Vijana tuna hali ngumu sana katika utawala huu wa awamu ya 5

Sigara Kali

JF-Expert Member
May 28, 2017
3,623
8,428
Nimetafakari sana na kushindwa kumwelewa huyu rais wa awamu ya 5 ndugu Pombe Magufuli

Utawala huu unaonekana wazi hauna nia ya kuboresha Maisha ya vijana wa Nchi hii ambao ndio robo tatu ya watu wote ,ndio wapiga kura na ndio wachapa kazi wa Nchi hii

Vijana wa Tanzania tunakejeriwa,hatuthaminiwi,tunaitwa wavivu wapiga dili.

Vijana wametoka chuo wameshindwa kuajiriwa,sawa nafasi za ajira chache tuwezeshwe basi hata mitaji tukalime mchicha huko na nyanya,raisi hana muda anajali kujenga reli na kununua vipanga boi na terrible teen(Boeing dreamliner)

Vijana wa Nchi hii wamekosa dira,wamekosa malezi mema ya viongozi wao,hawajajengewa mazingira rafiki ya kujiajiri,wanaishia kusimangwa,kubaguliwa,kukejeliwa na kuonwa wavivu wakati nchi haijawaandalia msingi

Serikali ya awamu ya 5 ndo inaonekana kabisa haina time na vijana wa nchi hii, Leo hii vijana watanzania wamekua wakiishi Maisha ya kubahatisha,kijana ili ale inabidi akabeti, akacheze kamari kwenye mashine za wachina na hii inafanikiwa baada ya kupambana kupata mia 5 akafanye shughuli hiyo

Wanasiasa,viongozi wamewasahau vijana wa Nchi, wanawadharau, hawawathamini wanaowaona kama ni wajinga, wazembe, wavivu, tegemezi hawana manufaa kwa nchi yao

Leo vijana wengi wamekata tamaa kwenye nchi yao has a baada ya kuingia huu utawala wa awamu ya 5 chini ya Magufuli

Vijana hawajajengewa mazingira yoyote bora ya kuboresha Maisha yao leo lawama zote kwao, Serikali inaona bora kuwekeza kwenye mambo yasiyomnufaisha mtanzania wa kawaida hasa kijana nguvu ya nchi hii wanadeal na vitu vinavyowanufaisha wachache akiwemo raisi na ukoo wake na wale wote wenye nazo

Vijana wa Tanzania wanaishi kwa kudra za Mungu waliowaamini kuwatengenezea mazingira mazuri kwao wamewasaliti, hawawajali, wanawadharau, kuwakejeli na kuona vijana hawa wanastahili tabu , mateso na shida katika nchi yao.

Mungu ibariki Tanzania
Mungu wabariki vijana wote wa taifa ili la Tanzania
 
Vijana acheni kulia lia fanyeni kazi; kijana pambana kuliko kuja kulia mitandaoni haikusaidii kitu.

Ndugu yangu kwa vile wewe unapakujishikiza. Kiuhalisia watu wana maisha magumu sana Mimi mwenyewe jamaa yangu kitaani alichoniambia Leo nimeumia sana. Tangu Ramadhani ianze hajawahi kufuturu, yaani yeye anahangaika na hela ya daku tu na ana familia. Amejiajiri ni mfanyabiashara kila day biashara yake inazidi kushuka.

Ngoja niswali kwanza.
 
Kama vijana tupo serious kuna mambo kadhaa tunaweza kufanya
1. Kufanya mobilization.Tuanzishe forum tukutane tuunde kundi tujisajili tukachukue mikopo halmashauri.Maneno bila vitendo ni sawa na bure.
2.Tutafute maeneo yenye rutuba tufanye KILIMO chenye tija kwenye kilimo serikali imeondoa tozo SUMBUFU na watu wanapiga mpunga kupitia KILIMO tuwe serious.kama kuna mtu aliye serious na hii ishu ajitokeze.Kukaa kulaumu mtandaoni sio solution.
3.Tunaweza hata humuhumu kuanzisha forums kwa ajili ya kupeana mikakati ya kupiga biashara.Kukaa kulaumu serikali tutalaumu hadi kuzeeka.
Kama upo serious muda ni huu kama unataka kuendelea kuwa mlalamikaji JF basi utabaki kila siku kulaumu serikali,
 
Nenda ukalime kijana ujipange kumwadhibu 2020! Tuvijana twenzenu TWA uvccm tunasema maisha yako vizuri mno!
 
Kama vijana tupo serious kuna mambo kadhaa tunaweza kufanya
1. Kufanya mobilization.Tuanzishe forum tukutane tuunde kundi tujisajili tukachukue mikopo halmashauri.Maneno bila vitendo ni sawa na bure.
2.Tutafute maeneo yenye rutuba tufanye KILIMO chenye tija kwenye kilimo serikali imeondoa tozo SUMBUFU na watu wanapiga mpunga kupitia KILIMO tuwe serious.kama kuna mtu aliye serious na hii ishu ajitokeze.Kukaa kulaumu mtandaoni sio solution.
3.Tunaweza hata humuhumu kuanzisha forums kwa ajili ya kupeana mikakati ya kupiga biashara.Kukaa kulaumu serikali tutalaumu hadi kuzeeka.
Kama upo serious muda ni huu kama unataka kuendelea kuwa mlalamikaji JF basi utabaki kila siku kulaumu serikali,
Wewe inaonekana, " You feel a bit ahead of the game and start to think it's because of your "Ingenuity" you've managed to make a headway".

But surely, you can be one of those fellows currently enjoying the handouts this regime offers to it's loyalists.

You can't establish a forum that targets to empower the youths to be self employed in say, agriculture when the handicap that hinders them to do so is basically lack of capital, a challenge that the government is supposed to tackle but is not.

The government should provide facilities for the youths to enable them initiate productive activities that can sustain them and at the same time enable the government to enhance its revenue capacity. It's a noble obligation that they cannot avoid.
 
Kama vijana tupo serious kuna mambo kadhaa tunaweza kufanya
1. Kufanya mobilization.Tuanzishe forum tukutane tuunde kundi tujisajili tukachukue mikopo halmashauri.Maneno bila vitendo ni sawa na bure.
2.Tutafute maeneo yenye rutuba tufanye KILIMO chenye tija kwenye kilimo serikali imeondoa tozo SUMBUFU na watu wanapiga mpunga kupitia KILIMO tuwe serious.kama kuna mtu aliye serious na hii ishu ajitokeze.Kukaa kulaumu mtandaoni sio solution.
3.Tunaweza hata humuhumu kuanzisha forums kwa ajili ya kupeana mikakati ya kupiga biashara.Kukaa kulaumu serikali tutalaumu hadi kuzeeka.
Kama upo serious muda ni huu kama unataka kuendelea kuwa mlalamikaji JF basi utabaki kila siku kulaumu serikali,
Kilimo alafu ukivuna serkali ukupangie bei na wapi uuze .haya maviongozi sijui yana akili gani
 
Back
Top Bottom