Zulu Man Tz
Member
- Sep 23, 2020
- 73
- 99
Utangulizi.
Dira ya 1 ya Maendeleo ya Taifa ni ya Mchakato wa mwaka 1969 ambayo ilitoa tathmini ya Maendeleo kuanzia Mwaka 2000-2025. Takribani miaka 22 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa ikitekekeza dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025. Tume ya uratibu, uhariri, uandishi, uchambuzi na usambazaji wa Dira hiyo ya Maendeleo 2025 iliyoongozwa na Mwenyekiti Dr. Donas Kibogora.
Mipango ya Dira ya 2025.
Mipango hii ilitazamiwa kufikisha Taifa Uchumi wa kipato Cha kati 2025. Mipango hiyo ilikuwa kama ifuatavyo;
1. Maisha bora na mazuri
2. Amani, utulivu na umoja
3. Utawala na uongozi bora
4. Jamii iliyoelimika na inayopenda kujifunza zaidi
5. Uchumi shindani na imara.
Mafanikio ya Dira ya 2025
1. Serikali ya Tanzania kuingia uchumi wa Kati hadhi ya chini na hali ya umasikini umepungua kutoka 35.7% mwaka 2001 mpaka kufikia 24.6% mwaka 2017/2018. Hapa kipato Cha mtu mmoja mmoja kimeongezeka kutoka Us$1036 mpaka Us$4045 Mwaka 2020.
2. Wastani wa kuishi umeongezeka kutoka miaka 51 mwaka 2000 mpaka kufikia miaka 67 mwaka 2022.
3. Vifo vya kinamama vimepungua kutoka 854 kwa vizazi 100,000 na vifo 99 kwa vizazi 1,000 Mwaka 2000 hadi vifo 524 kwa vizazi 100,000 na vifo 36 kwa vizazi 1000 Mwaka 2020.
4. Kiwango Cha udahili wa wanafunzi wa shule ya msingi kimeongezeka kutoka 58.8% Mwaka 2000 mpaka kufikia 95.7% Mwaka 2020.
5. Upatikanaji wa Maji safi umeongezeka kutoka 50% Mwaka 2000 hadi 86.7% mwaka 2020 kwa mijini na 55% kwa Mwaka 2000 hadi 72.3% Mwaka 2020 kwa vijijini.
6. Upatikanaji wa nishati ya umeme umeongezeka na kufikia 59.8% kwa Mwaka 2020.
Changamoto ya Dira ya Maendeleo 2000/2025
1. Kudorora kwa Uchumi wa Dunia mwaka 2007-2008.
2. Ugonjwa wa uviko 19 Mwaka 2020/2021 na Uchumi ulipungua kutoka 7% Mwaka 2019 mpaka kufikia 4.8% Mwaka 2020.
3. Mabadiliko makubwa ya Tabia ya Nchi.
4. Vita vya Urusi na Ukraine.
Chimbuko la Maandilizi ya Dira la 2050.
1. Kuelekea ukomo wa utekelezaji wa dira ya 2025.
2. Kuendeleza mafanikio yaliyofikiwa Kutokana na utekelezaji wa Dira 2025.
3. Uhitaji wa mkakati na mabadiliko ya teknolojia yanayoendelea kuibuka Ulimwenguni kama Blue economy, matumizi ya roboti, Biashara ya hewa ukaa na Blockchain technology.
4. Uhitaji wa mikakati utakaoainisha Agenda ya Maendeleo ya Nchi na mikakati mingine ya Umoja wa Mataifa, AU, EAC na SADDC etc.
Maandilizi ya Dira 2050 yatajumuisha hatua kuu tatu nazo ni:
1. Maandilizi ya Awali na mapitio
2. Usanifu, uchambuzi na uandishi wa Dira.
3. Uidhinishaji, Uzinduzi na usambazaji wa Dira.
1. Uwezo wa kutumia teknolojia mpya kama vile AI, Blockchain, Machine learning, loT na Fintech hasa kwny mifumo ya elimu yetu.
2. Watanzania wenyewe wawe waendeshaji wa ubunifu na utekelezaji wa mifumo bora ya Serikali Mtandao.
3. Uzalishaji wa vifaa vya kielectronics kwa kuwa Tanzania tuko na utajili wa madini ya kimkakati (critical minerals).
4. Matumizi ya nishati mbadala ili kulinda Mazingira yetu adhimu ya asili ya uoto.
5. Mfumo mmoja wenye taarifa kede kede za wananchi kupitia unique National Identity ili kuboresha security.
Haya na ww ndugu Yangu una maoni gani kuhusiana na Uzinduzi wa Mchakato wa Maandilizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050?🤔🤷
Asante.
Dira ya 1 ya Maendeleo ya Taifa ni ya Mchakato wa mwaka 1969 ambayo ilitoa tathmini ya Maendeleo kuanzia Mwaka 2000-2025. Takribani miaka 22 Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa ikitekekeza dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025. Tume ya uratibu, uhariri, uandishi, uchambuzi na usambazaji wa Dira hiyo ya Maendeleo 2025 iliyoongozwa na Mwenyekiti Dr. Donas Kibogora.
Mipango ya Dira ya 2025.
Mipango hii ilitazamiwa kufikisha Taifa Uchumi wa kipato Cha kati 2025. Mipango hiyo ilikuwa kama ifuatavyo;
1. Maisha bora na mazuri
2. Amani, utulivu na umoja
3. Utawala na uongozi bora
4. Jamii iliyoelimika na inayopenda kujifunza zaidi
5. Uchumi shindani na imara.
Mafanikio ya Dira ya 2025
1. Serikali ya Tanzania kuingia uchumi wa Kati hadhi ya chini na hali ya umasikini umepungua kutoka 35.7% mwaka 2001 mpaka kufikia 24.6% mwaka 2017/2018. Hapa kipato Cha mtu mmoja mmoja kimeongezeka kutoka Us$1036 mpaka Us$4045 Mwaka 2020.
2. Wastani wa kuishi umeongezeka kutoka miaka 51 mwaka 2000 mpaka kufikia miaka 67 mwaka 2022.
3. Vifo vya kinamama vimepungua kutoka 854 kwa vizazi 100,000 na vifo 99 kwa vizazi 1,000 Mwaka 2000 hadi vifo 524 kwa vizazi 100,000 na vifo 36 kwa vizazi 1000 Mwaka 2020.
4. Kiwango Cha udahili wa wanafunzi wa shule ya msingi kimeongezeka kutoka 58.8% Mwaka 2000 mpaka kufikia 95.7% Mwaka 2020.
5. Upatikanaji wa Maji safi umeongezeka kutoka 50% Mwaka 2000 hadi 86.7% mwaka 2020 kwa mijini na 55% kwa Mwaka 2000 hadi 72.3% Mwaka 2020 kwa vijijini.
6. Upatikanaji wa nishati ya umeme umeongezeka na kufikia 59.8% kwa Mwaka 2020.
Changamoto ya Dira ya Maendeleo 2000/2025
1. Kudorora kwa Uchumi wa Dunia mwaka 2007-2008.
2. Ugonjwa wa uviko 19 Mwaka 2020/2021 na Uchumi ulipungua kutoka 7% Mwaka 2019 mpaka kufikia 4.8% Mwaka 2020.
3. Mabadiliko makubwa ya Tabia ya Nchi.
4. Vita vya Urusi na Ukraine.
Chimbuko la Maandilizi ya Dira la 2050.
1. Kuelekea ukomo wa utekelezaji wa dira ya 2025.
2. Kuendeleza mafanikio yaliyofikiwa Kutokana na utekelezaji wa Dira 2025.
3. Uhitaji wa mkakati na mabadiliko ya teknolojia yanayoendelea kuibuka Ulimwenguni kama Blue economy, matumizi ya roboti, Biashara ya hewa ukaa na Blockchain technology.
4. Uhitaji wa mikakati utakaoainisha Agenda ya Maendeleo ya Nchi na mikakati mingine ya Umoja wa Mataifa, AU, EAC na SADDC etc.
Maandilizi ya Dira 2050 yatajumuisha hatua kuu tatu nazo ni:
1. Maandilizi ya Awali na mapitio
2. Usanifu, uchambuzi na uandishi wa Dira.
3. Uidhinishaji, Uzinduzi na usambazaji wa Dira.
- Timu ya uandishi ina wajumbe 17.
- Timu ya uhariri ina wajumbe 14.
- Kamati ya Maandilizi ya Dira ina wajumbe 39 kutoka wizara za Serikali, Taasisi Binafsi na taasisi za kitafiti. Timu zote hizi zipo chini na kuratubiwa na wizara ya Fedha na mipango.
1. Uwezo wa kutumia teknolojia mpya kama vile AI, Blockchain, Machine learning, loT na Fintech hasa kwny mifumo ya elimu yetu.
2. Watanzania wenyewe wawe waendeshaji wa ubunifu na utekelezaji wa mifumo bora ya Serikali Mtandao.
3. Uzalishaji wa vifaa vya kielectronics kwa kuwa Tanzania tuko na utajili wa madini ya kimkakati (critical minerals).
4. Matumizi ya nishati mbadala ili kulinda Mazingira yetu adhimu ya asili ya uoto.
5. Mfumo mmoja wenye taarifa kede kede za wananchi kupitia unique National Identity ili kuboresha security.
Haya na ww ndugu Yangu una maoni gani kuhusiana na Uzinduzi wa Mchakato wa Maandilizi ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050?🤔🤷
Asante.