Uzinzi ni dhambi ya mauti...

Hicho ndicho kilichoandikwa kwenye Biblia. Siyo msimamo wangu.
Japo kimeandikwa ila umetafsiri kwa hisia zako, hatari ya hiyo tafsiri yako ni kuwa watu watadhani dhambi ya uzinzi ndo dhambi isiyosameheka. Kumbe dhambi hiyo inasameheka na inaondolewa kwa kitubio kupitia damu ya Yesu Kristu.
 
million 10!? Kwan hiyo bikra Ina nini hasa
 
Nakazia hapa,1 Wakorintho 6:18-Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe....
 
million 10!? Kwan hiyo bikra Ina nini hasa
Hii ni ili wazazi wajitume zaidi katika kuhakikisha watoto wao wa kike wanakuwa sio breki pumbuz.
Its a virtue being virtuous and should be dully rewarded!
 
Nakazia hapa,1 Wakorintho 6:18-Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe....
Barikiwa sana kwa kufuatilia mkuu.
 
kabisa na hilo linaeleweka ila pale unapo onyesha jitihada za makusudi kuushinda uzinzi basi utakuwa kwenye njia salama kabisa. endelea hivyo hivyo.
Asante na ubarikiwe sana
 
Japo kimeandikwa ila umetafsiri kwa hisia zako, hatari ya hiyo tafsiri yako ni kuwa watu watadhani dhambi ya uzinzi ndo dhambi isiyosameheka. Kumbe dhambi hiyo inasameheka na inaondolewa kwa kitubio kupitia damu ya Yesu Kristu.
Mkuu, neno la Mungu ni siri. Na kwa mujibu wa Biblia yenyewe (1Wakorinto 14:26) inasema, kila mtu ana tafsiri yake juu ya neno la Mungu kulingana na namna anavovuviwa na Roho Mtakatifu.

Bilashaka hujauelewa vizuri uzi wangu, sasa kama dhambi ya uzinzi haisameheki, kivipi mimi niseme nimeokoka (nimesamehewa dhambi) na nilikuwa mzinzi wa kupindukia?

Labda niweke kumbukumbu sawa, hakuna dhambi isiyosameheka, damu ya Yesu iliyomwagika Msalabani ndiyo upatanisho wetu kwa Mungu (1Yohana 2:1-2).

Biblia imetumia lugha kali ya utisho (kutokusameheka), ili kuonyesha gadhabu ya Mungu juu ya dhambi hii ya uzinzi ikifanyika kwa mazoea eti kwasababu kuna msamaha, lakini ukiomba msamaha wa dhati kwa Mungu na kuahidi kutoirudia tena basi atakusamehe kwasababu yeye ni mwaminifu na wa haki.
 
Nikupe hongera kwa uamuzi wako wa hekima ku-surrender kwa Mungu.
Nikushauri kidogo tu,
1. Fahau kuoa sio solution la kushinda uzinzi.Utaendelea kujaribiwa mpaka proven victorious kwenye eneo hilo,na zipo njia za kuku-sustain ushinde, know them.
2. Kubali kuwa mwanafunzi ufundishwe ili uukuliwe wokovu(watch out na mafundisho potofu as we live at the end of edges).
Matendo 8:26-34..
Verse 31. Akasema nitawezaje kuelewa,mtu asiponiongoza?Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.
(Ni habari ya yule towashi kutoka Kushi/Ethiopia ambaye Filipo alimsaidia kuelewa alichokuwa anakisoma kwenye chuo Cha nabii Isaya).
Siwezi kuweka hapa maana ya kumkufuru Roho Mtakatifu kimaandiko nafikiri sio mahali sahihi sana.
Incase utahitaji waweza kunicheki pm.
Mungu akubariki na kukupa ushindi wa kuushinda mwili na tamaa zake, through him we are more than the conquerors.
 
Mkuu, kwanza nikushukuru sana kwa mchango wako mzuri. Kabla sijakufata PM na kwa faida ya wengine pia, naomba uziweke hapa njia za kuniwezesha kushinda. Tafadhali sana...
 
Mkuu, kwanza nikushukuru sana kwa mchango wako mzuri. Kabla sijakufata PM na kwa faida ya wengine pia, naomba uziweke hapa njia za kuniwezesha kushinda. Tafadhali sana...
Atiririke tuko wengi tungependa kuzijua hizo njia...
 
Injili kwa mataifa yote Mkuu.
 
Tumia akili yako kujua kama usinzi ni dhambi. Eva aliletwa kwa Adam, wakazaana na kuijaza Dunia. Ninachojua kubaka ni kosa, unalazimisha. Hiyo starehe kaweka Mungu. Mme au mke wa mtu ni kosa, nimemaliza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umesema hujasoma uzi wote halafu umesha-conclude! Huenda jibu la swali lako lipo kwenye content ya uzi wangu.

Now I have come to a conclusion that EVEN COMMON SENSE IS NOT COMMON.
Hilo neno la mwisho kuna ticha wetu moja wa majengo sec moshi alikuwa anapend sana kulitumia..... any way tupo hapa kupeana challenge tu ....
 
Asante kwa kutukumbusha mkuu!. Barikiwa sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…