Mentor anajaribu kutujulisha kwamba magari yetu haya (Si Verossa tu) yana matumizi mengi. Kuna mengine yanatumika kama guest house kwa kufanya mambo ya ngono. Kuna lift zinatolewa na sugar mummies, kwa wavulana wadogo na kwa lift hizo hao wamama ndani ya Verossa wanawarubuni vijana wadogo, halikadhalika kwa ma-sugar daddy wanavyowarubuni wasichana wadogo kwa ahadi kemkem. Ni katika magari yetu humo humo zinatungwa mimba, yanazalishwa magonjwa mbalimbali ukiwemo ukimwi, frustration za maisha ikiwemo kufeli mitihani zinaanzia humo, kwa sababu wanafunzi wanasahau kusoma badala yake wanakwenda kujirusha kutumia magari hayahaya. Kwa ujumla Mentor ametukumbusha mengi yanayofanyika kwenye magari yetu likiwemo gari la Verossa. Please, observe matumizi ya gari yako.