SCOOBY DOO
Member
- Dec 16, 2013
- 76
- 69
CHAMA CHA DEMOKRASI NA MAENDELEO MKOA WA MARA KINAWAFAHAMISHA KUWA WAFUATAO WAMESIMAMISHWA NAFASI ZA UTENDAJI WA CHAMA WILAYA YA BUNDA KUANZIA TAREHE 15/08/2015
1. ALFRED SAMWEL IMANANI - MWENYEKITI WA JIMBO BUNDA
2. RITHA SALVATORY IKANDILO - KATIBU WA WILAYA
3. EMMANUEL MACHUMU MARIBWA - MWENEZI JIMBO
4. DAMAS KUNJU - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
5. MWITA NG'WENA - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
6. DICKSON KUJELWA - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
7. DAVID ARBOGAST - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
8. JUMANNE D. MOSSY - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
9. NOAH LAWRENCE - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
10. JACTON MUYENGI - MJUMBE WA KAMATI TENDAJI JIMBO
11. MATALA ATHUMANI - KATIBU BAVICHA KATA SAZIRA
SABABU ZA KUSIMAMISHWA KWAO NI:
1. Kumpiga na kumjeruhi sana aliyekuwa mtia nia wa jimbo la Bunda Mjini Ndugu Chacha Nyamhanga ambaye alilazwa kwa muda wa siku tisa katika Hospitali ya Wilaya ya Bunda. Sababu za kumpiga mtia nia huyo ni baada ya kukataa kutoa rushwa na kuhamasisha wenzake wasitoe rushwa kwa viongozi hao.
2. Kuhujumumatokeo ya kura za maoni kwenye kata zaNyamuswa, Nyamakokoto, Nyasura, Manyamanyama na kufanya vikao vya uteuzi wa madiwani nje ya ofisi bila vikao vya kikatiba ili kuifanya CCM ishinde kata zote za Wilaya ya Bunda, mfano; kwenye kata Nyamakokoto walimteua ndugu EMMANUEL MALIBWA aliyepata kura 5 badala ya ndugu GEORGIES MIYAWA aliyeshinda kwa kura 37, Kata ya Nyasura aliteuliwa Jumanne Mosi aliyepata kura 17 na akaachwa Mwamba Wasira aliyepata kura 47.
3. Kuiba mihuri ya Ofisi kwa lengo la kugushi nyaraka za chama.
4. Kuwataka wagombea wa nafasi za udiwani kutoa rushwa ya kiasi cha shilingi laki tano ili waweze kuteuliwa na kamati tendaji kama wagombea wa nafasi hizo.
5. Kuwasiliana na mgombea ubunge wa CCM Ndugu Steven Wasira kwa lengo la kuhujumu Chama ili mgombea huyo kutoka CCM apite bila kupingwa.
6. Mwenyekiti wa Jimbo na aliyekuwa mtia nia wa ubunge Ndugu Ismail Pius Masululi amekuwa na mawasiliano na Mkuu wa Wilaya ya Bunda Ndugu Mirumbe kwa lengo la kuhujumu chama.
7. Matumizi mabaya ya fedha za chama.
IMETOLEWA NA
KATIBU WA MKOA MARA