Kiwi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 1,054
- 990
Nimesikia kichefuchefu baada ya kusikia kwenye taarifa ya habari ya ITV usiku huu kauli za kejeli na dharau isiyoweza kuvumilika kwa wananchi wa Mtwara.
Mbunge wa Sumve Mh. Ndassa - 'watu wa Mtwara hawana uwezo wa kufikiria na kufanya mambo kama waliyoyafanya leo. Kuna mtu anayewasukuma'.
Suleiman Zedi Mbunge (sikumbuki jimbo lake) - 'watu wa Mtwara waelimishwe ili waelewe'.
jk 'serikali imechoshwa na vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani na itawashughulikia watu wote wa Mtwara waliohusika na vurugu za leo'.
Kauli zote hizi maana yake ni moja: Wananchi wa Mtwara hawana akili za kufikiria, wanapaswa kuelimishwa ili waelewe na kukubaliana na matakwa ya serikali; wasipokubali kutii basi washughulikiwe ipasavyo. Hii ni dhana iliyopitwa na wakati. Ni mawazo ya kikoloni yasiyostahili kuwepo kwenye serikali ya nchi inayojiita 'huru, ya kidemokrasia na sikivu'.
Ninawalilia wananchi wa Mtwara, ninaililia nchi yangu Tanzania. Wapi tulipopotea hadi 'vinyago' hivi vikaingia madarakani?
Mungu Ibariki Tanzania!
Mbunge wa Sumve Mh. Ndassa - 'watu wa Mtwara hawana uwezo wa kufikiria na kufanya mambo kama waliyoyafanya leo. Kuna mtu anayewasukuma'.
Suleiman Zedi Mbunge (sikumbuki jimbo lake) - 'watu wa Mtwara waelimishwe ili waelewe'.
jk 'serikali imechoshwa na vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani na itawashughulikia watu wote wa Mtwara waliohusika na vurugu za leo'.
Kauli zote hizi maana yake ni moja: Wananchi wa Mtwara hawana akili za kufikiria, wanapaswa kuelimishwa ili waelewe na kukubaliana na matakwa ya serikali; wasipokubali kutii basi washughulikiwe ipasavyo. Hii ni dhana iliyopitwa na wakati. Ni mawazo ya kikoloni yasiyostahili kuwepo kwenye serikali ya nchi inayojiita 'huru, ya kidemokrasia na sikivu'.
Ninawalilia wananchi wa Mtwara, ninaililia nchi yangu Tanzania. Wapi tulipopotea hadi 'vinyago' hivi vikaingia madarakani?
Mungu Ibariki Tanzania!