Vipi kuhusu kejeli kwenye lile tamko la Maaskofu kuwa Kanisa lilifunga mkataba wa MoU na serikali ya Ujerumani na serilali ya Tanzania ilihusishwa kama observer tu?
Ndani ya MOU ninavyoelewa serikali ilitakiwa isitaifishe mali za kanisa kama ilivyokuwa imefanya hapo mwanzo, na hatimaye ikashindwa kuendesha hizo hospitali. Ujerumani ikakubali kuendelea kusupport hospitali kama serikali ya Tanzania haitataifisha tena. Badala ya kujitoa moja kwa moja katika suala la tiba kwa raia wake, ambao hawana Hospitali mfano Waislamu. Serikali ikakubaliana na makanisa yatoe huduma, na serikali itoe wafanya kazi na mishahara na madawa ili raia wote watibiwe sawa. Kumbuka wanaotibiwa ni raia, wawe ni wakristo au waislamu na wapagani wote ni raia, serikali inawajali kwa kukubaliana na Hospitali za wakristo zilizopo. Je, kama serikaliitaacha kutoa ruzuku na hospitali zikatoza gharama za juu, wewe utatibiwa wapi? Serikali itakapokuwa imejenga hospitali zake haitakuwa haja na MOU. Nanyi jengeni Hospitali zenu mtaingia kwenye MOU.