Vikao vya Bunge vipunguzwe!

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,796
12,239
Hali ya fedha katika serikali yetu ni mbaya sana kiasi kwamba motisha ya kufanya kazi kwa watumishi wake imeshuka sana kutokana na kukosa vitendea kazi nyeti na muhimu.
  1. Ukitembelea ofisi nyingi za serikali watumishi wengi wanapiga soga na kusubiri muda wa kuondoka.
  2. Mahakamani kesi nyingi ama hazijaanza kusikilizwa au zimeahirishwa kutokana na ukata(Rejea maelezo ya jaji mkuu kwa JK siku ya mahakama)
  3. Wanafunzi wengi wa vyuo vikuu wamekosa mikopo kwa kuwa serikali haijapeleka fedha.
  4. Wakandarasi wengi wamepunguza kasi ya kujenga miradi mbalimbali kwa sababu ya kutolipwa madai yao kwa wakati.
  5. Madaktari interns waligoma kwa kucheleweshewa posho zao za miezi miwili.
  6. Halmashauri nyingi za wilaya hazijapelekewa fedha za maendeleo kwa takribani miaka miwili.
  • Orodha ni ndefu sana!
Pamoja na ukata huu, Bunge limekuwa likifanya vikao vyake kama kawaida! Viongozi wakuu wamekuwa wakifanya ziara kama kawaida! Kwa maneno mengine fedha kidogo ambayo imekuwa ikikusanywa inaishia kwa Bunge na ziara za viongozi.

Hii si sawa kabisa!
  • Bunge lina vikao vinne (4) kwa mwaka ambavyo huchukua miezi takribani minne(4) ( Kikao cha bajeti miezi 2 na ushee, Kikao cha Novemba wiki 2, Kikao cha Februari wiki 2 na Kikao cha Aprili wiki 2). Vikao vyote hivi hufanyika Dodoma.
  • Vikao vya kamati za bunge ambavyo havina muda maalumu ambavyo hufanyika kabla na baada ya vikao vilivyoorodheshwa hapo juu. Vikao hivi hufanyika Dar es Salaam.
Kutokana na hoja hizo nadhani wakati umefika nalo bunge likapunguza vikao vyake ili kubana matumizi. Aidha kwa kupunguza vikao wabunge wataelewa kwa uhalisia hali ya kifedha ilivyo na hivyo kutoa miongozo inayoeleweka kwa serikali ili kuongeza mapato ya nchi.

Wana JF naomba tujadili!
 
Natambua dhamira njema aliyonayo mleta thread, lakini hoja ya msingi si vikao. Hoja ni bunge kupunguzwa kwa kuondoa; (1) Viti Maalum, (2) Nafasi 5 za BLW. Aidha mtoa thread hajaelewa nini anakusudia kwa tafsiri ya Bunge.

Kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge toleo la 2007, kikao cha bunge ni kila siku ambayo bunge litakutana hivyo mtoa thread alikusudia kusema "BUNGE LIPUNGUZE MIKUTANO YAKE" Ikumbukwe kuwa katika uhai wa miaka 5 Bunge letu lina mikutano 20 ikwa ni mikutano 4 tu kwa mwaka hivyo ili litekeleze kikamilifu majukumu ya kikatiba ya kuisimamia serikali, nidhahili mikutano hiyo si mingi kwani serikali dhaifu kama yetu isipofuatiliwa mara kwa mara ipo siku bunge litakuta nchi imeshauzwa.
Nawsilisha
 
Ndiyo nchi yetu inavyokwenda hivyo hivyo.

Na wanaosafiri kila siku mbona haujawaandika.
 
Hali ya fedha katika serikali yetu ni mbaya sana kiasi kwamba motisha ya kufanya kazi kwa watumishi wake imeshuka sana kutokana na kukosa vitendea kazi nyeti na muhimu.
  1. Ukitembelea ofisi nyingi za serikali watumishi wengi wanapiga soga na kusubiri muda wa kuondoka.
  2. Mahakamani kesi nyingi ama hazijaanza kusikilizwa au zimeahirishwa kutokana na ukata(Rejea maelezo ya jaji mkuu kwa JK siku ya mahakama)
  3. Wanafunzi wengi wa vyuo vikuu wamekosa mikopo kwa kuwa serikali haijapeleka fedha.
  4. Wakandarasi wengi wamepunguza kasi ya kujenga miradi mbalimbali kwa sababu ya kutolipwa madai yao kwa wakati.
  5. Madaktari interns waligoma kwa kucheleweshewa posho zao za miezi miwili.
  6. Halmashauri nyingi za wilaya hazijapelekewa fedha za maendeleo kwa takribani miaka miwili.
  • Orodha ni ndefu sana!
Pamoja na ukata huu, Bunge limekuwa likifanya vikao vyake kama kawaida! Viongozi wakuu wamekuwa wakifanya ziara kama kawaida! Kwa maneno mengine fedha kidogo ambayo imekuwa ikikusanywa inaishia kwa Bunge na ziara za viongozi.

Hii si sawa kabisa!
  • Bunge lina vikao vinne (4) kwa mwaka ambavyo huchukua miezi takribani minne(4) ( Kikao cha bajeti miezi 2 na ushee, Kikao cha Novemba wiki 2, Kikao cha Februari wiki 2 na Kikao cha Aprili wiki 2). Vikao vyote hivi hufanyika Dodoma.
  • Vikao vya kamati za bunge ambavyo havina muda maalumu ambavyo hufanyika kabla na baada ya vikao vilivyoorodheshwa hapo juu. Vikao hivi hufanyika Dar es Salaam.
Kutokana na hoja hizo nadhani wakati umefika nalo bunge likapunguza vikao vyake ili kubana matumizi. Aidha kwa kupunguza vikao wabunge wataelewa kwa uhalisia hali ya kifedha ilivyo na hivyo kutoa miongozo inayoeleweka kwa serikali ili kuongeza mapato ya nchi.

Wana JF naomba tujadili!

UMAKINIKAJI,KWA MFANO UKIFUATILIA VIKAO VYA BUNGE NCHINI KENYA UTAONA WALIVYOSEREOUS KWANI WANABREAK SAA 2 tu siyo saa 4 kama hapa TZ WANAO SINGIZIA VIKAO VYA KAMATI.Hata hivyo umeonyesha Uchokozi Mzuri kuhusu Mapesa yetu.
 
Vikao vya bunge ni muhimu sana, bali watendaji wengi katika muhimili huo yaani Wabunge, awaelewi nini
kinapaswa kufanyika Bungeni. Na wanahitajika kuelimishwa mara kwa mara kuhusu muendelezo wa Bunge,
nasemea haswa kwa Wabunge wa chama tawala. Na vikao vya Bunge vinahitajika kuongezeka, pamoja
na vikao vya dharura kwa jambo lolote kubwa linalotokea kujadiliwa mara moja, na kutolewa maamuzi.
Swala la Wabunge wa viti maalum hivyo viondolewe mara moja, sababu vinaleta gharama ambazo si za lazima.
Katika kuongeza idadi ya Wabunge Wanawake, ni watu kujumuisha idea zao, na kuangalia mfumo gani
utafaa. Kwani kila uchaguzi majimbo yanakuwa yanaongezeka, kwa uwezekano wa kupata hata robo tatu ya
Wabunge Wanawake, itabidi watengewe majimbo maalum ambapo ugombeaji utakuwa ni kwa Wanawake tu.
Au itabidi kuangalia uwezekano wa kugawana majimbo, kutokana na idadi iliyokuwepo katika mkoa, kutokea hapo
Wanawake watakuwa na haki ya kuwakilisha Bunge, kutokana na ridhaa ya Wananchi. kwa mfumo huo idadi ya
Wabunge itakuwa imepungua kwa kiasi fulani, na hata gharama zitakuwa zimepungua.
 
Natambua dhamira njema aliyonayo mleta thread, lakini hoja ya msingi si vikao. Hoja ni bunge kupunguzwa kwa kuondoa; (1) Viti Maalum, (2) Nafasi 5 za BLW. Aidha mtoa thread hajaelewa nini anakusudia kwa tafsiri ya Bunge.

Kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge toleo la 2007, kikao cha bunge ni kila siku ambayo bunge litakutana hivyo mtoa thread alikusudia kusema "BUNGE LIPUNGUZE MIKUTANO YAKE" Ikumbukwe kuwa katika uhai wa miaka 5 Bunge letu lina mikutano 20 ikwa ni mikutano 4 tu kwa mwaka hivyo ili litekeleze kikamilifu majukumu ya kikatiba ya kuisimamia serikali, nidhahili mikutano hiyo si mingi kwani serikali dhaifu kama yetu isipofuatiliwa mara kwa mara ipo siku bunge litakuta nchi imeshauzwa.
Nawsilisha

Kwa mtazamo wako unaonyesha kuwa muda wa mikutano ya bunge mfupi! Lakini ukweli ni mrefu sana na usio na tija, chukulia bunge la bajeti:
  • Bajeti nzima ya serikali hujadiliwa katika hotuba za waziri wa fedha na Waziri Mkuu na wabunge hupata muda wa kutosha kuchangia hotuba hizo. Katika hotuba ya waziri wa fedha mgao wa fedha kwa kila wizara huainishwa, hivyo hakuna haja ya mjadala mrefu katika wizara husika ambazo wabunge wetu huzitumia kushukuru na kupongeza familia zao. Kimsingi hotuba za wabunge huwa hazibadili cho chote katika bajeti za wizara.
  • Mikutano mingine mitatuinaweza kuunganishwa kwa kuwa wabunge huishia kuwa na mikutano ya kivyama badala ya kujadili maswala ya kitaifa.
  • Kamati za bunge nazo hakuna kipya kinachoibuliwa kwa kuwa Mkaguzi mkuu huwa tayari amefanya kazi yake hivyo kinachotakiwa ni kutekeleza maoni ya mkaguzi mkuu.
Hivyo ni wazi kuwa muda wa vikao vya wabunge unaweza kupunguzwa na hivyo kuwapa muda zaidi wabunge kusimamia miradi ya maendeleo katika majimbo yao.
 
Ndiyo nchi yetu inavyokwenda hivyo hivyo.

Na wanaosafiri kila siku mbona haujawaandika.
Watumishi wanaosafiri mara kwa mara wanatumia udhaifu wa usimamizi katika serikali! Endapo serikali itawajibika ipasavyo na pia ikakubali kuwajibishwa, mambo haya yatakwisha!
 
Idadi ya wabunge pia ipunguzwe! viti maalum vifutwe ni mzigo!

mungu atusaidie tupate kiongozi anayeelewa..hatuna sababu na wabunge wa viti maalum..japo mheshimiwa msekwa anajaribu kuelezea hadi ughaibuni essense yake lakini ni ****** mtupu..na hata idadi ya majimbo ni uchafu mtupu..
matatizo ya wananchi yanaeleweka yote hata tukiongeza majimbo ya uchaguzi na idadi ya wabunge hawataongeza chochote kwani tatizo letu ni mitaji ya kufanyia maendeleo..IKIWA NI PAMOJA NA UONGOZI BOOOORA.
 
mungu atusaidie tupate kiongozi anayeelewa..hatuna sababu na wabunge wa viti maalum..japo mheshimiwa msekwa anajaribu kuelezea hadi ughaibuni essense yake lakini ni ****** mtupu..na hata idadi ya majimbo ni uchafu mtupu..
matatizo ya wananchi yanaeleweka yote hata tukiongeza majimbo ya uchaguzi na idadi ya wabunge hawataongeza chochote kwani tatizo letu ni mitaji ya kufanyia maendeleo..IKIWA NI PAMOJA NA UONGOZI BOOOORA.
Ni jambo la kusikitisha kuona serikali yetu inaendelea kuongeza/kubuni mikoa, wilaya, majimbo na kata bila kueleza ongezeko la mapato ya serikali katika kuendesha maeneo mapya. Kitendo cha kuongeza maeneo ya utawala maana yake ni kuongeza gharama za uendeshaji wa serikali.

Aibu kwa serikali ni kuwa maeneo yote ya utawala yaliyoongezwa yameshidwa kuanza kazi kwa sababu ya ukata!
 
Back
Top Bottom