Uzi Maalum Kwa Ajili ya Maonesho ya Kimataifa ya Biashara - Sabasaba 2019

kisokolokwinyo20

JF-Expert Member
Apr 15, 2019
472
422
Habari Wakuu,

Ni kipindi kingine tena cha mwaka ambapo kama ilivyo ada kunakuwa na Maonesho ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba.

Kupitia maonesho haya, wafanyabiashara na watoa huduma mbalimbali kwa jamii hupata nafasi ya kujinadi kwa shughuli mbalimbali wanazozifanya.

Ni ukweli usiopingika kuwa maonesho haya yana tija sana katika kuinua uchumi wa nchi kupitia biashara zinazofanyika hasa bidhaa za viwandani. Lakini pia kwa watoa Huduma wengine hunufaika kwa kupata mirejesho mingi kutoka kwa wapokea huduma zao.

Kwa mwaka huu wa 2019, maonesho haya yameanza vizuri ikiwa ni pamoja na wanaomiliki majengo/mabanda kukamilisha maandalizi yao mapema na wachache ambao wanamalizia matayarisho kwa hatua za mwisho.

Leo ikiwa ni siku ya kwanza tayari kumechangamka na kumependeza.

Karibuni wananchi wenzangu tujionee na kuwaunga mkono wajasiriamali wadogo, wakubwa na wote wanaojihusisha na kujitangaza katika viwanja hivi.

Nawasilisha.
 
Habari Wakuu,

Ni kipindi kingine tena cha mwaka ambapo kama ilivyo ada kunakuwa na Maonesho ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba.

Kupitia maonesho haya, wafanyabiashara na watoa huduma mbalimbali kwa jamii hupata nafasi ya kujinadi kwa shughuli mbalimbali wanazozifanya.

Ni ukweli usiopingika kuwa maonesho haya yana tija sana katika kuinua uchumi wa nchi kupitia biashara zinazofanyika hasa bidhaa za viwandani. Lakini pia kwa watoa Huduma wengine hunufaika kwa kupata mirejesho mingi kutoka kwa wapokea huduma zao.

Kwa mwaka huu wa 2019, maonesho haya yameanza vizuri ikiwa ni pamoja na wanaomiliki majengo/mabanda kukamilisha maandalizi yao mapema na wachache ambao wanamalizia matayarisho kwa hatua za mwisho.

Leo ikiwa ni siku ya kwanza tayari kumechangamka na kumependeza.

Karibuni wananchi wenzangu tujionee na kuwaunga mkono wajasiriamali wadogo, wakubwa na wote wanaojihusisha na kujitangaza katika viwanja hivi.

Nawasilisha.
Siku ya korosho ni lini?
 
Haya tutajuzana kwapicha bidhaa nzuri zenye bei za ofa ya saba saba mana wengine tupo madongo kuinama
 
Bado wanafunga saa 12 jioni au pako wazi usiku?

Nilikuja miaka michache iliyopita, nikakuta sehemu nyingi wanafunga saa 12 jioni wakiogopa wezi.
 
Nini Cha kununua chenye manufaa ya baadae na hakipatikani kirahisi Tanzania?
 
Back
Top Bottom