Miwatamu
JF-Expert Member
- Oct 2, 2012
- 1,450
- 487
Kama kawaida yangu napenda thread zangu zijikite sana katika kutengeneza Tanzania yenye weredi. Katika thread hii naomba tuchangie hili la ajira za hapa nchini. Mara nyingi kumekuwepo na maelezo kuwa watanzania wengi hawana uwezo wa kujieleza pindi wanapoitwa kwenye Interviews, aidha utakuta wengi wao hawajui wanakwenda pale kufanya nini, hawana feedback ya kampuni au shirika wanalokwenda kuomba kazi na wengine hawajui hata majukumu ya nafasi wanazoziomba.
Tatizo kubwa hapa limekuwa likitokana na watu waliotangulia kuwa katika nafasi zao zenye maamzi kutumia nafasi hizo kulazimisha waajiri kuwapa upendeleo watu wao hata kama nafasi iliyopo ni tofauti na professional yake. Mara nyingi utasikia mtu akipiga simu .. Naomba umchukue tu ndugu yangu, atajifunza hivyohivyo tu polepole au anaingia pale ofisini kwa ki-memo, pindi anapoingia ofisini utacheka kwani hajui hata pa kuanzia. Huku kubebana hata pale ambapo hapatakiwi kufanyiwa dhihaka ndiko kumepelekea watanzania tuonekane vilaza mbele ya mataifa mengine, hali hii ndiyo iliyopo katika Taasisi ya vitambulisho vya Taifa NIDA kuwa kama ilivyo kwa sasa. Ni vichekesho tupu, wana jamvi jaribuni kufuatilia hawa waliochukuliwa kama DATA ENTREY, utachoka mwenye kwani pale wamewekwa hata waliomaliza mambo ya hotel management, Surveys, nk, mbaya zaidi nasikia umalaya umetangulizwa mbele kuliko. Haya kazi kwenu.