Viongozi wa CHADEMA wanapotosha Umma zuio la mahakama kutofanya siasa Linaendea

Viongozi wa CHADEMA wanapotosha Umma zuio la mahakama kutofanya siasa Linaendea

Troll JF

Platinum Member
Joined
Feb 6, 2015
Posts
9,277
Reaction score
13,703
VIDEO:

Siku chache baada ya viongozi waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA @ChademaTZ2) wakiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala Rugemeleza kuutangazia umma kuwa zuio la Mahakama Kuu lililokuwa limetolewa Juni 10.2025 likipiga marufuku chama hicho kuendelea na shughuli zote za kisiasa na kiutendaji hadi hapo kesi ya msingi inayohusu usawa kwenye 'mgawanyo wa mali' itakapotolewa maamuzi, hatimaye tamko hilo la CHADEMA limepingwa rasmi

Wakili Gido Semfukwe anayeongoza jopo la Mawakili wa waleta maombi (aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Saidi Issa Mohamed na wenzake wawili) kwenye, amejitokeza mbele ya Waandishi wa Habari na kukanusha vikali tamko la chama hicho, sambamba na kutoa wito kwa umma kupuuza kile alichokiita ni 'upotoshaji wa makusudi' unaofanywa na viongozi wa CHADEMA

"Amri ya Mahakama inapotolewa inakuwa halali na kuzifunga pande zote husika, pamoja na umma kwa ujumla kutegemea na muktadha wa shauri lenyewe mpaka ambapo amri hiyo itatenguliwa na Mahakama yenye mamlaka, pia tunachukua fursa hii kurejea amri husika (amri namba 2, ukurasa wa 20) kutoka maombi madogo Na. 8960/2025 ambayo ilieleza kinagaubaga kuwa mazuio haya ni ya kudumu hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa maamuzi" -Wakili Gido

Aidha, Wakili huyo kutoka Hyperion Legal & Corporate Consultant ametoa rai kwa makada wa CHADEMA na Watanzania kwa ujumla wake kujiepusha na upotoshaji unaofanywa na viongozi wao na kuacha kujihusisha na uvunjwaji wa sheria za nchi, kwani matamko hayo yapo kinyume na sheria na yanatazamiwa kuhamasisha, kuvunja na kudharau amri za Mahakama ikiwa ni mkakati wa kupima uwezo wa vyombo vya Dola katika kutimiza utawala wa sheria na utekelezaji wa amri halali za Mahakama.
 
VIDEO:

Siku chache baada ya viongozi waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA @ChademaTZ2) wakiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho Wakili Dkt. Rugemeleza Nshala Rugemeleza kuutangazia umma kuwa zuio la Mahakama Kuu lililokuwa limetolewa Juni 10.2025 likipiga marufuku chama hicho kuendelea na shughuli zote za kisiasa na kiutendaji hadi hapo kesi ya msingi inayohusu usawa kwenye 'mgawanyo wa mali' itakapotolewa maamuzi, hatimaye tamko hilo la CHADEMA limepingwa rasmi

Wakili Gido Semfukwe anayeongoza jopo la Mawakili wa waleta maombi (aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Saidi Issa Mohamed na wenzake wawili) kwenye, amejitokeza mbele ya Waandishi wa Habari na kukanusha vikali tamko la chama hicho, sambamba na kutoa wito kwa umma kupuuza kile alichokiita ni 'upotoshaji wa makusudi' unaofanywa na viongozi wa CHADEMA

"Amri ya Mahakama inapotolewa inakuwa halali na kuzifunga pande zote husika, pamoja na umma kwa ujumla kutegemea na muktadha wa shauri lenyewe mpaka ambapo amri hiyo itatenguliwa na Mahakama yenye mamlaka, pia tunachukua fursa hii kurejea amri husika (amri namba 2, ukurasa wa 20) kutoka maombi madogo Na. 8960/2025 ambayo ilieleza kinagaubaga kuwa mazuio haya ni ya kudumu hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa maamuzi" -Wakili Gido

Aidha, Wakili huyo kutoka Hyperion Legal & Corporate Consultant ametoa rai kwa makada wa CHADEMA na Watanzania kwa ujumla wake kujiepusha na upotoshaji unaofanywa na viongozi wao na kuacha kujihusisha na uvunjwaji wa sheria za nchi, kwani matamko hayo yapo kinyume na sheria na yanatazamiwa kuhamasisha, kuvunja na kudharau amri za Mahakama ikiwa ni mkakati wa kupima uwezo wa vyombo vya Dola katika kutimiza utawala wa sheria na utekelezaji wa amri halali za Mahakama.
Umelogwa
 
 
Kwa nini faschists wa Zanzibar wanapenda kuwatumia mawakili wenye uwezo mdogo wa akili na maarifa?Msomi wakili Regemeleza alieleza wazi kwa mantiki na rejea za maamuzi mbalimbali ya mahakama kuu kuhusu zuio lolote. Hiyo ni general rule. Halafu huyu wakili bwege wa hao maruhani wa Zanzibar anapiga blah blah za kisiasa bila ya rejea yoyote ya kisheria!!
 
Kwa nini faschists wa Zanzibar wanapenda kuwatumia mawakili wenye uwezo mdogo wa akili na maarifa?Msomi wakili Regemeleza alieleza wazi kwa mantiki na rejea za maamuzi mbalimbali ya mahakama kuu kuhusu zuio lolote. Hiyo ni general rule. Halafu huyu wakili bwege wa hao maruhani wa Zanzibar anapiga blah blah za kisiasa bila ya rejea yoyote ya kisheria!!
Kiufupi Nshala huwa hakurupuki!!
 
Kiufupi Nshala huwa hakurupuki!!

Nshala Rugemeleza ni wakili msomi hasa, mwenye uelewa mkubwa wa masuala ya kisheria na mwenye umakini wa hali ya juu katika kila jambo la kisheria na kimahakama, siyo kama hao mawakili wa mchongo. Mawakili hopeless kabisa ni wa mawakili wa Serikali, hao hutegemea sana kubebwa na mahakimu/majaji wa mchongo ili kupata ushindi. Ndiyo maana wakienda kwenye mahakama za kimataifa ambazo majaji hawategemei kutoa uamuzi kwa kupigiwa simu na watawala, huwa wanafeli vibaya sana.
 
Nshala Rugemeleza ni wakili msomi hasa, mwenye uelewa mkubwa wa masuala ya kisheria na mwenye umakini wa hali ya juu katika kila jambo la kisheria na kimahakama, siyo kama hao mawakili wa mchongo. Mawakili hopeless kabisa ni wa mawakili wa Serikali, hao hutegemea sana kubebwa na mahakimu/majaji wa mchongo ili kupata ushindi. Ndiyo maana wakienda kwenye mahakama za kimataifa ambazo majaji hawategemei kutoa uamuzi kwa kupigiwa simu na watawala, huwa wanafeli vibaya sana.
Maana Nshalah kafanya rejea za mahakama ya juu ya hiyo ya huyo Jaji wa Zanzibar anayeifanya kesi iliyofunguliwa kwa hati ya dharula iendeshwe kikawaida!
 
Back
Top Bottom