Inaonekanan huo msiba ulimgusa sana, kwa kawaida sisi binaadamu tunapoondokewa na mtu wa karibu na tuliyeshibana naye tunakuwa kama tumepoteza sehemu ya miili yetu.
Kuna mengi yanayoweza kuwaliza watu katika misiba, kama vile ukaribu, utegemezi, (yaani ulikuwa unamtegemea sana marehemu au alikuahidi kukusaidia jambo fulani ambalo lingekuletea manufaa,) na mambo mengine kama hayo, mara nyingi watu wa aina hiyo wanahitaji ushauri nasaha maana wanakumbwa na kukata tamaa, kiasi kwamba wanaweza hata kuyumba katika shughuli zao.......