Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 264
nimepata CD mbili kutoka source tofauti ambazo watu wamefanya compilation ya matukio ya Arusha kuanzia maandamano, mahakamani, na mazishi. inaonekana ni clips zilizochukuliwa kutumia vyombo mbali mbali lakini wote siyo wataalamu wa kufanya hiyo kazi. pia inaonekana ni matukio ambayo yamechukuliwa katika mazingira mbali mbali, yaani huku watu wakikimbia, wamesimama, labda wengine walikuwa majumbani au madukani au ofisini mwao, n.k
binafsi nimevulia kofia matumizi ya technolojia ya kisasa, yaan simu, digital camera, na vyombo vingine. Pia nimevulia kofia waliounganisha hivyo vipande kiasi kwamba hatuhitaji kuandika historia ya jambo fulani kwa kutegemea kilichoripotiwa na vyombo vya habari tu au vyombo vya dola.
kwa ujumla ni hali ya kutisha. lakini ni ishara kwamba serikali bado iko kwenye karne ya nyuma sana. karne ambayo ni serikali tu ndiyo iliyokuwa na mamlaka ya kuchukua kumbukumbu za tukio. kwamba tukio lisipochukuliwa na waandishi wa habari basi halikutokea. kwamba waandishi wa habari tu ndio wanaoweza kutoa habari. karne ambayo kwamba kauli ya serikali ilikuwa ya kweli daima!
binafsi nimevulia kofia matumizi ya technolojia ya kisasa, yaan simu, digital camera, na vyombo vingine. Pia nimevulia kofia waliounganisha hivyo vipande kiasi kwamba hatuhitaji kuandika historia ya jambo fulani kwa kutegemea kilichoripotiwa na vyombo vya habari tu au vyombo vya dola.
kwa ujumla ni hali ya kutisha. lakini ni ishara kwamba serikali bado iko kwenye karne ya nyuma sana. karne ambayo ni serikali tu ndiyo iliyokuwa na mamlaka ya kuchukua kumbukumbu za tukio. kwamba tukio lisipochukuliwa na waandishi wa habari basi halikutokea. kwamba waandishi wa habari tu ndio wanaoweza kutoa habari. karne ambayo kwamba kauli ya serikali ilikuwa ya kweli daima!