Uzinzi ni dhambi ya mauti...

Unavyosema ulifanya sana ndo ukaokoka, basi na wengine watasema acha tufanye then tutaokoka.
 
Dhambi inaua!! Dhambi ni mauti??

Kivipi? Hii kitu huwa siielewagi, kwamba mtenda dhambi ndio hufa?

Kama mshahara wa dhambi ni mauti mbona sote tunakufa sasa?
 
Mimi baharia mstaafu nakujuza uzinzi hufubaza akili, unawaza na kutenda chini ya kiwango, huondoa baraka kwa kukufanya mtapanyaji na kubwa jinga, kiroho unakosa dira na kijamii unadharaulika na kupoteza mvuto kiuchumi unapoteza focus, unawaza kustarehe zaidi na kuburudika kuliko kuwekeza maisha mwisho utazeeka maskini wa kutupwa na kuchekwa, kimbia zinaa
 
Zambi zote ni sawa,

Ukiomba msamaha kwa kumaanisha husameheka mbele za Mungu.,
Mungu anasamehe immediately!
Kitu watu hawaelewi ni zile effect za hiyo dhambi ila unakuwa umesamehewa !
Madhara yake yako palepale mpk ujue namna Tena ya kwenda mbele za Mungu Kwa kutumia Damu ya Yesu
Ndo application ya Blood of Jesus utaiona hapa!
 
[emoji120][emoji120][emoji120]fact
 
Mtoa lost unafeli wapi. Yaan niache kukamua papuchi kisa dhambi. Hata ukioa lazima uzini na mkeo ndo mzae. Hata wewe hapo ni matokeo ya kuzini
 
Umedadavua vizuri sana mkuu. Nakushukuru sana tena sana.
 
Kama ulikuwa hujui, mstari mmoja wa Biblia unaweza ukawa na tafsiri zaidi ya moja kulingana na vile Roho Mtakatifu anavokuvuvia kutafsiri mstari huo.

Hata ukisoma 1Wakorintho 14:26 utathibitisha hiki ninachokizungumza hapa.

Biblia siyo Civics kwamba ukiulizwa Tanganyika ilipata Uhuru mwaka gani basi jibu lake ni lazima liwe mwaka 1961.

Kama una hoja weka facts hapa ili ku-prove kwamba sijaisoma Biblia vizuri. Karibu...
 
Reactions: Cyb
Nini maana ya kukufuru?
Ni maneno ya dhihaka, dharau, kejeli, matusi kinyume na Mungu.
Ayubu 2:9 Ndipo mkewe akamwambia,je wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu ukafe.
Walawi 24:16 Na yeye atakayelikufuru jina la BWANA hakika atauawa, mkutano wote watampiga kwa mawe....
Agano la kale(torati) aliyemkufuru Mungu ilimpasa auawe kwa kupigwa kwa mawe.
Agano jipya imeenda zaidi kwa anayekufuru kutosamehewa milele,na na imekuwa specified kumkufuru Roho Mtakatifu.
Kwa tunaoamini kuhusu uungu nafikiri tutaelewa kirahisi kwanini sio Mungu baba,wala Mwana bali Roho Mtakatifu?
Marko 3:28-29 Amin nawaambia dhambi zote watasamehewa wanadamu na kufuru zao watakazokufuru zote,
29.bali mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hana msamaha hata milele ila atakuwa na dhambi ya milele.
Luka 12:10 Na kila mtu atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa,bali aliyemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Kwanini Roho Mtakatifu?
Yohana 16:8 Naye akiisha kuja huyo,atauhakikishia ulimwengu kwa habari ya dhambi,na haki,na hukumu.
Roho Mtakatifu ndiye anayetushuhudia kwa habari ya dhambi zetu,huachilia hali ya kusikia hatia(convict)tunapokosea mioyoni mwetu ili tutubie dhambi zetu kwa toba,hutuelekeza kwenye haki.
Yeye ndiye anayewavuta wenye dhambi kwa kuweka hali ya kujutia makosa yao na kuamua kuokoka.
So Biblia inamaanisha huyo Roho Mtakatifu akifanya hayo yote kwako na kumjua Mungu na kumtumikia chini ya nguvu ya Roho Mtakatifu ukaona kwa dhahiri nguvu na uwezo wa Mungu kwa dhahiri watu wakajua na kukuheshimu kama mtu wa Mungu na shetani amejua,ghafla ukiiacha hiyo neema na kuanza kukufuru matukufu ya Roho Mtakatifu ndio inaitwa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu.
Unakuwa umemhuzunisha na kumnyamazisha ndani yako unasaidikaje?
Unakuwa kama mnyama tu,husikii hali ya hatia,huhisi tena hukumu ukikosea ili utubu nafsi inakuwa imekufa haiwezi kufanywa hai tena maana aletaye hali ili utafute kuwa hai anenyamaza kwa kumnyamazisha makusudi kwa dhihaka,dharau.
2 Petro 2:12 ...Kama wanyama wasio na akili...wakimufuru....wataangamizwa.
Waefeso 6:4 Kwa maana hao waliokwisha kupata nuru na kukionja kipawa cha nguvu,na kufanywa Washirika wa Roho Mtakatifu,
5,na kulionja neno zuri la Mungu na nguvu za zamani ,zijazo
6.Wakaanguka baada ya hayo HAIWEZEKANI kuwafanya UPYA TENA hata WAKATUBU,kwa kuwa wamsulubisha Mwana wa Adamu mara ya pili kwa nafsi zao na KUMFEDHEHI KWA DHAHIRI.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…