Hasa babamkwe akiwa timu pinzani ndugu!!!!
Ok...Nilifikiri unambembeleza babamkwe asilie...akikomaa na wewe itakuwaje? teh teh teh...hakuna mzee mjini Dar. Uzee mwisho Chalinze.
Hahahaaaaaa! Nimesema hapo ni MKOLONI full! Hawezi labda atakuwa anijisevia MIJIMAMA ya enzi zile!
Tena wale wa moshi ndo kabisaa...au hujui mambo yalivyokuwa yanakwenda? Uzee mwisho chalinze...kaa chonjo mjini hapa.
Khabari Wanajamviii!!!
Mie mzima, ila ndo hivo tena husikeni na kichwa cha habari hapo juu!!!
Mi ni mdada kati ya wadada wachache wanazi wa soka, si la nje si la ndani, yote nimo. Huko nje niulize Ligi gani nisiyofatilia Si Premier League, La Liga, Seria A, Bundensliga (Unabisha nini?) hadi League 1 bila kusahau FA na UEFA!!!! Njoo bongo mimi Yanga Damuuu!
Kijamii haipendezi binti kuwa shabiki wa mpira namna hiii! Unaweza kukosa mume atiii hasa akiwa timu pinzani!!! LOL! Kama mjuavyo mpira gharama sana, DST ya SS chanel si mchezo, hivo siku za ball inabidi kutafuta ustaarabu! Kuna mtu wangu tuna date bana! Kwao mambo poa, Kitu LG Flat Screen, Nchi kibao, LED, High Definition, Crystall Clear, DST full Package afu hakuna kelele za bar, ila shurti tuangalie mpira na Dingi yake a.k.a Bamkwe!!!! Mpo Hapo?
Mi nikakubali, kwani Babamkwe anang'ata? Simba mkali ila anazaa vile vile! Ila Dingi Mchaga Mkoloni Haswaaaa! Mi kufika pale na vitenge vyangu (niliombwa nizingatie itifaki ya kwenda ukweni!!! LOL!) Dingi kaniuliza mama wewe timu gani? Machale yakanicheza!!! Mi chelsea Damuuuu, afu inafatia Arsenal! Ila nikamtega Mkwe! Baba kwani we timu gani? Dingi kafunguka Mi Man UTD damuuu! Nilisoma textiles Manchester sijui chuo gani, BLAH! BLAH! BLAH!
Nikaona ishakuwa soo, ngoja NIHAMIE KUSHABIKIA MAN UTD kwa MKOPO, basi nikajifanya MAN U damu, full kuwataja kina Andy Cole na Dwight York, sio Robie Kean, hadi mkongwe Teddy Sherigham, scholes ndani, bonge nyanya Rooney ndani, hadi Sung Park nikamtaja, hata Rafael na mwenzi wale madogo mapacha mmoja kahamishwa kwa mkopo, ndani ya story, Beckham Hakusahaulika hadi Peter Shmichael alikumbukwa!!! RVP nae ndani ya stori. Basi Dingi akanidhibitisha pasi shaka lolote mie ni MAN UTD Damuu! (CHEZEA KUMUIPRESS MKWEO KIFOOTBALL?)
Ball likanzaa kama kawa Totenhama Hot Spurs wakawa wanagawa DOZI NENE, Bonge nyanya Rooney hoi, nafurahije, japo usoni nipo kihuzuni!! Ikaendelea, Dingi anasunya tu, hadi akaanza kujidunga mzinga wa konyag, mie roho kwatuuuu! Kimbembe THS walipo piga bao la tatu ikawa 3-1 nikajisahaa si NIKARUKA JUUU ! Yeaaaaaah! nikiwa juu nikakumbuka hili soo basi nikamalizia YEAHHHHHH! SHIIIIIIIIIT! STUPID KABISA! Bahati yangu nikiwa katika kuzuga MAN UTD wakarudisha moja!! Salaleeeeee! LOLEST!
Kosa kosa zilivoanza dingi akawa ashanitilia shaka MIMI NI MAMLUKI wa CHELSEA!!! LOL! 5minutes baada ya kurudisha la 2 dingi AKAZIMA TV YAKE NA KUINGIA NA REMOT CHUMBANI. Akamwbia mwanae mpleke hapo Bar mkamalizie kuangalia!!! IMAGINE!!!!! Umamluki wote ukanitoka! LOL! BF alinilaumuje!!! Hadi leo kanuna!! Nikamalizia kwa kucheki score LIVE SCORE na kwa SHAFII DAUDA BLOG!!!
Hapa sina pa KUANGALIA BALL TENA WADAU!! WENYE BIG SCREEN MNIOKOE!!! Mpaka league iishe mbona nitakuwa sina Bwana!!!!
Hahahaaaa! Nashukuru kwa ONYO ila NAJIAMINIA hawezi kunizidi akili, Nimezaliwa hapa hapa MUJINI sikuja na mabegi!!! LOL! na NIMENGANGANIA SO FAR, pamoja na kupata kazi shirika kubwa MKOA nimegoma kwenda!!!! TUTABANANA HAPA HAPA!!!!
Nimepapenda hapo Baba mkwe aliposema anaipenda Man U damu damu becausea alisoma Leeds Varsity mambo ya Textiles hahaha:biggrin:
Kwani hujui ndege mjanja ndio ananaswa na tundu bovu? Kuja na mabegi inaweza kuwa faida kuliko kuzaliwa mjini na kuendelea kuishi kwa mazoea wakati mambo kibao yanabadilika.
lara 1 bana..lol ..yaani msredi wako unavyoupamba utadhani movie vile..
Ndio taabu ya kudanganya hiyo aisee..Kuna siku Jamhuri Morogoro nilikaa jukwaa la Ndala huku mie Msimbazi ebwanaee..nilijikaushausha mwanzoni ila baadaye wachache walinistukia..sema sikuwa na midadi kama yako vinginevyo wangeniua...
Hasa babamkwe akiwa timu pinzani ndugu!!!!
teh teh teh, lara 1 umenikosha sana. mnimeupenda mtiririko wa stori. Haya hebu niambie huko ligue 1 unashabikia timu gani?