Uzazi kwa njia ya upasuaji

Mwana CCM.

Member
Jan 4, 2011
83
10
Mimi na mke wangu katika suala la uzazi tulipanga kama Mungu akitujaalia tuwe na watoto wawili tu. Na miezi mitatu iliyopita tulijaariwa kupata mtoto wetu wa kwanza kwa njia ya operation hii ilitokana na njia kutokufunguka kwa wakati. Sasa tunaambiwa mtu akijifungua mtoto wa kwanza kwa operation hata wanaofuatia watapatikana kwa njia hiyohiyo hasa ukizingatia mke wangu ana umri wa miaka 33 sasa. Sasa tupo kwenye wakati mgumu wa kuamua kama tuongeze mtoto mwingine au la! na woga wetu unajikita katika uvumi unaosema mwanamke akijifungua kwa njia ya upasuaji kwa zaidi ya mara moja ni hatari sana. Naomba ushauri kama tupange kuongeza mtoto au lah?
 
Sijui kajifungua katika Hospitali gani na amefanyiwa hiyo operation na akina nani. Mke wangu kajifungua kwa operation mara mbili thr Specialists Muhimbili(MNH) Fast Track, hana matatizo yoyote, Kwa maelezo yao kuzaa kwa operation ni salama zaidi kuliko uzazi wa kawaida. Nakushauri nenda kawaone kwa mfano Dr. Kamugisha pale MNH nimemkubali.
 
Si lazima kwa operation uzazi wa pili, japo inashauriwa hivo kutegemea na sababu ya operationya 1. Na kwa kuwa njia haikufunguka nadhani watalam wangeshauri kisu next child birth.
Nimeona kina mama wamejifungua kwa kisu hadi mara 3,4. japo wanadai kizazi kinachoka kila baada uzazi and ukizingatia umri wa huyo mama mwili madrs wanadai matatizo yanaongezeka with umri.
Cha muhimu nenda kwa dr wa kinamama atakupa options,
Dont worry too much broda bado waweza ongeza population.
 
Mkuu Mwana CCM ( japokuwa ni mpinzani wangu) si kweli kwamba mama akijifungua kwa 'operation' mzao wa kwanza, basi uzao wote unaofuatia atajifungua kwa 'operation' tuu. Hii inategemea na sababu ya kufanyiwa operation ya kwanza. Kuna sababu zinazojirudia mfano maumbile (ufupi, nyonga ndogo, ulemavu n.k) hizi ni lazima itakuwa operation tuu kwa kila uzao. Lakini kuna sababu zisizojirudia mfano njia kutofunguka, mtoto mkubwa, mtoto kukaa vibaya, mtoto kuchoka n.k, kwa hizi mama anaweza kujifungua kawaida tu mzao unaofuatia ila inabidi awe kwenye unagalizi mkubwa wa daktari kwani lile kovu lililo katika mfuko wa uzazi (uterus) linaweza chanika wakati wa uchungu.

Nimeshaona mara nyingi tu kina mama waliojifungua kwa operation katika uzao wa kwanza kujifungua uzao unaofuatia kawaida tu bila tatizo lolote.

Kutokana na uwezo wa kovu katika mfuko wa uzazi kuhimili uchungu kupungua kila idadi ya operation inapoongezeka...kitaalamu inashauriwa kuwa mama anayejifungua kwa operation basi zisizidi 3, kwani baada ya hapo unaongeza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa mfuko kupasuka wakati wa uchungu na kuhatarisha maisha ya mama na mtoto.
 
Sijui kajifungua katika Hospitali gani na amefanyiwa hiyo operation na akina nani. Mke wangu kajifungua kwa operation mara mbili thr Specialists Muhimbili(MNH) Fast Track, hana matatizo yoyote, Kwa maelezo yao kuzaa kwa operation ni salama zaidi kuliko uzazi wa kawaida. Nakushauri nenda kawaone kwa mfano Dr. Kamugisha pale MNH nimemkubali.

Wakuu nimewapata sana, alijifungua TMJ hosptal
 
Nimesikia tuhuma kwamba baadhi ya hospitali za binafsi hupendelea operation zaidi kwa vile zina tija zaidi kwao. Sijui ni kweli?
 
Pia unatakiwa ujipe muda wa miaka mitatu au minne kabla ya kuongeza mtoto mwingine. Hii ni kwa ajili ya kulinda afya na usalama wa mama. Kujifungua mara ya pili bila operation inawezekana, lakini tahadhari ni kwamba kunakuwa na 50-50 probability ya kushindikana na kufanikiwa. Inaposhindikana inakuwa hatari sana, na mfuko wa uzazi unaweza kupasuka na kuhatarisha maisha ya mama na mtoto. Ili Kuondokana na hiyo risk ya kushindikana, mara nyingi inashauriwa kufanya tena operation.
 
Mimi si mtaalam sana ila kwa macho yangu nimeshuhudia familia mbili ambazo mama amezaa watoto watatu kwa operation, sasa sijui kama hiyo hatari huwa inachagua... Ila cha msingi tu ni kupata muda wa kutosha ili kidonda na kovu lipone kabisa!!!!
 
Mama anatakiwa apate muda wa kutosha kabla hajapata ujauzito mwingine, pia previous scar ni moja ya indication ya kupitia caesarian section tena. Inategemea na sababu ya kwanza. Kwa uelewa wangu kidogo 3 ni mwisho zaidi ya hapo ni risk kwa mama na mtoto. Kwa ufafanuzi zaidi onana na wataalam wa masuala ya wanawake. All the best.
 
me cjui kitu ila nachojua mama yetu alituzaa wote kwa operation na tuko wa3, mama ana 57yrz sasa, me niliambiwagwa wa3 ndio mwisho
 
Back
Top Bottom