Viongozi wa Tanzania mnaishi nchi gani ambapo hamuathiriwi na gharama za maisha?

nyumba-serikali.
chakula-serikali.
umeme-serikali.
maji-serikali.
usafiri wa kifahari na gharama zake-serikali
matibabu-serikali
starehe-serikali

walioweka haya walikuwa na nia nzuri sana ili kiongozi atulize akili katikakutatua changmotl tu,ila hawa panya wanaona ni kama watu waliobarikiwa kula mpaka wanajiongezea nyingine bila uoga.
 
nyumba-serikali.
chakula-serikali.
umeme-serikali.
maji-serikali.
usafiri wa kifahari na gharama zake-serikali
matibabu-serikali
starehe-serikali

walioweka haya walikuwa na nia nzuri sana ili kiongozi atulize akili katikakutatua changmotl tu,ila hawa panya wanaona ni kama watu waliobarikiwa kula mpaka wanajiongezea nyingine bila uoga.
Siasa tamu
 
Kati ya vitu ninavyoshindwa kuelewa ni kama hili suala.

Naombeni kwanza mniambie mimi mwananchi wetu sehem gani au ni mkoa gani ambao mmejitenga wenyewe

Maana haiwezekani wananchi wenu gharama ya maisha inapanda kiasi hiki alafu mnakuja mnajitokeza mnatoa majibu mepesi kwa vitu ambavyo vinawagharimu wananchi wenu,

Ina maana kama msoto huu unaoendelea hapa nchini tungekuwa tunakula wote, na kuishi wote mngejua namna ya kumsaidia mwananchi wenu,

Vitu vinapanda ovyo ovyo alafu anajitokeza kamtu kamoja kanaanza kusema, uchumi umeyumba kwenye nchi za wenzetu ndio maana haya yanatokea, hivi akili zenu zipo sawa.

Mara paah miujiza ya Mungu hiyoo Tanzania imehamia Jupiter au Mars na mpo wenyewe huko yaani watz tu sayari nzima hakuna nchi jirani wala misaada ya wahisani, Mngechukua hatua gani kuongoza nchi yenu?

Kiufupi hamtendi haki kazi kupeana vyeo ambavyo hata sioni vinamsaidia nini mwananchi ambaye saizi analia na mbolea, analia na mafuta,

Mnashindwa hata kuiga mifano nchi za wenzetu, kazi tu miradi ya kimkakati, mwananchi hoi nyie mpo tu

Wao wanakula kwa urefu wa kamba zao huo ugumu wa maisha atausikiaje
 
Mkuu madelu ameshasema sera za nchi zipo vizuri huku akiwa kajificha kwenye kichaka cha vita ya Ukraine........kwa hiyo usitarajie chochote cha maana kutoka kwa aina ya hawa viongozi wa kutafuta vichaka vya kujificha.
 
hakuna anaenyanyua mdomo kulijadili hili

wao kazi kujisemelesha ovyo kwenye media
 
Mkuu viongozi hawaishi maisha yetu. Hawajui na wala hawawezi kujua struggle zetu.

Nyumba bure, usafiri bure, umeme, maji, simu, internet, houseboy, housegirl, hata wakipumua wanalipwa posho ya usumbufu....

Ni kweli viongozi wa nchi hawaishi maisha kama ya wananchi wao hivyo hawajui mateso wanayopata kutokana na mfumuko wa bei!! Wananchi wanalalamika, lakini anakuja kiongozi anatoa majibu mepesi mepesi tu kuwa hakuna Jinsi kwani hali hiyo ni kwa Dunia nzima!!! Haya sio Majibu ya kiongozi anayejitambua na ana uchungu wa Jinsi wananchi wanvyopata taabu. Nimesikitishwa sana na maelezo ya Waziri wa fedha kuhusu mfumuko wa bei nchini na jinsi ya kuuthibiti ili kuwasaidia watu hasa wa kipato cha chini. Kumbukeni kwa mfano waajiriwa mshahara haujapanda kwa muda mrefu lakini bei za bidhaa zinapanda kila leo hivyo maisha yao lazıma yaathirike!
 
Back
Top Bottom