BANDOKITITA
JF-Expert Member
- Oct 4, 2022
- 1,616
- 2,983
Inaskitisha km siyo kuhuzunisha, kuona kiongozi anaeongoza kundi kubwa la wasomi tena wengine waliomzidi umri na elimu kuongea mbele za watu km muwindaji wa porini alieamua maisha yake ayamalizie kukimbizana na wanyama au ndege.
Siku ya MAY MOSI ni siku ya wafanyakazi kueleza mbele ya kiongozi wa serikali changamoto na matatizo wanayokumbana nayo sehemu ya kazi kwa kuomba kusaidiwa kutatuliwa. Miongoni mwa mambo hayo ni kuomba kuboreshewa maslahi, kuongeza vitendea kazi na watendaji kazi. Pia ku address kero mbali kutoka kwa viongozi wanaowaongoza wafanyakazi sehemu zao za kazi nk.
Lakini MAY MOSI ya mwaka huu 2025 imeskitisha sn kuona kiongozi wa TUCTA alitoa ombi la HOVYO ambalo halijawahi kuombwa na kiongozi yeyote wa TUCTA. Hivi hawa viongozi wa wafanyakazi wanajua kuwa wanaongoza wasomi na siyo kondoo. Je aliyoongea huyu kiongozi wa TUCTA ndo kero na mahitaji ya wafanyakazi. Je aliyoongea alitumwa na wafanyakazi au alitumwa na matawi yao yanayoneemeka na POSHO na mishahara minono wanayojichotea kutoka kwenye makato ya mishahara ya wafanya kazi.
Yani kiongozi unaonba kusiwepo tena vyama vya wafanyakazi!!! Serious, kweli. Kwa hiyo anaona vyama hivyo vinakuja ku challenge ulaji wao. Hivi hiyo sheria ya kuzuia kusajiliwa vyama vya wafanyakazi aliisoma wapi na kutoka katiba ipi ya Jamhuri ya Muungano wa Tz.
Hivi hawa wanaojiita viongozi wa wafanyakazi huchaguliwa kweli kihalali na wafanyakazi au hujiteua kupitia mlango haramu wa rushwa.
Siku ya jana ndo wafanyakazi wamejua rangi zenu halisi. Ndo maana kwenye vyombo vya ulinzi na usalama hakuna ujinga unaoitwa VYAMA VYA WAFANYAKAZI au UMOJA WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI. Maana kwa Tz vyama vya wafanyakazi ni chaka la upigaji na uwepo wa MAPANDIKIZI YA WATAWALA.
WITO:
Viongozi wa wafanyakazi siku ya MAY MOSI ongea mambo mliyoagizwa na wafanyakazi wenzenu mnaokusanya makoto kutoka kwenye mishahara yao na siyo kujifungia viongozi peke yenu chumbani na kuja na hisia zenu mbele ya mgeni rasmi.
Pia, viongozi wa wafanyakazi acheni kutanguliza matumbo na matakwa yenu mbele na kusahau wafanyakazi wanaowalipa mishahara. Mfano jana mlikomaa na POSHO ZISIKATWE KODI. Hivi ni wafanyakazi wangapi wanaonufaika na hizo POSHO km siyo nyie MABWANYENYE.
MWISHO.
Nyie ni wafanyakazi wa umma au binafsi, acheni tabia za wanasiasa za kuongea uongo na kujipendekeza kwa mamlaka za serikali. Kwa kufanya hivyo hamtaweza kutetea haki za wafanyakazi wenzenu bali kushibisha matumbo yenu. Or else nyie ni MAPANDIKIZI.
Nimemaliza: Said, BANDOKITITA