Vigogo Mashuhuri wajitoa CUF

Vigogo Mashuhuri wajitoa CUF

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Viongozi mashuhuri wa CUF wamejitoa katika chama hicho leo.Viongozi hao ni aliyekuwa meneja kampeni wa Urais wa Lipumba Bw Said Miraji na aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Temeke kupitia CUF Bw Kadawi Lucas Limbu.Viongozi hao kwa pamoja wamesema wanajitoa CUF rasmi leo kutokana na vurugu kubwa zinazoendelea ndani ya chama hicho na pia wasingependa kuona chama hicho kikizikwa wakiwa bado wanachama.SOURCE: CHANEL TEN
 
nini mustakabali wao kisiasa au wameamua kuachana na siasa kabisa!! CUF is a dying horse!!it kicks very hard!!
 
Wamehamia wapi jama wafanye fasta waje huku kwetu

kwetu pazuuuri nimeshapakumbuuka
 
Masahihisho kidogo, ni Kadawi Lucas Limbu, aliyegombea Temeke.
Lakini bado utamsikia mtatiro akijibodoa kwamba bora wameondoka wenyewe kwakuwa baraza kuu lilikuwa na mpango wa kuwafukuza.
Ukimsikiliza ismail justa atakwambia hao ni wakristo ndio sababu wameamua kujiengua!

Cuf kinakwenda kaburini, la sivyo maalim seif aachie ngazi kama anakipenda chama chake!
 
Mtatiro mapovu yanazidi kumtoka,hongereni kwa kujitoa CCM B ila mnafuata Hamad kwenye chama chake kipya.
 
Maalim seif anatakiwa kutoka mafichoni kuokoa chama. Naona ukimya wake na huu mwendelezo wa kujitoa kwa wanachama hautakiwi kuachwa bila ufumbuzi. Kufikia 2015 chama cha CUF kinaweza kisiwepo tena.
 
Hao wameamua kuchana na aibu na kashfa ya kugeuzwa nyumba ndogo ya CCM. Heri wamuachie Seif Sharriff aibu yake na mtu wake Ismail Juha.
 
Masahihisho kidogo, ni Kadawi Lucas Limbu, aliyegombea Temeke.
Lakini bado utamsikia mtatiro akijibodoa kwamba bora wameondoka wenyewe kwakuwa baraza kuu lilikuwa na mpango wa kuwafukuza.
Ukimsikiliza ismail justa atakwambia hao ni wakristo ndio sababu wameamua kujiengua!

Cuf kinakwenda kaburini, la sivyo maalim seif aachie ngazi kama anakipenda chama chake!

Nakushukuru mkuu nimeshafanya masahihisho
 
Back
Top Bottom