Vile mashauzi yalivyoniumbua

Vile mashauzi yalivyoniumbua

Ila hizi mambo zetu wadada za kuignore na kuringa tukiitwa barabarani na watu tusiowafahamu sometime sio kabisa

Imewahi nitokea nakumbuka enzi za chuo hiyo siku weekend tumetoka hostel na shosti yangu lengo tukatafute msusi ila tukaenda mtaa ambao hatuufahamu vizuri.

Sasa tuko busy tunabahatisha njia tukapita sehemu wakaka wamekaa kama wa4 hivi na ilikua kama garage hizi za mtaani tu ambazo sio rasmi wakawa wanatuita aah tukakaza huku tunaambiana hao vipi kutuita ita hamna kuitika! Lahaulaaa kumbe tulipokua tunaelekea mbele hakuna njia inatoka hiyo njia ilikua inaenda ishia nyumbani kwa mtu! Kufika mbele hatuoni njia yaan kwanza tulijikuta tunacheka na aibuu maana tutapita vipi pale na tumegoma kupokea salamu zao.

Ikabidi turudi na kukutana nao tena tukawasalimia kwa aibu yaan walitupa maneno kibao tukajikaza na kuwauliza njia wakatuelekeza tukaendelea na safari yetu.
Kiukweli tangia siku hiyo kiburi barabarani niliweka pembeni salamu za watu naitikia vema na kwa adabu.
Akili zenu zinawazaga mtongozo tu.
 
Kuna mshkaji wangu anaishi Kawe. Nishawahi kuishi kwao kwa zaidi ya mieizi miwili kwahiyo nazijua njia za maeneo hayo vizuri tu. Kisha nikaondoka Dar kwa zaidi ya mwaka nilivyorudi tena Dar nikawa naishi kwetu sasa nikapanga kwenda kumtembelea mshkaji.

Siku imefika nikafunga safari nikaelekea Kawe. Kipindi hicho wimbo maarufu ni Prakatatumba wa Cabo Snoop na nilivaa kama mshkaji. Supra, jinzi chupa (enzi hizo haziitwi model), halafu jinzi inaingizwa ndani ya supra na fulana nikachomekea.

Nikafika sehemu ambayo ina kibaraza natakiwa niambae kufuata kibaraza kisha nikutane na kichochoro halafu hiko kichochoro kimekunja kulia halafu hapo ndo kinitoe kwenye njia pana ndiyo nikute uwanja anapokaa mshkaji.

Kwenye kibaraza nikakuta mabinti na wanawake wanasukana, nikawapita mwendo mdundo. Nikaingia kichochoroni nikakunja kulia nakuta kumezibwa kwa michongoma. Nikafikiria mwendo niliowapita pale nikaona kurudi siyo kweli na nilivyovaa itakua aibu.

Nikaparamia ile michongoma.

Kumbe katikati waliweka na miti ili michongoma isimame.

Nikakomaa. No backing down hapa.

Paramia na teke kwa mara ya pili pakalegea. Nikajipenyeza penyeza nikafanikiwa kupita.

Bwana wee nilijichana chana na ile miiba maeneo ya usoni na mgongoni. Fulana imechafuka kwa vumbi.

Did I learn anything? No. Am the same nigga who is shy kusalimia kundi la wamama.
Huyu mwamba n mpambanaji hakujali kizuiz na changamoto aliyokutana nayo n kusonga mbele tu ilaa watu...
 
Pole mkuu, Kuna harusi nilihudhuria miezi 2 iliyopita, sasa MC kaita mdada aliyependeza akafungue champagne,, mara paap kanyanyuka mdada na mashauzi kama yote, alikuwa kashaanza kulewa, sasa kumbe alilowana km Ni hivi obviously alienda toilet akajiswafi na vuzi lake maji yakalowesha au alianza breed, Sina hakika maana rangi ya nguo ilikuwa maroon,, watu wakamuita ili kumzuia, dada akahisi wanamshangilia yaani ndo biize kubinua mgongo anacheza kwa madoido,,, aibu niliyopata siku ile Kama ndo mie Yani

By the way, tangu nilipopataga breed katikati ya hadhara na mie sinaga kuumwa tumbo, Sina hili Wala lile,, nachoshukuru tu nyuma yangu alikuwepo mkaka naefahamiana nae aliniita taratibu akasema umechafua nguo yako, akavua sweta, nikajifunga, nilipata fundisho kubwa mno nilipunguza kabisa mashauzi kwa wakaka, hivyo hutokea unapita sehemu hadhara inakupa umakini wao,, Cha Kwanza huwa najiwazia nguo,, ni zipu Kama ya mtoa mada, nikijikagua akilini nikaona niko poa najua wadau wanashangaa uumbaji wa Mungu tu

Wanaume mna roho nzuri Sana katika hizi ishu mbarikiwe mno huwa mnatusitiri Sana kuliko wanawake wenzetu, anakuona unaaibika ila ndo kwanza anamuonyesha na mwenzie
Nimependa hapo mwishoni.. Wakaka kwenye mambo yetu wanatustiri sana..

Mimi mwenyewe Mwezi ulioisha nipo kwenye heka heka zangu.. nilikuwa nimevaa gauni..Kumbe kwa chini zipo imeachia ila juu haina shida.. Gauni zile za kuvaa na mkanda..

Mara ghafla sina hili wala lile nimeingia Duka moja ni Mkaka anauza.. Uzuri tulisalimiana vizuri tu.. ile naingia kugeuka akaniambia Dada hiyo gauni yako imeachia.. Kushika ilipoachia sasa.. Nilichoka.. ila Mkanda niliokuwa nimevaa ndiyo ulibana pasionekane kwa haraka..Kilichofuata ilikuwa kuangalia namna ya kuitengeneza.. Ila ile hali ilinikosesha raha nikijiuliza muda iliyoachia na watu ni wengi kiasi gani wameniona..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asee binafsi nikiitwa njiani ntasimama niskilize sababu ya kuitwa..

Kuna siku nlikua natembea njiani sina habari.. kuna kaka alikua anakuja mbele yangu, akanisimamisha akanisalimia kama ananijua nkamwitikia vizuri tu (nna haiba ya ku smile everytime ).. akaniambia dada chupi yako nzuri nkashtuka kaonaje chupi yangu huyu? Kuja kujiangalia zipu ya suruali ipo wazi nkacheka nkamshukuru nkaifunga nkaendelea na safari.
Sa nkawaza ningeringa ningechunguliwa na wangap sku iyo
Itakuwa nzuri hongera sana
 
Kuna mshkaji wangu anaishi Kawe. Nishawahi kuishi kwao kwa zaidi ya mieizi miwili kwahiyo nazijua njia za maeneo hayo vizuri tu. Kisha nikaondoka Dar kwa zaidi ya mwaka nilivyorudi tena Dar nikawa naishi kwetu sasa nikapanga kwenda kumtembelea mshkaji.
Hii kusalimia wamama hata mimi sipendi, unaweza jikuta umekisalimia kitoto kidogo chenye umbo kubwa.
 
Back
Top Bottom