GE2025 Viongozi wa Dini na Wananchi Dodoma wasisitiza umuhimu wa Amani kwa Maendeleo ya Taifa

GE2025 Viongozi wa Dini na Wananchi Dodoma wasisitiza umuhimu wa Amani kwa Maendeleo ya Taifa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
Kuelekea kwenye Zoezi la uchaguzi Mkuu wa Tanzania Jumatano ya Oktoba 29, 2025, Viongozi wa dini, kijamii pamoja na wananchi wa Mkoa wa Dodoma wameungana pamoja kuhimiza amani, wakiitaja kama rasilimali muhimu kwa maendeleo ya Kijamii, kiuchumi, Viongozi wa dini wakisema amani ndiyo Neema muhimu zaidi kwenye nchi yoyote duniani.

Mchungaji Pendo Yohana kutoka Kijiji cha Michese, Askofu Antony Saimon, Mwenyekiti wa Umoja wa madhehebu ya Kikristo Mkoa wa Dodoma pamoja na Sheikh Ahmed Said Ahmed, Msemaji wa Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, ni miongoni mwa Viongozi wa dini wanaohamasisha kuhusu amani, wakisisitiza kila Mtanzania kuwa Mlinzi wa amani na kujiepusha na matendo yote yenye kuhatarisha amani iliyopo.

 
AMANI WAKATI SERIKALI INATEKA WATU WEWE NDUGU YAKO ATEKWE WEWE UWE NA AMANI
 
Back
Top Bottom