Vijana mnakwama wapi?

Vijana wengi wanapishana na magari ya mishahara wenyewe halafu wanawalaumu watu wengine
Ndiyo hapo sasa! Mtu ambaye haoni umuhimu wa kununua hata vocha ya buku ili aombe kazi kesho ndiyo umtegemee aje kazini tena kwa wakati?
 
Mkuu nifanyie mpango nipate kazi.
 
Kwa lugha hizi hata kama ulidhamiria kumdhamini lazima uingiwe ubaridi.tatizo linakuja hawajui kuandika kulingana na mazingira text seriously wanaandika kama wapo kwenye magrup ya shule za msingi.
Mnatuonea aisee. Sio wote tupo hivyo mkuu
 
Mdogo wangu kwa sasa hatumi tena text kwangu maana hua nakereka sana na text zake za "xijambo, xijui
 
Wamekuxoma xabaxeven
 
Nyie wazee mnaotufanyia mambo hayo mkizeeka wakati sisi tupo kwenye system tunarudisha kikokotoo ili mpate 25% dadadeq.
Sasa hivi si mnaona mmetoboa sababu mliwahi kuzaliwa.. sasa mtazeeka tu na sisi tutaingia kwenye system na yote mnayotufanyia tutalipa..
 
Vijana wengi wanapishana na magari ya mishahara wenyewe halafu wanawalaumu watu wengine
Hayo mambo tulifundishwa kidato cha pili lakini hatuzingatii
 
Acha kuwalaumu vijana kiasi hicho, hata wewe kumbuka kuna watu wanakuona una zingua ila tu wanakustahi/wanakuwa waelewa kwani lawama hazisaidii.

Note: Jifunze kuelewa hali na tabia za watu wa rika tofauti tofauti ndani ya nyakati tofauti. Kunyooshea kidole mapungufu ya rika fulani/mtu fulani hakukufanyi uonekane wewe uko perfect.

Wewe hutowasaidia hao vijana ila tupo tutakao wasaidia kwasababu tunaelewa hali halisi ya hawa vijana wetu.

Acheni complications za ajabu ajabu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…