akiongea kwa kiswanglish cha ki-teenager, (si unajua namna huwa wanatamka L zao) violet mzindakaya ameweka wazi vitu wanakavyoviongea kesho Jangwani amesema watanzania kwa muda mrefu wamekua wakidanganywa kwamba wao ndio wana maisha magumu wakati dunia nzima hali ya uchumi ni ngumu, sasa wanataka kutumia nafasi ya mkutano wa kesho kuwaambia watanzania ukweli, wanataka watanzania watambue hali ya maisha ni ngumu si tu tanzania ila hata sehemu nyingine duniani tofauti na wanavyodanganywa na wapinzani hasa CHADEMA.
Mithali 17:20
Hata mpumbavu akinyamaza, huhesabiwa hekima;
Akifumba midomo yake, huhesabiwa ufahamu.
Ingawa heading ya thread na kilichoandikwa naona ni tofauti, anyways.... Tanzania ni moja ya nchi 5 masikini duniani, hata hilo nalo ni la kubisha?? Waende zao bhana!
Si kila sehemu duniani ina Gold, Tanzanite, Diamond, Nickel, Uranium, gas, oil, misitu, Mbuga za wanyama, bahari, maziwa, mito, Mt Kilimanjaro, arable land. Si kila sehmu duniani utakuta serikali yake inatumia 38% ya National budget kununulia magari ya kifahari kwa ajili ya wakubwa wachache! Si kila sehemu duniani utakuta serikali inafanya mazungumzo na wezi - grand thefts! Si kila mahali.
Ni mtoto wa FISADI Chrisantus Mzindakaya, yule mbunge aliyekuwa mchawi sana kiasi kwamba hakuna mtu alikuwa anasubutu kugombea Ubunge. Yule ambaye ili kuwaonesha wapiga kuwa kuwa ana nguvu za kichawi alitundika koti hewani. Hebu funga macho halafu uone ni kwa jinsi gani unaweza rusha koti hewani likabaki limening'ia!!! Nafikie pia alitumika kupata ile juju uliyommaliza yule mtu alikuwa anapinga masuala fulani na akafa na tukasikitika wengi!!!!!!!! So sad!!! Ukimwoa huyu umeoa uchawi!!
asigwa you have made my day nimecheka sana best. so she has nothing to tellhawa watoto wa vigogo walio kulia nje ya nchi unapozungumzia maisha magumu kwao huwa ni KUKOSA HELA YA KUBADILI LOSHENI ya kupaka usoni..au kunywa chai isiyo na maziwa hasubui asubuhi ...
hawajui kuwa kuna mtu huwa anakosa hata buku mbili ya kung'oa jino hospitali inabidi akimbilie kanisani akaomewe
SHAME ON THEM
Kama mlikuwa mnadhani kuna kijana mwenye akili timamu bado yupo CCM basi mmekosea sana. Angalieni jinga lingine hili hapa.
Cyprian Majura Musiba
KESHO CCM JANGWANI KUWAONYESHA WATAALAM WA KUPOTOSHA CHADEMA KWAMBA BILA CCM NCHI ITAYUMBA..KWENYE MSAFARA WA MAMBA HATA KENGE WAMO..
KENGE NI VYAMA VYA SIASA KIKIWEMO CHADEMA
CHADEMA WATASHANGAA UWANJA WA NYUMBANI WA CCM JANGWANI UTAKAVYOFURIKA
VUA GAMBA,VUA GWANDA..VAAAAAA UZALENDO HALISI
ATAKUWEPO MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI AMBAYE PIA NI RAIS WA TANZANIA MHE.JAKAYA MRISHO KIKWETE.
WATAKUWEPO MABALOZI WA NCHI MBALIMBALI
DK SLAA KURUDI CCM RASMI KESHO KWA KISHINDO JANGWANI BAADA YA KUSHINDWA KUELEWANA NA MWENYEKITI WAKE FREEMAN MBOWE KWA MUDA SASA.
DK SLAA ATAAMBATANA NA VIONGOZI KADHAA WAANDAMIZI WA CHADEMA
Si kila sehemu duniani ina Gold, Tanzanite, Diamond, Nickel, Uranium, gas, oil, misitu, Mbuga za wanyama, bahari, maziwa, mito, Mt Kilimanjaro, arable land. Si kila sehmu duniani utakuta serikali yake inatumia 38% ya National budget kununulia magari ya kifahari kwa ajili ya wakubwa wachache! Si kila sehemu duniani utakuta serikali inafanya mazungumzo na wezi - grand thefts! Si kila mahali.
kwenye hayo mabano ndo yumo huyo anaetembea na mke wa mtu? umetumia kigezo gan kubuni?Mwenye haki ni yule ambae anatembea na mke wa mtu kinyume na mafundisho ya Mungu wa kitabu chochote kile?
..aache uongo!!
..sisi tuliokula chumvi tunajua uongo na visingizio vya CCM tangu zamani.
..kwanza walikuwa wanasingizia kuvunjika kwa jumuiya ya afrika mashariki.
..baadaye wakaja na visingizio vya vita vya Kagera.
..wakasema kuna wahujumu uchumi na walanguzi.
..baadaye wakadai hakuna fedha za kigeni.
..wakaja wakadai ni masharti magumu ya IMF na WB.
..kupanda kwa bei ya mafuta ktk soko la dunia.
..wakasema tunafunga mikanda kulipa madeni ya nje.
..halafu ukaja mtikisiko wa uchumi wa dunia.
..TANGU CCM IANZISHWE IMEKUWA NI VISINGIZIO TU. SASA TUMEAMUA KUWATOA MADARAKANI.
rwanda wanasonga mbele hawana resources kama sisi wao wapo dunia gani?mwaka 1990 tulikua sawa kila kitu na singapore
...mkuu, nakuhakikishia kuwa hapa umenisisimua si vidogo! Koti linaning'inia hewani!? You cannot beat those nyinyiM and you definitely cannot join them. Mkuu lakini wengi utakuwa umetuacha gizani. mimi umeniacha gizani. Hii ilikuwa wapi na lini? na huyu mkuu aliyemalizwa kwa kupinga masuala fulani ni yule wa mwaka 1984 kati katiya Dom na Mor?