Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Kuelekea kwenye Zoezi la uchaguzi Mkuu wa Tanzania Jumatano ya Oktoba 29, 2025, Viongozi wa dini, kijamii pamoja na wananchi wa Mkoa wa Dodoma wameungana pamoja kuhimiza amani, wakiitaja kama rasilimali muhimu kwa maendeleo ya Kijamii, kiuchumi, Viongozi wa dini wakisema amani ndiyo Neema muhimu zaidi kwenye nchi yoyote duniani.
Mchungaji Pendo Yohana kutoka Kijiji cha Michese, Askofu Antony Saimon, Mwenyekiti wa Umoja wa madhehebu ya Kikristo Mkoa wa Dodoma pamoja na Sheikh Ahmed Said Ahmed, Msemaji wa Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, ni miongoni mwa Viongozi wa dini wanaohamasisha kuhusu amani, wakisisitiza kila Mtanzania kuwa Mlinzi wa amani na kujiepusha na matendo yote yenye kuhatarisha amani iliyopo.
Mchungaji Pendo Yohana kutoka Kijiji cha Michese, Askofu Antony Saimon, Mwenyekiti wa Umoja wa madhehebu ya Kikristo Mkoa wa Dodoma pamoja na Sheikh Ahmed Said Ahmed, Msemaji wa Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, ni miongoni mwa Viongozi wa dini wanaohamasisha kuhusu amani, wakisisitiza kila Mtanzania kuwa Mlinzi wa amani na kujiepusha na matendo yote yenye kuhatarisha amani iliyopo.