Tanzaniaist
Senior Member
- Nov 29, 2011
- 161
- 156
Inawezekana huu mwaka wa 2012 ndio mwisho wa Ben Mkapa kisiasa na hata ndio mwanzo wa kuporomoka kwa umaarufu na heshima miongoni wa Watanzania..,Ben Mkapa ulikuwa mwiba mkali uliowashinda Agustino Mrema,Ibrahim Lipumba,James Mbatia lakini kijana mdogo toka kule Musoma Mh.Vincent Nyerere ameweza kuumeza mfupa uliowashinda wapinzani wengi baada ya kumpa Ben Mkapa vidonge stahiki wakati wa Kampeni Arumeru hadi kufikia hatua ya kuhaha kwa ndugu wa nyerere kuomba msamaha...! Namfananisha Vincent Nyerere na David aliyemwangua Goliath (ben mkapa) kwenye mapambano..., Nafikiri kazi aliyekuwa nayo sasa hv Ben Mkapa ni kurudi tu kijijini kwao Mtwara kufanya shughuli za kilimo kama wastaafu wenzake..Baada ya kupata mbabe wake kwenye uringo wa siasa