I must do something. Kwa muda huu nilijihisi kuwa nimezaliwa ili niweze kuimaliza changamoto hii pekee. Nothing else matters. Maisha ya watu wengi yako mikononi mwangu, naweza kuwanusuru. Mhandisi kumbea, hasnat, mama yake na mimi mwenyewe.

"I have a plan", nikajisemea mwenyewe tena moyoni. Ubaya ni kwamba nilikuwa na hakika hakuna ambaye angekubali nitekeleze plan hiyo. Hakuna ambaye angekubali nifanye kitu cha hatari nilichokuwa nimekipanga kichwani. Lakini sikuwa na namna nyingine!

"I have a plan" nikajisemea tena moyoni nikijipa moyo.

Mara kigari aina Vitz kikapaki karibu yangu! Isack.
Akashuka kwenye gari yake na kuingia ndani ya gari yangu. Baada ya salamu na kumpa mrejesho wa yaliyojiri kuhusu ufuatiliaji wa ishu ya Mhandisi Jaffar Kumbea Wizara ya mambo ya ndani (sikumwambia chochote kuhusu "kutekwa" kwangu na Usalama wa Taifa), nikaenda moja kwa moja kwenyd point yangu.

"Hivi kuna kifaa chochote cha kuzuia mtu asikusikie endapo amekuwekea 'bug' ya kunasa sauti nyumbani kwako au kwenye gari au kwenys nguo?" Nikamuuliza Issack

"What? Aaaahh i guess kipo aaaahh! Hey what the fu*k is going on man? Nadhani imefika mda uache kunificha kinachoendelea!!" Issack akabwata.

"Come on man, I promise nakwambia, nijibu basi hicho kifaa kipo kuzuia 'bug' iendelee kuwepo ila mtu asikusikie?" Nikamuukiza kwa msisitizo.

"Aaaahh yeah kipo! Kinaitwa aaaahh dah jina limenitoka kidogo, aaaahh kinaitwa pink noise generator! Yes, kinaitwa pink noise generator!" Akajibu Isack huku ana tabasmu baada ya kukumbuka jina.

"Ndio kinafanyaje?" Nikamuulza

"Well, aaaahh unajua vile mfano ukiwa unatafuta station ya radio alafu redio kuna mda kama 'inapiga miluzi' hivi, yes the same thing pink noise generator inaingilia frequency za ile 'bug' yule anayekusikiliza kule anakuwa anasikia kama miluzi ya redio tu sauti yako wewe haisikii hata tone!" Isack alijibu huku anatabasamu, huyu rafiki yangu anapenda sana kumuelekeza mtu jambo

"Nakipataje?" Nikamuuliza

"Well, kibongo bongo ngumu but unaweza kukinunua eBay kwa mfano, inachukua kama siku tano au sita mpaka kifike bongo" akanijibu Isack

"Ok then, agiza vinne au zaidi"

"Ok, but for what??" Akauliza kwa mshangao.

"Nimeshakwambia nitakueleza! Hilo jambo la kwanza, la pili unakumbuka Jana tumeongea kuhusj Eric Kaburu?"

"Yes nakumbuka vizuri tu"

"Ok! Nataka ukae chini utulie uchimbe historia yake, chochote utakachokipata kuanzia utotoni mpaka utu uzima.. Pia weka mkazo zaidi kwenye kesi yake ta mauaji ya mpenzi wake miaka miwili iliyopita! Chimba kila kitu kuhusu ile kesi.. Mpenzi wake ni nani, walikutanaje, kifo chake kilikuwaje, mpelelezi alikuwa nani, Jaji wa kesi alikuwa nani, mashahidi walioletwa akina nani na kadhalika! Pia chimba kuhusu kampuni yake ya Ndeshema Safaris! Kila kitu kitu utakachokipata.!" Nikamueleza haraja haraka.

"Ok, but what the fu…."

"Sijamaliza!" Nikamkatisha, "leo funga funga vitu vyako kesho uje Morogoro, na kuanzia kesho nakupa ajira rasmi Sote Hub! Congratulations!" Nikamwambia kwa utani lakini nikimaanisha..

Isack akabaki ameduwaa tu! Sijui alikuwa anafikiria nini kichwani mwake.

"Hey Isack namuwahi Cheupe Ubungo, tafadhli anza kuyafanyia kazi hayo niliyokuambia"

"Kichwa! What the fu*k is going on man?" Isack akauliza bado akiwa na mshangao.

"I have a plan! Jitahidi kesho ufike Moro mapema" nikamueleza Isack huku nikilazimisha kutabasamu nikikumbuka jinsi wazo langu lilivyo la kiwendawazimu.

Isack akatoka na kuelekea kwenye gari yake. Na mimi nikakanyaga mafuta kuelekea Ubungo kumchukua Cheupe tuanze safari ya Moro.

"I have a plan!" Nikajisema tena moyoni. Nikajipa moyo. Nikakanyaga mafuta.




Itaendelea leo saa mbili usiku..
 
NEW EPISODE (EPISODE 6) POST # 1656


Divine... glory to yhwh Nifah BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga succinate coA hydrogenase SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea Shareef Conscious wambeke The Boss deejay Nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly The Wolf Firegironsa everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Juma chief Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi @gambada YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody King Easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 Mazigazi KIDUDU buffalo44 winlicious RIZIKI ALLYS MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome StraTon MemPhis GhaZar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga haa mym KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Blaki Womani Erasto kalinga Chrizo kichakaa man kulubule FORTALEZA poleni Mshuza2 shibumi ZE DONE gkileo umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Clkey Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici T-King gkileo mij TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo Mwangungulu marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 George Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom