Vicky Mtetema & Flora Nducha wa BBC Waula!

Kieleweke,

Na kuajiriwa kwa Asha Rose Migiro UN ni kwa ajili ya automtic-favor?


Mkuu, soma post yangu vizuri. Kuna wakati nilipoituma network ilileta problem ikaja robo na hivyo nikaiedit. Pitia hapa upya hapa chini.

 

No research no right to speak!

Umefanya research gani ukaona watanzania tuko nyuma kihivyo? Umeangalia nchi zote za Africa, Africa mashariki ama kusini mwa jangwa la sahara???????????????????????Tusijibeze watanzania jamani, hata mwenye chongo ana nafuu kwa kipofu

Wewe unataka tushindane na wazungu wakati ujaangalia continental-wise? Hata mbuyu ulianza kama mchicha mzee. Ebu ilinganishe Tanzania na nchi nyingine za Africa kwanza kabla ya kuanza kubeza hizo post wanazopata ndungu zetu na kudai haziwafai!

Vicky Mtetema amepata post hiyo baada ya hile research/study yake kuhusiana na biashara ya Albino na wala si kwamba kwa sababu Albino wako Tanzania. Mara ngapi tumeona project kibao lakini country directors wanakuwa Wazungu direct hata kama zinashughulikia matatizo ya watanzania? Mfano miradi ya malaria n.k? Yule Albino, President wa "Under The Same Sun" alipeleka ile study Canada, Weupe wakamkubali Vicky na kuamua kumpa U-country Director! So dont just write Mr. Great Thinker!

Kuhusu huyo bwana aliyeenda kufanya presentation Korea! Ulifuatilia kujua theme ya presentation ilikuwa ni nini ama ilikuwa ni open presentation? Na kama ilikuwa ni open presentation kuna tatizo gani mtu kupresent kitu anachofikiri ni right? Wewe ulitaka a-present nini?
 

Theme ya presentation ya yule jamaa ndiyo ilinifanya nishange kwa alicho-present. Vinginevyo nisingeshangaa.

Soma vizuri thread yangu uone kama sijawataja watanzania waliothubutu. Kumbuka Salim hakushinda ile competition ya UN-Secretary General lakini nimempa credit na aliporudi tuliimba mashairi kumpongeza.

Inawezekana na wewe hujafanya research kuona ninachosema. Ninachokisema hakina tofauti na walichokisema Rais Kikwete na Dr. Asha Rozi Migiro.

Aliyeanza ni Kikwete alipopata tu urais akatamka watanzania wagombanie ajira kwenye UN agencies kwani na sisi tunalipa fee huko kama mataifa mengine. Ingawa JK aliongeza contetx kwamba watanzania walioko kwenye agency hizo hawawaambii wenzao availability ya post hizo.

Wakati JK anasema hayo Migiro alikuwa bado Foreign Minister. Siku chache alipohamia UN Asha Migiro akarudia kilekile alichokisema JK. Nadhani ilimstua kuona hali aliyoikuta huko kwamba ajira zinashindaniwa na wenzetu.

Hivyo siko tofauti na hao hata kama nimetumia source na utafiti wangu.

Unasema Mtatema kafanya research yake kuhusu biashara ya albino. Mkuu mbona unarud palepale Mimi ninauliza tena ukitaka kufanya research ya biashara hiyo unadhani ni nchi gani umeikia albino wakiwindwa kwa wingi. Ni nchi gani ambapo viongozi wa dini wametenga sala kuombea ukomeshaji wa mauaji ya albino.

Ni nchi gani ambako waziri mkuu alitoa machozi bungeni kwa ajili ya mjadala wa albino?

Unamkumbuka yule mkurugenzi mkuu wa Celtel iliyouja kuitwa Zain kwamba ni mtanzania.

Nilimalizia kauli yangu kwa kusema sisi tuna akili sawa na wazungu lakini tusibweteke na yale yanayohitajika lakini tunayoyajua.

Kiswahili, Umaskini, mauaji ya albino, vimejikita nchi gani?
Kama huamini basi weka neno "kiswahili" uone google itakuletea nchi gani.

Ukimaliza hapo weka maneno "albino killings" kwenye google halafu uone ni nchi gani itatokea sana. Unajuaje kuwa huyo bosi wa tasasi ya Ualbino hakuanza kwa kufanya hivyo?
 
Bw. Kieleweke, hoja zako ni sawia kabisa..ila nionavyo itachukua muda sana mtu mwenye kichwa kigumu kama jiwe kukuelewa.

Ila usikate tamaa kuwajuza.
 
Hongereni sana Flora na Vicky..wishing you all the best in your new roles
 

Mi naona umemtaja Dr. Salim, labda unieleze watanzania wengine ni wapi ulowataja?

Kwa hiyo wewe kufanya kazi ama kushikilia post anayoshikilia Mzungu ndo kupiga hatua? Nimekwambia kwenye post yangu kwamba umeilinganisha Tanzania na nchi gani Africa hadi useme Watanzania hawashikilii international post? Je Tanzania ni ya ngapi if you are to rank it? Do you have the database of all UN or international TZ employees starting with just a mere Personal Secretarty? Au mpaka mtu awe UN General Secretary? Umeangalia AU kuna wabongo wangapi pale Addis Ababa? Naona unaongelea wazungu tu? Go to UN agencies website, be it UNDP, WFP, UNHCR, UNICEF, FAO, mention any, then uniambie watanzania hawapo ama wakienda wanachemka kuliko wakenya waganda, weamalawi, warundi ama wazimbabwe! U dont need to generalise kwa information za kuokota baa tu, go back to your desk come with facts here!

Unaposema niangalie kwenye google Kiswahili kinazungumzwa nchi gani na ndio maana Flora kapata hiyo post, Unajua Boss wa BBC Idhaa ya Kiswahili Londoni anatoka nchi gani? Anayemli-place Vicky Mtetema ofisi ya Dar, usishangae hatatoka Tz pia.
 
Bw. Kieleweke, hoja zako ni sawia kabisa..ila nionavyo itachukua muda sana mtu mwenye kichwa kigumu kama jiwe kukuelewa.

Ila usikate tamaa kuwajuza.


Mkuu Abdulhalim, inapobidi kukata tamaa inabidi iwe hivyo. Sasa kama nimetaja kwamba Kikwete na Migiro wanalalamika vilvile mwenzetu kama huyu hapa chini tutamsaidia vipi!

 

Sasa na wewe si uwataje kuliko kuongeza blah blah ya kusema kuna post hii kuna post ile. Mbona na wewe unaishia kumtaja Flora Nducha tu.
 
Mi naona umemtaja Dr. Salim, labda unieleze watanzania wengine ni wapi ulowataja?


Mkuu, nakusbiri uwataje. Lakini ukiwataja usisahau na wale wanaofanya kazi za kufagia vyoo au kukata miwa mashambani.

Taja na wanajiriwa kama ma-houseboy au kuuza kwenye supermarket na wengine kuleta watoto au Nursery-Kindergaten.

Kumbe list ni ndefu. Tunawasubiri.
 
Mi naona umemtaja Dr. Salim, labda unieleze watanzania wengine ni wapi ulowataja?


Unajua wewe bwana mzee, unadhani unatetea kumbe unawadidimiza hao unaowatetea. Hebu taja detail za hao unaowaona wanaleta sifa huko nje uone huko waliko hawako kwenye institution mbayo ni affiliated na Tanzania.

Maana ya kwamba aidha inatoa misaada, au inafanya research. Tafuta hao walioko hata huko UN je si zile section ambazo zinatakiwa uelewa wa nchi masikini kama yetu.

Je hapo kuna utaalamu wowote hapo wakati umasikini ndiyo mazingira yetu? Je kwa kiswahili kama ni utangazaji au hata kufundisha Kiswahili University of Havard hivi hili ni jambo la kujivunia kweli.

Hivi unawajengea nini watu hawa. Wataingia kweli kwenye world competition. Nani duniani ana-compete kujua Kiswahili na kwa kipi Tanzania tunachochangia katika uchumi wa dunia hii.

Nitamsifu vipi mchina kuajiriwa ITV iwapo Mengi ataanzisha idhaa ya kichina.

Hivi ni kweli tumekuwa vilaza kwa masuala mengine. Je kuna kampuni zetu zinagombaniwa Brazil, Sweden, Swizlerland, Cambodia au wapi.

Mkuu unataka tuanzie Afrika ndipo tupande juu. Mbona shuleni tulisoma sylabus zilezile na tulisoma mambo yaleyale bila kujali eneo tulilotoka.

Sisi hatwacheki. TUnataka kuwapa moyo kwamba hata makubwa yanawezekana tujipinde migongo yetu kwenye research. Labda kama hatujiamini kwamba tuna wasiwasi hata mashuleni hatukufaulu bali tulikuwa tunadesa.
 
Mkuu Abdulhalim, inapobidi kukata tamaa inabidi iwe hivyo. Sasa kama nimetaja kwamba Kikwete na Migiro wanalalamika vilvile mwenzetu kama huyu hapa chini tutamsaidia vipi!

Naona unamtaja sana Kikwete, mara Oh hata Kikwete kaongea! Nafikiri hili ndilo linakufanya ushikilie hoja yako kisa Raisi wa nchi kaongea! At JF, matter/arguments are critically discussed, no matter the statement come from the President!
 
Sasa na wewe si uwataje kuliko kuongeza blah blah ya kusema kuna post hii kuna post ile. Mbona na wewe unaishia kumtaja Flora Nducha tu.

Wabongo bwana, unataka nikutafunie umeze???

Sinimekutajia hayo maeneo? Jaribu kufuatilia! ama unataka orodha ya majina?? Acha uvivu wa kitanzania, keep googling!
 

Kazi ni kazi mkuu mradi mkono uende kinywani? Kweli exposure ni muhimu! Wewe hujasikia kuna professional housekeepers?

Wewe kazi yako ni ipi mzee?
 
Hivi unawajengea nini watu hawa. Wataingia kweli kwenye world competition. Nani duniani ana-compete kujua Kiswahili na kwa kipi Tanzania tunachochangia katika uchumi wa dunia hii.

Nchi ngapi za Africa zinachangia kwenye global economy? Naona hata statistics za umasikini wa Tanzania huna hadi unafikiria iwe kwenye level ya juu ya kuchangia katika uchumi wa dunia!

Nitamsifu vipi mchina kuajiriwa ITV iwapo Mengi ataanzisha idhaa ya kichina.

Sisi hatuhitaji kumsifu Mchina ila Wachina watakuwa na haki ya kumsifu just like ninavyowapa Hongera Vicky na Flora! Try to understand the issues, dont rush to comment!

Hivi ni kweli tumekuwa vilaza kwa masuala mengine. Je kuna kampuni zetu zinagombaniwa Brazil, Sweden, Swizlerland, Cambodia au wapi.

Why not Nigeria or South Africa first? Dont be Euro-centric bwana!

Mkuu unataka tuanzie Afrika ndipo tupande juu. Mbona shuleni tulisoma sylabus zilezile na tulisoma mambo yaleyale bila kujali eneo tulilotoka.

Charity begins at home Man/Woman!
 
All the best dada zetu mkaitangaze Tanzania vyema uko muendako
 

Refer to reds.

Red-01: (umasikini wa Tanzania ):
Cha msingi unalikubali hilo na hutalitolea stats.

Red-02: (Sisi hatuhitaji kumsifu Mchina):
Wewe na wenzako ambao akili zimegoma kujua rangi si qualification ya kumsifia mwanadunia mwenzako. Dunia nzima ilimuona Salim Ahmed Salim ni jabari isipokuwa wamarekani tena Jimmy Carter tu aliyepiga kura ya veto.

Red-03: (Dont be Euro-centric):
Nani kakwambia kwamba kuwa Euro-centric ni dhambi. Si ndiyo maana nilikujua wewe ni kitchen-party-centric au harusi-centirc na nikakuweka katika kundi hilo mapema.

Mwisho wa yote hebu badili jina maana unachafua maana halisi ya Mjasiriamali. Mjasiriamali Shupavu ni yule anayejasiriamali kona zote za dunia na haogopi kujificha uvunguni kulikobatizwa jina Charity-at-Home.

Unatuzuga Home yako ni Africa tuanzie huko wakati East Africa yenyewe kwako maji marefu. Si umeona Museveni alivyopigwa chenga ya mwili na watu kama nyinyi alipokuja na sera yake ya aliposema Political Federation in 2012.

Mjaluo Laira Oginga alitushangaa akaja na mbinu ya kutubembeleza huku akijua weakness yetu akisema tusiwaogope Wakenya lakini hakufanikiwa kwani mliwaogopa kama ukoma wote walio hug hiyo idea.

Warundi na wanyarwanda pamoja na udogo wao waliwashangaa lakini kwa vile walitaka na wao wawemo hawathubutu kusema neno. Subiri quoram yao itimie miaka ijayo uone kama watawasubiri au kuwabembeleza.

Watawashiti na nyie mbaki mnapigizana kelele na wale wenzenu mnaopenda kuitana nyinyi ni nchi au siyo nchi.
 

Big Up ladies. Do your thang!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…