DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Baadhi ya viongozi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Geita Mjini mkoani Geita wameeleza kusikitishwa kwao na namna mchakato wa kura za maoni za kupata wagombea ubunge na madiwani ulivyokwenda huku wakidai kugubikwa na rushwa kwa baadhi wagombea na wajumbe.
Wakizungumza na JAMBO TV kwa nyakati tofauti baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho wamedai baadhi ya watia nia walionekana wakitoa rushwa ya fedha na vitenge kwa wajumbe hali ambayo imeibua wasiwasi juu ya uhalali wa wagombea hao huku wakiomba viongozi ngazi za juu kuingilia kati.
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita, Michael Msuya mbali na kutotaka kuzungumzia suala hilo amedai chama kina utaratibu wake hivyo mwenye malalamiko awasilishe.
Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, James Ruge akizungumza kwa njia ya Simu na JAMBO TV amekiri kupokea malalamiko na kuyafanyia kazi huku akiahidi kutoa taarifa kamili Agosti 13, 2025.
Wakizungumza na JAMBO TV kwa nyakati tofauti baadhi ya viongozi na wanachama wa chama hicho wamedai baadhi ya watia nia walionekana wakitoa rushwa ya fedha na vitenge kwa wajumbe hali ambayo imeibua wasiwasi juu ya uhalali wa wagombea hao huku wakiomba viongozi ngazi za juu kuingilia kati.
Akizungumza kwa njia ya simu Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Geita, Michael Msuya mbali na kutotaka kuzungumzia suala hilo amedai chama kina utaratibu wake hivyo mwenye malalamiko awasilishe.
Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, James Ruge akizungumza kwa njia ya Simu na JAMBO TV amekiri kupokea malalamiko na kuyafanyia kazi huku akiahidi kutoa taarifa kamili Agosti 13, 2025.