Video: Nape alipoangua kilio hadharani jimboni kwake Mtama

chinchilla coat

JF-Expert Member
May 16, 2016
5,107
10,961
Sijajua ilikuaje hadi mheshimiwa akawa over-come na emotions huko kwao, sijajua ni super V.I.P treatment na heroic welcome aliyopipata huko kwao ukilinganisha na alivyokuwa treated Dar na kupuuziwa na mkubwa wake wa kazi au au ni remorse na guilty ya aliyoyafanya zamani au ni vipi.

 
Tunahitaji majibu ya maswali haya kuhusu utekaji
1: Watekaji ni kina nani?
2: Wamekamatwa?
3: Waliwateka wasanii kwa ajili gani? (What were they demanding)
4: Waliteswa?
5: Kuna ushahidi wa majeraha? Au damu kutoka kwa aina yeyote ile.
6:Studio kuna CCTV camera? If yes zilishika sura za watekaji?
7: Wameachiwa huru au police wamewaokoa? Hao mashujaa/police ni akina nani? Tunaweza kuwajuwa tuwapongeze?
8: Wasanii wanaweza kutoka hadharani mubashara nakutuelezea kilichotokea ili tuwatizame machoni?
Nikipata majibu ya haya maswali nitakuja na mengine 10.
 
Sijajua ilikuaje hadi mheshimiwa akawa over-came na emotions huko kwao, sijajua ni V.I.P treatment na heroic welcome aliyopipata huko kwao ukilinganisha na alivyokuwa treated Dar na kupuuziwa na mkubwa wake wa kazi au au ni remorse na guilty ya aliyoyafanya zamani au ni vipi......


Nape amekata tamaa u radhi kwa lolote iwe heri ama shari , kitendo cha kumtolea bastola hadharani tena na mtu ambaye hajielewi kisa katumwa na asiye jielewa kina mpa mateso makali sana hasa akikumbuka kazi aliyo ifanya kwamoyo mkunjufu kuwa fitini wengine ili waliopo sasa wapate nafasi wanazo zitumia kumnyanyasa.
 
mpumbavu huyu, kwa ujinga wake kaondolewa cheoni analia

ahame chama aende chadema kisha agombee, huwezi kuwa mpinzani wa bosi wako ukaangaliwa, yeye nani??

walijiandaa kuuondoa magufuli amegunduliwa mapema sana

na leo kathibitisha kuwa Magufuli hakukosea kabisa kabisa!

kama alikuwa na majibu ya kamati kwa nini aliunda kamati? alikuwa anampumbaza nani? mpuuzi huyu

na ndio mwisho wake, mark my words

mozes nnauye hakuwa mjinga hivi
 
mpumbavu huyu, kwa ujinga wake kaondolewa cheoni analia

ahame chama aende chadema kisha agombee, huwezi kuwa mpinzani wa bosi wako ukaangaliwa, yeye nani??

walijiandaa kuuondoa magufuli amegunduliwa mapema sana

na leo kathibitisha kuwa Magufuli hakukosea kabisa kabisa!

kama alikuwa na majibu ya kamati kwa nini aliunda kamati? alikuwa anampumbaza nani? mpuuzi huyu

na ndio mwisho wake, mark my words

mozes nnauye hakuwa mjinga hivi

Wangapi walijua kuwa Mwakyembe baadae angekuja kuwa Senior Minister wa Jk wakati ule wa 2008 kwny Scandle ya Richmond ?

Weka Akiba ya Maneno

2007 Nape alikatwa kwny Mchujo wa Uenykt UV-CCM na alipojaribu kukata Rufaa Katibu Mkuu wa Chama Mzee Makamba akamwambia rufaa yako imefungwa Mbinguni na Ardhini lakin Miaka minne baadae akawa Bosi wa Mzee Makamba.

Siasa hazina' Mtabiri wa Hali ya hewa 'we tembea na Mwamvuli tu Muda wote inaweza kunyesha.
 
Huyu bwana akiendelea hivi ni wazi 2020 atakataliwa vibaya sana sio na wafuasi wa vyama vya upinzani tu,bali hata wana-CCM wenzake.

Huyu mh. asiposoma alama za nyakati na kujirekebisha,anaweza kuambulia asilimia 40 ya kura zote zitakazopigwa na hata asilimia 35 kabisa.

Ule umati mkubwa uliojitokeza ulikuwa unatuma salam kwake kuwa mbunge wao ni shujaa na zaidi hakutendewa haki.Hii ni dalili mbaya sana kwa mkulu.

Narudia,Bashite ana play role ya Mohamed Bouazizi ya kuleta mabadiliko ya kiutawala nchini kama ambavyo Bouazizi alivyokuwa chanzo cha mabadiliko nchini kwake Tunisia na baadae katika ulimwengu wa nchi kadhaa za kiarabu.

Bahati mbaya sikio la kufa halisikii dawa.

Time will tell.
 
Lakini amechangia pakubwa kuwepo kwa haya yote!si alisema chama chake lazima kishinde hata gwa goli like la tambwe kwa kichuya!kuna mchungaji yule a tauni kuwa lazima uvune unachopanda
 
Acha kuchochea, karudi jimboni kwake ulitegemea iweje!?

Tena hao mbona sio wanamtama wote. Ungeona wenzake wa CCM waliokaa meza kuu, walivyokuwa hawampigii makofi kwa mengi aliyoongea ndio ungejua kuwa anachemka na leo kajionyesha zaidi kuwa ni mtu hatari wa mabaya.

Mtanyooka tu
 
Back
Top Bottom