Zoezi la ubomoaji vibanda vyote vya biashara katika jengo la Machinga Complex Ilala , Dar es salaam, limewaacha wengi kwenye majonzi.
Wafanyabiashara hao kwa masikitiko zaidi wanasema kubomolewa vibanda vyao vya biashara na uharibifu wa Mali zao ni uonevu na wao hawana la kufanya.
Kuna taarifa zingine zinasema wafanyabiashara hao walitafadhalishwa na uongozi tokea awali kwamba wabomoe vibanda vyao na wahamie ndani ya Jengo hilo la Dar es salaam Business Park, au Machinga Complex.
Wafanyabiashara wamewasha moto katikati ya barabara eneo la Machinga Complex jijini Dar baada ya kukuta vibanda vyao vimevunjwa.
kwa hiyo walikataa kukaa ndani wakaweka vibanda nnje ya jengo la biashara ili watu wasiingie ndani wakija waishie hapo nnje, wao hawalipi kodi huku wanauza, walio ndani wanalipakodi lakini hawauzi.
kwa hiyo walikataa kukaa ndani wakaweka vibanda nnje ya jengo la biashara ili watu wasiingie ndani wakija waishie hapo nnje, wao hawalipi kodi huku wanauza, walio ndani wanalipakodi lakini hawauzi.
jingo lina masharti makubwa na ni gharama ukilinganisha na uhalisia wa biashara. wale jamaaa wamekua mkombozi kwa mtanzania mwenye kipato cha chini. nimefikiria zaidi ya kile ninachokijua
Watanzania tumekuwa tukisingizia sana vyama hata kwenye jambo lililo wazi katika kuvuruga taratibu. Kwanza vile vibanda havikuwepo kwenye plan, na vilikuwa kero sana hata kama walikuwa wanalipa kodi.