Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 37,136
- 55,605
KIJIWE CHA KAHAWA
Siku moja nilienda kutembelea kijiwe kimoja cha kahawa, huko mkoani Kilimanjaro bara bara ya kuelekea mlima kilimanjaro.
Kulikuwa na wazee na vijana wengi wakipata kahawa, huku wakileta stori za hapa na pale, ili mradi kuchangamsha kijiwe, huku tukisikiliza BBC matukio ya dunia. Na kutokana na hali ya hewa, kijiwe kilichangamka.
Mzee mmoja, akasema wajukuu zangu, ‘’nawausia sana, msiwe na tamaa ya pesa, mnaliona lile jengo kubwa pale karibu na mjini, lina historia ndefu.
Waliolijenga hilo jengo ambao ni wamiliki walishatangulia mbele za haki, walikuwa vijana wawili, walienda machimboni na walikuwa marafiki kweli kweli, na wote walikuwa wanatoka kijiji kimoja.
Baada ya kufika huko machimboni, walifanikiwa kupata jiwe lenye thamani kubwa; na baada ya kuliuza walipata hela nyingi, wakaamua kulijenga hilo jengo ili liwe hotel.
Wakalisimamisha hilo jengo kwa haraka sana, pamoja na kuweka mazingira ya nje kwa ajili ya kuvutia wateja.
Kwa bahati mbaya, mmoja kati ya wale wamiliki akaingiwa na roho ya ubinafsi, tamaa, na kutaka kumzidi kete mwenzie. Akamfanyia mwenzie mambo ya ajabu ajabu mpaka umauti ukamfika huko machimboni.
Kwa sababu yule kijana ndio aliyebaki, na ndiye anapafahamu kwa mwenzie ambaye ni marehemu, alitoa taarifa kwao, na akafanya utaratibu wa kusafirisha mwili kwa ajili kuweka msiba. Taratibu za mazishi zikapangwa, na akazikwa.
Lakini wazazi wa yule marehemu wakawa wana maswali mengi kuhusu kifo cha mtoto wao; ndipo wakatoa tamko, tunafanya tambiko kwa yeyote aliyehusika kwa kifo cha mtoto wetu, naye adhurike; wakafanya machinjo ya mifugo pamoja na mila zao.
Haikuchukua wiki, yule kijana akaanza kuvimba tumbo; na hatimaye akaenda kukiri ndiye aliyemsababishia umauti mwenzie, na baada ya hapo naye alifariki.
Ikawa wote wamiliki wa lile jengo wamefariki, na hakuna mmiliki mwingine aliyebaki; lile jengo likawa limetelekezwa kwa miaka mingi, na kwa sababu liko sehemu nzuri kibiashara likawa linawavutia wengi, lakini hawajui waanzie wapi kuja kulipata.
Baadaye kukawa na habari za chini chini mara limetaifishwa n.k’’
Cha kujifunza hapa, 'partnership' kwa sisi waafrika bado, mtaanza vizuri, lakini baadaye mafanikio yakionekana kuna kugeukana, kila mmoja atataka awe boss kwa mwenzie.
Leteni stori za vijiweni wakuu, tupate kujifunza
Siku moja nilienda kutembelea kijiwe kimoja cha kahawa, huko mkoani Kilimanjaro bara bara ya kuelekea mlima kilimanjaro.
Kulikuwa na wazee na vijana wengi wakipata kahawa, huku wakileta stori za hapa na pale, ili mradi kuchangamsha kijiwe, huku tukisikiliza BBC matukio ya dunia. Na kutokana na hali ya hewa, kijiwe kilichangamka.
Mzee mmoja, akasema wajukuu zangu, ‘’nawausia sana, msiwe na tamaa ya pesa, mnaliona lile jengo kubwa pale karibu na mjini, lina historia ndefu.
Waliolijenga hilo jengo ambao ni wamiliki walishatangulia mbele za haki, walikuwa vijana wawili, walienda machimboni na walikuwa marafiki kweli kweli, na wote walikuwa wanatoka kijiji kimoja.
Baada ya kufika huko machimboni, walifanikiwa kupata jiwe lenye thamani kubwa; na baada ya kuliuza walipata hela nyingi, wakaamua kulijenga hilo jengo ili liwe hotel.
Wakalisimamisha hilo jengo kwa haraka sana, pamoja na kuweka mazingira ya nje kwa ajili ya kuvutia wateja.
Kwa bahati mbaya, mmoja kati ya wale wamiliki akaingiwa na roho ya ubinafsi, tamaa, na kutaka kumzidi kete mwenzie. Akamfanyia mwenzie mambo ya ajabu ajabu mpaka umauti ukamfika huko machimboni.
Kwa sababu yule kijana ndio aliyebaki, na ndiye anapafahamu kwa mwenzie ambaye ni marehemu, alitoa taarifa kwao, na akafanya utaratibu wa kusafirisha mwili kwa ajili kuweka msiba. Taratibu za mazishi zikapangwa, na akazikwa.
Lakini wazazi wa yule marehemu wakawa wana maswali mengi kuhusu kifo cha mtoto wao; ndipo wakatoa tamko, tunafanya tambiko kwa yeyote aliyehusika kwa kifo cha mtoto wetu, naye adhurike; wakafanya machinjo ya mifugo pamoja na mila zao.
Haikuchukua wiki, yule kijana akaanza kuvimba tumbo; na hatimaye akaenda kukiri ndiye aliyemsababishia umauti mwenzie, na baada ya hapo naye alifariki.
Ikawa wote wamiliki wa lile jengo wamefariki, na hakuna mmiliki mwingine aliyebaki; lile jengo likawa limetelekezwa kwa miaka mingi, na kwa sababu liko sehemu nzuri kibiashara likawa linawavutia wengi, lakini hawajui waanzie wapi kuja kulipata.
Baadaye kukawa na habari za chini chini mara limetaifishwa n.k’’
Cha kujifunza hapa, 'partnership' kwa sisi waafrika bado, mtaanza vizuri, lakini baadaye mafanikio yakionekana kuna kugeukana, kila mmoja atataka awe boss kwa mwenzie.
Leteni stori za vijiweni wakuu, tupate kujifunza