Wakuu,
Mu wazima natumai..
Kwanza mniwie radhi kwa kuwakatisha uhondo kwa siku ya leo.. Nilikuwa na changamoto fulani hivi iliyokuwa inanilazima niwe na utulivu na concentration ili kuiweka sawa!
Nashukuru kwa wale wote ambao mmeelewa na kunitakie heri changamoto ikae sawa.! Asanteni sana..
Pia, ingawa hakuna umuhimu lakini naomba pia niwajibu wale ambao walikuwa "negative" juu ya taarifa iliyoletwa na roho yangu,
Nifah
Mkuu,
TUJITEGEMEE, naona hii mara ya pili unatoa comment kama hii mara ya kwanza ilikuwa ni siku nilichelewa kuweka episode kwa takribani dakika 40 nje ya muda na ukakosa uvumilivu na kusema kitu kinachofanana na ulichokisema leo.. Mimi niwe wa kwanza kupingana na wazo lako kwamba nisitishe simulizi kwa wiki tatu niandike kisha nianze kutupia episode! Wazo lako haliko sawa.. Tafakari utaelewa kwanini haliko sawa..
Mkuu
wise-comedian, nilitaka kuanzisha mtiti huo ugomvi wake ungetafuta pa kujificha, ila baada ya kuona comment yako ya pili, nimecheka tu

nimeelewa kwanini unajiita "wise-comedian"... No hard feelings
Mkuu Fasir, aisee naomba uwe na adabu na acha kutuchafulia uzi.. Mimi huwa mvumilivu sana lakini upuuzi kama huu wako hautakiwi kuachwa bila kukemewa..
Kuwa na adabu na jitahidi kuficha upumbavu wako..
Nifah ameleta taarifa kwa nia njema tu na actually ni mimi ndiye nimemuomba alete taarifa hii.. Unapomvunjia heshima yeye unanivunjia heshima na mimi.. Tuko kwenye huu uzi kwa ajili ya burudani na labda kujifunza mawili matatu.. Huu sio uzi wa mipasho hivyo narudia tena jitahidi kuficha upumbavu wako..
Unafahamu nini kimenipata?? Nilikuwa sitaki kusema hili ila wacha nikuulize, unafahamu nani aliyeniamuru nibadili majina ya characters??
Huyo
Nifah unaye mkejeli unafahamu amesimama na mimi kiasi gani katika katika masuala yangu yote katika maisha halisi huku mtaani?? Narudia tena na tena, ficha upumbavu wako na jiheshimu..
Mwisho,
Niwashukuru wote mlioelewa na kuvumilia... Na nimshukuru "cheupe wangu"
Nifah kwa role kubwa anayoplay kila mahali.! Yeye ndiye aliyenishawishi niwaletee simulizi hii, sikuwa na mpango wa kuiweka humu..
She is the most awosome woman I have never seen.. Tunalia pamoja, tunacheka pamoja, na tunafanikiwa pamoja.. I'm the luckiest man on earth..
Nawashukuru sana wakuu..
Kesho jumapili mchana Episode 6 inakuwa hewani..
The Bold.