Uzinduzi wa kampeni za uchaguzi Arumeru (CHADEMA)

yaani ni kwamba mgombea wa ccm katoga sikio, so wanasema ni muhuni hafai kuwa mbunge wa watu wastarabu kama wameru so wasimchague.

mm ni cdm damu lakini naamini uongozi mzuri hauusiani na sikio lililotogwa! Mbona sugu katoga na bado ni kiongozi mzuri sana!! Mbona mtiro naye katoga na ni balozi wa tz nchi za nje!!!!
 
..nimeanza kusikiliza wakati wa hotuba ya Mbowe.

..samahani lakini naona kama ilikuwa imekosa maandalizi.

..halafu hotuba yake sikuipenda na zaidi ilinichosha.

..binafsi sipendi kusikia MUNGU akitajwa, tena mara nyingi, katika mikutano ya kisiasa.

..zaidi, ingependaza kama Joshua Nassari, mgombea ubunge, angepewa muda mrefu zaidi kuzungumza.

..hata Nassari naye hotuba yake ilikuwa ya kulipua-lipua tu.

..hili ilikuwa ni nafasi ya kipekee kwa Nassari kuwapa wananchi wa Arumeru sababu za kwenda kumpigia kura.

..sote tujiulize, wananchi waliohudhuria mkutano ule wameondoka na kitu gani cha kuwahasisha na kuwasimulia wenzao waliokosa kuhudhuria mkutano ule kiasi kwamba siku ya uchaguzi wataacha shughuli zao na kwenda kumpa kura Joshua Nassari?

NB:

..the +ve thing ni kwamba muda wa kujirekebisha bado upo.

Huo ni uzinduzi mzee! we subiri sera za chadema utazisikia sana.... na umakini wao hauna shaka kabisa!!

Sasa linganisha uwezo wa kujieleza wa mwenyekiti wa chadema na wa CCM utacheka eti huyu ndite bora miongoni mwa CCM!

Pia usubiri umakini wa CCM ujionee vichekesho ...!! ni matakataka tu... mara hadija kopa arembuee, mara ze komedi na upuuzi mwingine.

Mwisho kabisa umenishangaza sana mkuu!!!!!!!!! yaani hupendi watu wamtaje Mungu kwenye mikutano ya siasa!
Nyerere alimtaja Mungu mara nyingi tu kwenye majukwaa ya kisiasa, Mandela na wengine wengi tu....ila Mbowe hutaki! Ulitaka amtaje shetani!? CCM bwana.
 
mm ni cdm damu lakini naamini uongozi mzuri hauusiani na sikio lililotogwa! Mbona sugu katoga na bado ni kiongozi mzuri sana!! Mbona mtiro naye katoga na ni balozi wa tz nchi za nje!!!!

Bigi usijali hivyo ni vijikolombwezo tu vya ulingo kama bondia kuna muda anapiga tu- ngumi fulani tumboni kwa mpizani wake hatuongezi pointi , ila tunamchosha mpinzani kwa namna fulani.
 
Nimepitia thread yote sijaona mahali imeripotiwa kuwa kny huo mkutano kulikuwa na kiburudisho kama kwaya, taarabu, komedi au ugawaji wa chakula na t-shirt.
Naomba kujulishwa kiburudisho gani kilikuwepo?
 
naamini kwenye uzinduzi ndio hutolewa brief ya vipaumbele vya kampeni lakini kwa kina.hii kitu imekosekana katika hotuba ya viongozi wakuu hasa mbowe na hasa hasa nasari ambaye ndio kama mwali.
 
nasari alitakiwa aseme kwa uwazi matatizo na changamoto zilizopo katika maeneo mbali mbali ya jimbo mfano tatizo la maji,barabara,shule na ardhi.lakini ametumia muda muhimu kuwatambulisha wazazi kitu ambacho hakikuwa na ulazima wowote.kumbuka ule mkutano umerushwa live nchi nzima.
 
nasari alitakiwa aseme kwa uwazi matatizo na changamoto zilizopo katika maeneo mbali mbali ya jimbo mfano tatizo la maji,barabara,shule na ardhi.lakini ametumia muda muhimu kuwatambulisha wazazi kitu ambacho hakikuwa na ulazima wowote.kumbuka ule mkutano umerushwa live nchi nzima.
Mkuu, mbona hayo matatizo aliyazungumza, lnaonesha hukufuatilia hadi mwisho au umesahau. Kazungumzia matatizo ya ardhi, afya, ajira, maji licha ya kuwepo kwa chemchem toka mlima Meru na kero za Mgambo
 
Kuhusu Update mkuu usiongope hii ndiyo Arusha mtapata kila kitu bila chenga....

mjomba wapi ile kanda au hotuba ya ufunguzi uliatuaidi kuwa utatuwekea kwenye youtube au basi tuwekee hata audio tuko tayari kusikiliza nakutakia kila la heri tunasubiri kwa hamu.
 
Back
Top Bottom