- Source #1
- View Source #1
- Source #2
- View Source #2
Wakuu nimekutana na hii video mtandaoni mara nyingi na inadaiwa kuwa ni kivuko cha kigamboni ambapo watu wakishuka huwa wanakimbia kwa spidi kama inavyoonekana kwenye video hiyo. JamiiCheck uhalisia ni upi?
- Tunachokijua
- Kumekuwapo na video inayosambaa mtandaoni ikiwaonyesha abiria wakishuka kwenye kivuko huku wakikimbia kwa kasi, ikidaiwa kurekodiwa maeneo ya Kigamboni, Dar es Salaam.Rejea picha hii ili kubaini ufanano wa vivuko hivi.
Ukweli wa video
Ufuatiliaji wa kimtandao uliofanywa na JamiiCheck kwa kutumia Google Reverse Image Search ulibaini picha ya kivuko kutoka Kenya, inayofanana na ile iliyo kwenye video inayodaiwa kutoka Kigamboni. Picha hiyo ilichapishwa kwenye ukurasa wa Ferry Kenya , ambao hutoa huduma za feri katika vivuko vya Likoni na Mtongwe - Bandari ya Kilindini, Mombasa.
Zaidi ya hayo, video iliyochapishwa kwenye mtandao wa TikTok na mtumiaji anayetumia jina la @soljaboyib inaonyesha eneo baada ya kushuka kwenye kivuko ambapo gari la rangi ya njano linaonekana, ambalo awali lilionekana upande wa kushoto wa video hiyo, ambayo inadaiwa kutoka Kigamboni.
Kadhalika, kwa kutumia Google Earth , ikibainishasha kuwa ni Mombasa nchini Kenya, inaonyesha kuonekana kwa eneo hilo mwaka wa 2023 wakati hapakuwa na mmea, ambayo ni sawa na eneo lililoonyeshwa na mmea kwenye video.
Kwahiyo video ya kivuko hicho, abiria wakishuka huku wakikimbia, si ya Kigamboni, Dar es Salaam bali ni kutoka Mombasa, Kenya.