[h=3]VIGOGO BODI YA KAHAWA MOSHI WACHUNGUZWA KWA UFISADI[/h]
JENGO LA MAKAO MAKUU YA BODI YA KAHAWA KAMA LINAVYOONEKANA.
Na Charles Ndagulla,Moshi.
VIGOGO watatu wa bodi ya kahawa nchini(TCB) yenye makao yake makuu mjini moshi akiwamo Mkurugenzi mwendeshaji wa bodi hiyo,Injinia Adolph Kumburu,wanachunguzwa na serikali wakituhumiwa kutumia vibaya madaraka yao kwa kufuja mamilioni ya fedha .
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa,Tume hiyo inawajumuisha maofisa kutoka Ikulu,Bodi ya zabuni ya taifa,Wizara ya Kilimo,chakula na ushirika pamoja na Tume ya utumishi wa umma .
Tume hiyo inachunguza mambo 11 ikiwamo utoaji wa zabuni bila kuzingatia sheria ya manunuzi ya umma ambako mkurugenzi huyo na wasaidizi wake wanatuhumiwa kutoa zabuni kinyemela kwa baadhi ya makampuni bila kushindani makampuni mengine.
Tuhuma nyingine zinazomkabili mkurugenzi huyo na wasaidizi wake ni kutumia vibaya madaraka yao kwa kuidhinisha dola 105,000 kwa ajili ya safari ya 'kutalii ' nchini Vietnam na China julai 12 hadi 31 mwaka jana ambako wajumbe wanane wa bodi hiyo na maofisa wawili walisafiri.
Inadaiwa kuwa, fedha hizo ziliidhinishwa na Mkurugenzi huyo na wasaidiazi wake bila kibali kutoka chombo kilicho juu ya bodi hiyo ambacho ni wizara ya Kilimo,chakula na Ushirika.
Tume hiyo ambayo ipo kwa zaidi ya siku tano sasa hapa mjini Moshi,tayari imeshawahoji Mkurugenzi anayeshughulikia ubora wa kahawa ndani ya bodi hiyo ,Primus Kimario,meneja wa fedha na ambaye pia ni kaimu mkurugenzi wa fedha(DF),Asteri Bitegeko na Mkurugenzi wao Injilia Adolph Kumburu.
Vigogo hao watatu ambao ndiyo waidhinishaji wakuu wa fedha(watia saini),wanatuhumiwa kutoa kandarasi ya kutathimini mali za bodi hiyo kwa kampuni moja ya mkoani Tabora yenye thamani ya sh,Milioni 60 bila kushindanisha makampuni mengine.
Pia wanatuhumiwa kuipa kandarasi kampuni moja ya Star Fish ya Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kutoa taarifa za bei ya kahawa kwa wakulima kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kupitia simu za kiganjani(SMS) kandarasi ya dola za kimarekani 15,000 kwa mwaka zaidi ya sh,Milioni 24 za Tanzania bila kushindanisha kampuni nyingine.
Hata hivyo pamoja na kukiri kuwepo na uchunguzi huo,Mkurugenzi wa bodi hiyo,Injinia Kumburu,amedai hiyo si tume bali ni kamati aliyodai ipo hapa mjini moshi kwa ajli ya ukaguzi wa kawaida japo hakuwa tayari kungia kwa undani ni mambo yapi kamati hiyo inachunguza.
Katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jumanne wiki hii,Kumburu hakuwa tayari kujibu tuhuma dhidi yake ambazo ni miongoni mwa mambo yanayochunguzwa na tume hiyo kwa kile alichodai kufanya hivyo ni kuingilia kazi ya tume.
Tuhuma nyingine zinazochunguzwa na tume hiyo ni kuwepo na watumishi wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi mishahara ambayo ni nje ya ile iliyoidhinishwa na hazina huku bodi hiyo ikituhumiwa kuwa na vikao vingi vyenye lengo la kulipana posho vikao ambavyo vinadaiwa havina tija kwa bodi.
Inadaiwa kuwa,tangu januari mwaka huu hadi sasa bodi hiyo imeendesha vikao sita na kila kikao inadaiwa hutumia kiasi cha sh,Milioni 20 ambapo mwenyekiti wa bodi hulipwa sh,350,000 kwa kikao kimoja,mkurugenzi ambaye ni katibu wa bodi na wejumbe wengine hulipwa sh,300,000 kila mmoja.
Mkurugenzi huyo pia hakukiri wala kukanusha tuhuma zinazoelekezwa kwake kuwa amekuwa akisafiri mara kwa mara hata safari ambazo hazina umhimu huku akidaiwa pia kuunda kanda nje ya kanunni za bodi hiyo za mwaka 2003.
Kwa mujibu wa habari za uchunguzi,mkurugenzi huyo ameanzisha kanda tatu za Tarime,Kigoma na Ruvuma nje ya kanuni za bodi huku akidaiwa kutenga Milioni 20 kila mwaka kwa kila kanda ingawa zipo taarifa kwamba fedha hizo huishia njiani.
MWISHO.
JENGO LA MAKAO MAKUU YA BODI YA KAHAWA KAMA LINAVYOONEKANA.
Na Charles Ndagulla,Moshi.
VIGOGO watatu wa bodi ya kahawa nchini(TCB) yenye makao yake makuu mjini moshi akiwamo Mkurugenzi mwendeshaji wa bodi hiyo,Injinia Adolph Kumburu,wanachunguzwa na serikali wakituhumiwa kutumia vibaya madaraka yao kwa kufuja mamilioni ya fedha .
Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi umebaini kuwa,Tume hiyo inawajumuisha maofisa kutoka Ikulu,Bodi ya zabuni ya taifa,Wizara ya Kilimo,chakula na ushirika pamoja na Tume ya utumishi wa umma .
Tume hiyo inachunguza mambo 11 ikiwamo utoaji wa zabuni bila kuzingatia sheria ya manunuzi ya umma ambako mkurugenzi huyo na wasaidizi wake wanatuhumiwa kutoa zabuni kinyemela kwa baadhi ya makampuni bila kushindani makampuni mengine.
Tuhuma nyingine zinazomkabili mkurugenzi huyo na wasaidizi wake ni kutumia vibaya madaraka yao kwa kuidhinisha dola 105,000 kwa ajili ya safari ya 'kutalii ' nchini Vietnam na China julai 12 hadi 31 mwaka jana ambako wajumbe wanane wa bodi hiyo na maofisa wawili walisafiri.
Inadaiwa kuwa, fedha hizo ziliidhinishwa na Mkurugenzi huyo na wasaidiazi wake bila kibali kutoka chombo kilicho juu ya bodi hiyo ambacho ni wizara ya Kilimo,chakula na Ushirika.
Tume hiyo ambayo ipo kwa zaidi ya siku tano sasa hapa mjini Moshi,tayari imeshawahoji Mkurugenzi anayeshughulikia ubora wa kahawa ndani ya bodi hiyo ,Primus Kimario,meneja wa fedha na ambaye pia ni kaimu mkurugenzi wa fedha(DF),Asteri Bitegeko na Mkurugenzi wao Injilia Adolph Kumburu.
Vigogo hao watatu ambao ndiyo waidhinishaji wakuu wa fedha(watia saini),wanatuhumiwa kutoa kandarasi ya kutathimini mali za bodi hiyo kwa kampuni moja ya mkoani Tabora yenye thamani ya sh,Milioni 60 bila kushindanisha makampuni mengine.
Pia wanatuhumiwa kuipa kandarasi kampuni moja ya Star Fish ya Jijini Dar es salaam kwa ajili ya kutoa taarifa za bei ya kahawa kwa wakulima kupitia ujumbe mfupi wa maandishi kupitia simu za kiganjani(SMS) kandarasi ya dola za kimarekani 15,000 kwa mwaka zaidi ya sh,Milioni 24 za Tanzania bila kushindanisha kampuni nyingine.
Hata hivyo pamoja na kukiri kuwepo na uchunguzi huo,Mkurugenzi wa bodi hiyo,Injinia Kumburu,amedai hiyo si tume bali ni kamati aliyodai ipo hapa mjini moshi kwa ajli ya ukaguzi wa kawaida japo hakuwa tayari kungia kwa undani ni mambo yapi kamati hiyo inachunguza.
Katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jumanne wiki hii,Kumburu hakuwa tayari kujibu tuhuma dhidi yake ambazo ni miongoni mwa mambo yanayochunguzwa na tume hiyo kwa kile alichodai kufanya hivyo ni kuingilia kazi ya tume.
Tuhuma nyingine zinazochunguzwa na tume hiyo ni kuwepo na watumishi wanaolipwa mishahara mikubwa zaidi mishahara ambayo ni nje ya ile iliyoidhinishwa na hazina huku bodi hiyo ikituhumiwa kuwa na vikao vingi vyenye lengo la kulipana posho vikao ambavyo vinadaiwa havina tija kwa bodi.
Inadaiwa kuwa,tangu januari mwaka huu hadi sasa bodi hiyo imeendesha vikao sita na kila kikao inadaiwa hutumia kiasi cha sh,Milioni 20 ambapo mwenyekiti wa bodi hulipwa sh,350,000 kwa kikao kimoja,mkurugenzi ambaye ni katibu wa bodi na wejumbe wengine hulipwa sh,300,000 kila mmoja.
Mkurugenzi huyo pia hakukiri wala kukanusha tuhuma zinazoelekezwa kwake kuwa amekuwa akisafiri mara kwa mara hata safari ambazo hazina umhimu huku akidaiwa pia kuunda kanda nje ya kanunni za bodi hiyo za mwaka 2003.
Kwa mujibu wa habari za uchunguzi,mkurugenzi huyo ameanzisha kanda tatu za Tarime,Kigoma na Ruvuma nje ya kanuni za bodi huku akidaiwa kutenga Milioni 20 kila mwaka kwa kila kanda ingawa zipo taarifa kwamba fedha hizo huishia njiani.
MWISHO.