ielewemitaa
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 11,016
- 9,720
Target ni tundu lile lile , haya mambo ya uzinzi sijui ndoa ni kukosa kazi
Uwe na moyo mkuu.Najitahidi japo si rahisi
Mtoa mada Mwenyezi Mungu akubariki sana kwa kutukumbusha kuishi vyema kadiri ya maagizo ya Mungu.
Binadamu tuna asili ya kujisahau na ndo hapo shetani huchukua point kutuvuta dhambini, ndio maana Yesu ametusihi tusali kila wakati ili tusiingie dhambini.
Sala ni chakula bora kwa afya ya mwanadamu, pia hutuweka karibu na Mungu hivyo maombi yetu husikilzwa na kujibiwa mapema
Tukimbieni zinaa, mifano hai ipo mitaani hakuna mahusiano yenye uzinzi ndani yake ambayo yanafika mbali, matukio ni mengi kusalitiana, kuuwana yote hutokana na kumchukiza Mungu kwa dhambi ya uzinzi
Sent using Jamii Forums mobile app



Lakini hapa tulipo siyo Mbinguni mkuu.Hili suala la ndoa limekuwa changamoto! Mbinguni hakuna kuoa Wala kuolewa na Wala hutaulizwa ulioa au kuolewa na wangapi??

Mkuu, kama ulichakata mbususu zaidi ya 500, unastahili kutubu kabisaa!
Ujumbe: Tuchakate mbususu kwa hasira kali sana![]()


Hili jambo huwa linanifikirisha sana,,,,, Huwa nawaza zile jamii za Africa ambazo hazija accept hii culture ya western,,,,ina maana wale wote ndio hawataona mbingu,,???? au dhambi zao zitaanza pale siku wakienda wakahubiriwa..???Hizo ni propaganda za westerns kutukwamisha tusizaliane. Haiwezekani tendo la kuunganisha jinsia mbili ili zitoe kiumbe kipya liwe tendo baya.
Favour is my name si unikubali nikuoe tu tushinde hii dhambi 🙏fact
Mkuu nyie si ndo mnawafungaga watu na sheria zenu halafu unasema umeokoka, umekwepa uzinzi lakini dili la kumteketeza mtu kupitia sheria unafanya.


Umeuliuliza maswali mazuri sana mkuu. Huku kwenye Sheria zetu tunasema "ignorance of the law is not a defence", yaani KUTOKUJUA SHERIA SIYO UTETEZI UNAPOTENDA KOSA LOLOTE LA JINAI. Sababu ni kwamba, mchakato wa utengenezaji wa Sheria fulani unashirikisha wananchi kama wadau wa Sheria hiyo; practically, hili halifanyiki (yaani wananchi hawashirikishwi kama tunavyoaminishwa).Hili jambo huwa linanifikirisha sana,,,,, Huwa nawaza zile jamii za Africa ambazo hazija accept hii culture ya western,,,,ina maana wale wote ndio hawataona mbingu,,???? au dhambi zao zitaanza pale siku wakienda wakahubiriwa..???
Linafikirisha sana hili jambo,,,Mungu angetaka iwe hvo nadhani angefanya kama alivyofanya kwenye Maziwa ya Mwanamke,,,Yanatoa maziwa mara tu Mwanamke anapojifungua mtoto,,,...Na hvyo kidume ilitakiwa mashine isimame pale tu wakati sahihi ukifika...
Ni mtazamo tu Wakuu
Habarini za wakati huu wakuu..
Mimi ni kijana wa kiume, umri wangu ni kati ya miaka 30-37, sijaoa. Kwa taaluma ni Mwanasheria. Pia ni mwandishi wa vitabu vya Sheria kwa lugha ya Kiswahili.
Niko JF tangu 2012, ukifuatilia nyuzi zangu nyingi tangu najiunga JF utagundua kwamba zilikuwa zikihusiana na uzinzi huohuo (Biblia inasema kile kimtokacho mtu ndicho kilichoujaza moyo wake), kiukweli nimeandika mabandiko mengi sana humu JF ya kuutukuza uzinzi kwasababu uzinzi ndiyo ulikuwa umeujaza moyo wangu.
Unajua, kwa sisi wanaume, ipo fahari ukiwa na wanawake wengi. Lakini kwenye ulimwengu wa kiroho ipo hatari kubwa mbeleni kuliko hata hiyo fahari ya muda mfupi. Nakushuhudia kwamba ujana wangu nimeutumia kufanya uzinzi/umalaya wa kiwango cha SGR, nimetembea na wanawake wa marika na sifa tofautitofauti. Nimeumiza sana mioyo ya wanawake bila kujua hatari niliyokuwa naikaribia.
Baada ya kupitia changamoto flani ofisini nikajikuta nimeokoka. Mungu alinipitisha kwenye jaribu ambalo lilinifanya nimgeukie yeye kwasababu, kibinadamu nilikosa majibu ya changamoto hiyo, nikajisalimisha kwake, lakini nikiwa wokovuni, dhambi pekee niliyokuwa napambana nayo vikali ilikuwa ni hiyo ya uzinzi na ulevi, nikawa bado nafanya zinaa na kunywa pombe kwa kificho halafu natubu, kuna mambo yangu yakawa hayaendi.
Mimi ni msomaji mzuri sana wa Biblia, msomaji mzuri mno. Nilitambua kwamba ni hatari kufanya dhambi kwa kujua; lakini nikawa napuuza, nikijipa moyo kwamba eti nitatubu baadaye! Kwahiyo nikawa mlokole vuguvugu.
Siku za hivi karibuni nikamuomba Mungu sana anisaidie niushinde uzinzi na ulevi. Sasa naamini kwamba yasiyowezekana kwa mwanadamu yanawezekana kwa Mungu, ni kweli nimefanikiwa kuachana na uzinzi na ulevi, sikatai kwamba majaribu ni mengi hasa kwenye uzinzi, lakini mara zote Mungu ananitengenezea mlango wa kutokea kwenye kila jaribu. Ukiokoka, wadada ndiyo wanajileta kwa wingi hadi inatisha, usipokuwa na nguvu za Mungu unaweza ukasalimu amri!
HATARI ZA UZINZI:-
Kwanza ukisoma Yakobo 4:4 inasema, "Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu?". Kwa lugha nyepesi kabisa ni kwamba, ukizini tu, automatically unakuwa adui wa Mungu.
Ufunuo 21:8 inawataja wazinzi na adhabu watakayokutana nayo huko Mbinguni, lakini mwishoni wa mstari huo wa 8 kuna maneno, "mauti ya pili".
KWANINI UZINZI NI DHAMBI YA MAUTI?
Kwanza nitoe angalizo kwamba hakuna dhambi kubwa wala ndogo. Ila kwa asili, mara baada ya kuwepo kwa misingi ya Ulimwengu, Mungu amekuwa akichukizwa sana na uzinzi (Soma Hesabu 25:1-3).
Uzinzi ni dhambi ya mauti kwasababu, kwetu Wakristo hii miili yetu ni hekalu (makazi) ya Roho Mtakatifu (1Wakorintho 6:19). Mathayo 12:31-32 inasema kwamba dhambi nyingine zote zinasameheka isipokuwa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Kwahiyo ukizini kwa kuutumia huo mwili wako ambao ni hekalu la Roho Mtakatifu unakuwa umemkufuru huyo Roho Mtakatifu aliyeko ndani yako, ataondoka na kukuacha ubaki peke yako.
Lakini pia, dhambi pekee inayofanyika mwilini katika amri 10 za Mungu ni dhambi ya uzinzi, dhambi nyingine zote ni nje ya miili yetu.
Kwahiyo ukizini na mwanamke unafanyika kuwa mwili mmoja naye (1Wakorintho 6:15-16) , kwahiyo kama mwanamke alikuwa na mapepo yanahamia kwa mwanaume, halikadhalika kama mwanaume alikuwa na mapepo yanahamia na kwa mwanamke. Kwa mfano; kama mwanamke/mwanaume unayezini naye ana pepo (roho) ya kukataliwa na wewe unaanza kukataliwa, kama alikuwa na pepo la umasikini, linahamia na kwako pia. So usishangae mambo yakibadilika, tatizo ni huo uzinzi wako.
Kwahiyo vijana wenzangu hasa humu MMU msione ufahari kuzini, mnaziangamiza nafsi zenu wenyewe. Hata Samsoni (Mnadhiri wa Mungu) aliiangamiza nafsi yake mwenyewe kwa uzinzi.
Mwisho, Mtume Paulo kwenye Waraka wake wa kwanza kwa Wakorintho Sura ile ya 7:1-2 anatuambia, tusiwaguse (tusizini na wanawake), lakini kwasababu wanaume tumejawa na tamaa, basi tuoe mke mmoja. Namuomba sana Mungu anitangulie katika mchakato wangu niliouanza wa kupata mke mwema.
Kwa wewe uliyeoa halafu ukazini, hatari ni kubwa zaidi, kwasababu maombi yako hayatajibiwa na Mungu (Soma 1Petro 3:7).
Sensa ya Watu na Makazi ni tarehe 23/08/2022; tujiandae kuhesabiwa, mimi niko tayari, wewe je?
Aksante kwa kusoma uzi wangu na Mungu akutie nguvu uufanyie kazi. Amen!
🤣🤣...serikali iingilie kati mahari mwisho iwe laki 2 tuu kwa wale ambao sio bikra na million 10 kwa wale ambao ni bikra
Kwanza Yesu mwenyewe alikuwa anakunywa divai wewe nani unakemea kulewa, kuwa na wanawake wengi bibilia haijazuia imeruhusu tuwaoe wwngiHabarini za wakati huu wakuu..
Mimi ni kijana wa kiume, umri wangu ni kati ya miaka 30-37, sijaoa. Kwa taaluma ni Mwanasheria. Pia ni mwandishi wa vitabu vya Sheria kwa lugha ya Kiswahili.
Niko JF tangu 2012, ukifuatilia nyuzi zangu nyingi tangu najiunga JF utagundua kwamba zilikuwa zikihusiana na uzinzi huohuo (Biblia inasema kile kimtokacho mtu ndicho kilichoujaza moyo wake), kiukweli nimeandika mabandiko mengi sana humu JF ya kuutukuza uzinzi kwasababu uzinzi ndiyo ulikuwa umeujaza moyo wangu.
Unajua, kwa sisi wanaume, ipo fahari ukiwa na wanawake wengi. Lakini kwenye ulimwengu wa kiroho ipo hatari kubwa mbeleni kuliko hata hiyo fahari ya muda mfupi. Nakushuhudia kwamba ujana wangu nimeutumia kufanya uzinzi/umalaya wa kiwango cha SGR, nimetembea na wanawake wa marika na sifa tofautitofauti. Nimeumiza sana mioyo ya wanawake bila kujua hatari niliyokuwa naikaribia.
Baada ya kupitia changamoto flani ofisini nikajikuta nimeokoka. Mungu alinipitisha kwenye jaribu ambalo lilinifanya nimgeukie yeye kwasababu, kibinadamu nilikosa majibu ya changamoto hiyo, nikajisalimisha kwake, lakini nikiwa wokovuni, dhambi pekee niliyokuwa napambana nayo vikali ilikuwa ni hiyo ya uzinzi na ulevi, nikawa bado nafanya zinaa na kunywa pombe kwa kificho halafu natubu, kuna mambo yangu yakawa hayaendi.
Mimi ni msomaji mzuri sana wa Biblia, msomaji mzuri mno. Nilitambua kwamba ni hatari kufanya dhambi kwa kujua; lakini nikawa napuuza, nikijipa moyo kwamba eti nitatubu baadaye! Kwahiyo nikawa mlokole vuguvugu.
Siku za hivi karibuni nikamuomba Mungu sana anisaidie niushinde uzinzi na ulevi. Sasa naamini kwamba yasiyowezekana kwa mwanadamu yanawezekana kwa Mungu, ni kweli nimefanikiwa kuachana na uzinzi na ulevi, sikatai kwamba majaribu ni mengi hasa kwenye uzinzi, lakini mara zote Mungu ananitengenezea mlango wa kutokea kwenye kila jaribu. Ukiokoka, wadada ndiyo wanajileta kwa wingi hadi inatisha, usipokuwa na nguvu za Mungu unaweza ukasalimu amri!
HATARI ZA UZINZI:-
Kwanza ukisoma Yakobo 4:4 inasema, "Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu?". Kwa lugha nyepesi kabisa ni kwamba, ukizini tu, automatically unakuwa adui wa Mungu.
Ufunuo 21:8 inawataja wazinzi na adhabu watakayokutana nayo huko Mbinguni, lakini mwishoni wa mstari huo wa 8 kuna maneno, "mauti ya pili".
KWANINI UZINZI NI DHAMBI YA MAUTI?
Kwanza nitoe angalizo kwamba hakuna dhambi kubwa wala ndogo. Ila kwa asili, mara baada ya kuwepo kwa misingi ya Ulimwengu, Mungu amekuwa akichukizwa sana na uzinzi (Soma Hesabu 25:1-3).
Uzinzi ni dhambi ya mauti kwasababu, kwetu Wakristo hii miili yetu ni hekalu (makazi) ya Roho Mtakatifu (1Wakorintho 6:19). Mathayo 12:31-32 inasema kwamba dhambi nyingine zote zinasameheka isipokuwa dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu. Kwahiyo ukizini kwa kuutumia huo mwili wako ambao ni hekalu la Roho Mtakatifu unakuwa umemkufuru huyo Roho Mtakatifu aliyeko ndani yako, ataondoka na kukuacha ubaki peke yako.
Lakini pia, dhambi pekee inayofanyika mwilini katika amri 10 za Mungu ni dhambi ya uzinzi, dhambi nyingine zote ni nje ya miili yetu.
Kwahiyo ukizini na mwanamke unafanyika kuwa mwili mmoja naye (1Wakorintho 6:15-16) , kwahiyo kama mwanamke alikuwa na mapepo yanahamia kwa mwanaume, halikadhalika kama mwanaume alikuwa na mapepo yanahamia na kwa mwanamke. Kwa mfano; kama mwanamke/mwanaume unayezini naye ana pepo (roho) ya kukataliwa na wewe unaanza kukataliwa, kama alikuwa na pepo la umasikini, linahamia na kwako pia. So usishangae mambo yakibadilika, tatizo ni huo uzinzi wako.
Kwahiyo vijana wenzangu hasa humu MMU msione ufahari kuzini, mnaziangamiza nafsi zenu wenyewe. Hata Samsoni (Mnadhiri wa Mungu) aliiangamiza nafsi yake mwenyewe kwa uzinzi.
Mwisho, Mtume Paulo kwenye Waraka wake wa kwanza kwa Wakorintho Sura ile ya 7:1-2 anatuambia, tusiwaguse (tusizini na wanawake), lakini kwasababu wanaume tumejawa na tamaa, basi tuoe mke mmoja. Namuomba sana Mungu anitangulie katika mchakato wangu niliouanza wa kupata mke mwema.
Kwa wewe uliyeoa halafu ukazini, hatari ni kubwa zaidi, kwasababu maombi yako hayatajibiwa na Mungu (Soma 1Petro 3:7).
Sensa ya Watu na Makazi ni tarehe 23/08/2022; tujiandae kuhesabiwa, mimi niko tayari, wewe je?
Aksante kwa kusoma uzi wangu na Mungu akutie nguvu uufanyie kazi. Amen!