VIDEO - Jeshi la Misri Lamvua Nguo Mwanamke Mwandamanaji

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
6132970.jpg

Mwanamke mwandamanaji alivyoshushiwa kipigo
Tuesday, December 20, 2011 10:30 PM
Katika hali ya kusikitisha na kukatisha tamaa, Polisi wa kijeshi (MP) wa Misri wamemtandika hadi kumuacha uchi mwanaharakati msichana aliyekuwa katika mshikamano wa kupinga utawala wa kijeshi na serikali ya kuokoa taifa la Misri.
Kuna mgawanyiko mkubwa miongoni mwa raia wa Misri kuhusiana na tukio hili. Kwa upande mmoja wanaharakati wanaopinga utawala wa kijeshi wanaona jeshi limetumia nguvu kupita kiasi na wanalitaka liondoke madarakani mara moja na nchi ikibadhiwe kwa waandamanaji.

Na upande wa pili unaoungwa mkono na raia wengi wa Misri wanaona kuwa jeshi limetekeleza wajibu wake na wanaliunga mkono liendelee kushika madaraka hadi utakapomaliza uchaguzi wa haki usio na uchakachuaji unaoendelea hivi sasa, ambapo matokeo yanaonesha kuwa vyama vya mlengo wa Kiislam vikiongoza kwa asilimia zaidi ya 65 ya viti vyote vya bunge vilivyogombaniwa hadi sasa.

Nifahamishe inatumia nafasi hii kuwatuliza ndugu jamaa na marafiki wa watanzania waliopo Misri kuwa ndugu zao wapo salama salimini wakiendelea na mambo yao kama kawaida licha ya utete wa hali ya kisiasa na vurugu za mara kwa mara.

Nifahamishe imeongea na baadhi ya raia wa Tanzania waishio Misri ili kujua maoni yao juu ya hali ilivyo hapa Misri na kuhakikishiwa kuwa vurugu zipo katika maeneo maalum na sana sana katikati ya mji mkuu Cairo, wala hazina madhara makubwa kwao ukiondoa ile hali ya hofu na kujihadhari sana.

Sasa angalia VIDEO ya mwanamke aliyeshushiwa kipigo na polisi na baadae kuvuliwa nguo zake.

VIDEO - Jeshi la Misri Lamvua Nguo Mwanamke Mwandamanaji
<iframe style="width: 490px" height="315" src="http://www.youtube.com/embed/wW-PEYT1Hu4?rel=0" frameborder="0" allowfullscreen=""></iframe>

<tbody>
</tbody>
 
Last edited by a moderator:
6132970.jpg

Mwanamke mwandamanaji alivyoshushiwa kipigo
Tuesday, December 20, 2011 10:30 PM
Katika hali ya kusikitisha na kukatisha tamaa, Polisi wa kijeshi (MP) wa Misri wamemtandika hadi kumuacha uchi mwanaharakati msichana aliyekuwa katika mshikamano wa kupinga utawala wa kijeshi na serikali ya kuokoa taifa la Misri.
Kuna mgawanyiko mkubwa miongoni mwa raia wa Misri kuhusiana na tukio hili. Kwa upande mmoja wanaharakati wanaopinga utawala wa kijeshi wanaona jeshi limetumia nguvu kupita kiasi na wanalitaka liondoke madarakani mara moja na nchi ikibadhiwe kwa waandamanaji.

Na upande wa pili unaoungwa mkono na raia wengi wa Misri wanaona kuwa jeshi limetekeleza wajibu wake na wanaliunga mkono liendelee kushika madaraka hadi utakapomaliza uchaguzi wa haki usio na uchakachuaji unaoendelea hivi sasa, ambapo matokeo yanaonesha kuwa vyama vya mlengo wa Kiislam vikiongoza kwa asilimia zaidi ya 65 ya viti vyote vya bunge vilivyogombaniwa hadi sasa.

Nifahamishe inatumia nafasi hii kuwatuliza ndugu jamaa na marafiki wa watanzania waliopo Misri kuwa ndugu zao wapo salama salimini wakiendelea na mambo yao kama kawaida licha ya utete wa hali ya kisiasa na vurugu za mara kwa mara.

Nifahamishe imeongea na baadhi ya raia wa Tanzania waishio Misri ili kujua maoni yao juu ya hali ilivyo hapa Misri na kuhakikishiwa kuwa vurugu zipo katika maeneo maalum na sana sana katikati ya mji mkuu Cairo, wala hazina madhara makubwa kwao ukiondoa ile hali ya hofu na kujihadhari sana.

Sasa angalia VIDEO ya mwanamke aliyeshushiwa kipigo na polisi na baadae kuvuliwa nguo zake.

VIDEO - Jeshi la Misri Lamvua Nguo Mwanamke Mwandamanaji
<iframe style="width: 490px" src="http://www.youtube.com/embed/wW-PEYT1Hu4?rel=0" allowfullscreen="" frameborder="0" height="315"></iframe>

<tbody>
</tbody>


Hawa ni wanyama, sio watu. Mwanamke anakabiliwa na wanyama wote hawa.
 
Last edited by a moderator:
inasikitisha sana hivi unawezaje kumpiga mwanamke kama mnyama,hivi watu hawajui hawa ndio mama zetu,ipo siku watajutia kitendo walichofanya
 
Inasikitisha sana. Nadhani hii kitu lazima iondoke na mtu, yaani wamemvua na yule jamaa kamkanyaga kwa mabuti usoni na kifuani then akajifanya kukimbia halafu akarudi. Poleni Egypt. Nadhani kwa hali hii naona bora hata Mubarak hakupaswa kufikishwa mahakamani kwani naona hawa jamaa ni zaidi ya Mubarak
 
Hakika hao wanajeshi ni zaidi ya wanyama! Maana wana akili na utashi lakini wanatenda hayo kama hayawani vile.
 
Back
Top Bottom