Juliana Shonza
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 2,009
- 1,607
Tangu nimejiunga ndani ya CCM, nimepata fursa ya kufanya tafiti na kugundua tofauti kubwa sana kati ya viongozi, wanachama na hasa vijana ndani ya CCM na wale wanaotoka vyama vya upinzani, vikiongozwa na CHADEMA.
Lakini hali hii inatokana na mfumo wa Chama Cha Mapinduzi ambao umejikita katika malezi na mafunzo kwa vijana wake kupitia jumuiya yake ya vijana (UVCCM) ambayo imejibainisha kuwa ni tanuru la kuoka viongozi wa chama na Serikali.
Kitu cha kipaumbele ktk uongozi na shabaha ya UVCCM ni kuongeza maarifa kwa vijana wa chama. Vijana wengi wameendelezwa kielimu (kwa fedha ya jumuiya) katika vyuo vikuu mbalimbali, jambo ambalo vyama vya upinzani hawafanyi, hawana mfumo wa ku-groom vijana wao na badala yake vijana wamekuwa wakijiongoza wenyewe na hivyo kupoteana.
lakini pia, Vijana wa UVCCM wana matumaini zaidi kuliko Vijana wa Chadema na wapinzani wengine, leo vijana wa Chadema na Wapinzani wanatamani wangekuwa CCM ili wanufaike na fursa za kupata maarifa na kujengewa uwezo, ndio maana akina Yericko Nyerere, Ben Saanane na wengineo wanafanya kazi za wagombea wa CCM kwa kuwa wamepoteza matumaini na viongozi wao kwenye vyama vyao.
Uwezo mdogo wa vijana wa chadema unajidhihirisha kwenye CV zao, kwani wengi ni mangumbaro wasio na elimu ya kutosha, lakini pia maneno wanayoandika kila kukicha katika jukwaa hili yanadhihirisha uwezo wao mdogo, thread za akina Henry Kileo, Tumaini Makene etc zinawavua nguo vijana wa Chadema.
USHAURI.
VIJANA wa vyama vya upinzani jiongezeni, mnalalamika hamna ajira wakati elimu ya kuunga unga, mnafikiri mtapata kazi kwa kuandamana..? Ongezeni maarifa ili muweze kuajirika, sio mnakesha kwenye ma-movement yasiyo na tija halafu mnategemea maisha bora.
Lakini hali hii inatokana na mfumo wa Chama Cha Mapinduzi ambao umejikita katika malezi na mafunzo kwa vijana wake kupitia jumuiya yake ya vijana (UVCCM) ambayo imejibainisha kuwa ni tanuru la kuoka viongozi wa chama na Serikali.
Kitu cha kipaumbele ktk uongozi na shabaha ya UVCCM ni kuongeza maarifa kwa vijana wa chama. Vijana wengi wameendelezwa kielimu (kwa fedha ya jumuiya) katika vyuo vikuu mbalimbali, jambo ambalo vyama vya upinzani hawafanyi, hawana mfumo wa ku-groom vijana wao na badala yake vijana wamekuwa wakijiongoza wenyewe na hivyo kupoteana.
lakini pia, Vijana wa UVCCM wana matumaini zaidi kuliko Vijana wa Chadema na wapinzani wengine, leo vijana wa Chadema na Wapinzani wanatamani wangekuwa CCM ili wanufaike na fursa za kupata maarifa na kujengewa uwezo, ndio maana akina Yericko Nyerere, Ben Saanane na wengineo wanafanya kazi za wagombea wa CCM kwa kuwa wamepoteza matumaini na viongozi wao kwenye vyama vyao.
Uwezo mdogo wa vijana wa chadema unajidhihirisha kwenye CV zao, kwani wengi ni mangumbaro wasio na elimu ya kutosha, lakini pia maneno wanayoandika kila kukicha katika jukwaa hili yanadhihirisha uwezo wao mdogo, thread za akina Henry Kileo, Tumaini Makene etc zinawavua nguo vijana wa Chadema.
USHAURI.
VIJANA wa vyama vya upinzani jiongezeni, mnalalamika hamna ajira wakati elimu ya kuunga unga, mnafikiri mtapata kazi kwa kuandamana..? Ongezeni maarifa ili muweze kuajirika, sio mnakesha kwenye ma-movement yasiyo na tija halafu mnategemea maisha bora.