Uzee una tabu jamani, sikieni tu!

NIMEONA

JF-Expert Member
Aug 4, 2019
3,866
5,679
nimeumizwa mno kumshuhudia mzee mmoja akiachwa na magari mawili yaliyokuwa katika haraka zao za kukimbilia abiria vituo vya mbele.

'achana nae atatuchelewesha huyo'!
'unaweza kuta ametoroka tu kwao bila kuaga wanakuja kutuhangaisha sisi huku'! hayo ndo yalikuwa maneno yao.

kilichoniuma zaidi ni kuwa mzee namfahamu, ni mzima kabisa kiakili ingawa mwili hauko bara bara kutokana na uzee....huwa anatembea kwa shida kidogo! safari yake hii alikuwa anaelekea kwa mtoto wake kupata msaada wa matibabu. viti kibao vya magari vilikuwa vitupu kabisa.....walimwacha mzee wa watu kinywa wazi ameshangaa huku wao wakiendelea na safari yao kwa vicheko.

tuwatunze na kuwaheshimu wazee wetu jamani, tunaelekea huko huko kwa kasi ya ajabu kabisa! tunaweza kujikuta tunalipwa, uzeeni kwetu, haya haya tuwatendeayo sasa hivi!!
 
Mbali na kufungua sredi hii wewe ulichukua jukumu gani kumsaidia huyo mzee, hasa ukizingatia kuwa unamfahamu na unajua alikokuwa anakwenda?
nilikuwa ndani ya moja ya gari hiyo, sikuweza kufanya chochote ingawa nilitamani nimsogeze mbele kidogo kwenye kituo chenye abiria wengi kiasi ili aingie nao
 
Wewe nawe una makosa. Baada ya kugundua anapokwenda alafu ukamwacha pasipo kumsaidia ulifanya makosa
hakukuwa na nafasi ya kufanya hivyo mkuu; konda na dereva wasingeweza kunisikiliza kamwe....ningeambulia matusi tu, huko nilikokuwa naenda nako kulikuwa na majanga yake na nilikuwa nyuma ya muda tayari.....ingekuwa changamoto kubwa kushuka!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
nimeumizwa mno kumshuhudia mzee mmoja akiachwa na magari mawili yaliyokuwa katika haraka zao za kukimbilia abiria vituo vya mbele.

'achana nae atatuchelewesha huyo'!
'unaweza kuta ametoroka tu kwao bila kuaga wanakuja kutuhangaisha sisi huku'! hayo ndo yalikuwa maneno yao.

kilichoniuma zaidi ni kuwa mzee namfahamu, ni mzima kabisa kiakili ingawa mwili hauko bara bara kutokana na uzee....huwa anatembea kwa shida kidogo! safari yake hii alikuwa anaelekea kwa mtoto wake kupata msaada wa matibabu. viti kibao vya magari vilikuwa vitupu kabisa.....walimwacha mzee wa watu kinywa wazi ameshangaa huku wao wakiendelea na safari yao kwa vicheko.

tuwatunze na kuwaheshimu wazee wetu jamani, tunaelekea huko huko kwa kasi ya ajabu kabisa! tunaweza kujikuta tunalipwa, uzeeni kwetu, haya haya tuwatendeayo sasa hivi!!
kwahiyo kuna uwezekano kua na yeye hapoa alikua analipwa kutokana na aliyoyafanya wakati yupo kijana!?..

natafakari tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom