Uzanzibari + Utanganyika = Utanzania

aleesha

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
775
1,117
Hapana asiejua kwamba Zanzibar inatawaliwa na kuburuzwa na Tanganyika. Kwa miaka sitini yote ya muungano, ndio kwanza Rais aliepo madarakani hivi sasa ndio mzaliwa wa Zanzibar, lakini waliomzunguka ndio walewale, wao ni wengi mmno. Wameshaota mizizi minene ndani ya CCM na serikali zake, anapotumia nguvu zake wao hutumia wingi wao na hujuma zao dhidi yake.

Wapo wenye chuki na uadui kwanini mzanzibari awe Rais wa Tanzania?! Chuki na uadui huu umo ndani na nje ya CCM! Wanasahau kwamba Zanzibar ni nchi kamili iliyoungana tu na Tanganyika ikapatikana Tanzania! Tokea mwanzo wa muungano, hapana mzanzibari aliewahi kuwa kiongozi mkuu wa taasisi kuu yoyote ya muungano, sio Mkuu wa Jeshi, wala Mkuu wa Polisi, wala Mkuu wa Uhamiaji, na wala usiseme hizo taasisi nyengine.

Sisi wazanzibari kipaumbele chetu sio muungano wala utanzania, kwa sababu tunajua wazi kwamba hizi ni njama tu na mbinu za kuumaliza zuanzibari. Sisi wazanzibari kipaumbele chetu ni Zanzibar yenye mamlaka kamili.

Hapana asiejua kwamba CCM Tanganyika ni waanzilishi na ni wasimamizi wa dhulma na ukandamizaji kwa wazanzibari. Na kinachosikitisha ni kuwaona CCM Zanzibar wameridhia hayo kwa sababu tu ya maslahi yao binafsi wanayoyapata ndani yake.

Wazanzibari kuishi Tanganyika sio lazima pawepo na muungano, na watanganyika wanaoishi Zanzibar pia sio lazima pawepo na uumngano. Watanganyika wapo kila nchi duniani wanaishi vizuri tu na wala hapana muungano baina ya Tanganyika na nchi hizo, na kwa wazanzibari ndio hivyohivyo. Kilicho bora zaidi na ni faida kwa pande zote mbili ni kuwa na muungano ambao hauna upendeleo wala malalamiko.

Hata hivyo, mimi siungi mkono na wala sipendi kuona chuki na ugomvi baina ya watanganyika na wazanzibari. Mwenyezi Mungu atunusuru tusije tukaja kupigana na kuuwana. Kuepusha hayo, ipo haja ya kuoneshana ubinaadamu na kuwekeana heshima za mila na tamaduni za pale ulipo. Hapana haja ya kudhalilishana wala kudogoana. Lakini tatizo ni mifumo ya kisiasa ya CCM na serikali zake, au labda niseme kuwa wanasiasa wengi wa Tanganyika hawana nia njema na Zanzibar.

Ismail Jussa
21/08/2022
Makunduchi Unguja
 
Nyinyi Wazanzibari kama vipi jitengeni tu. Kiukweli Watanganyika tulio wengi hata hatuoni umuhimu wenu kwenye Muungano. Na siamini kama kuna Mtanganyika anaye ulilia huu Muungano, ukiondoa ccm ambao wananufaika kisiasa.

Kila siku ni kulalamika tu na kunung'unika!
Yaani ni watu msiotosheka, wala kuridhika kwa chochote! Muda wote ni kulia lia tu!
I hope itatokea siku mtaishi kivyenu, na sisi tutaishi kivyetu.

God bless Tanganyika.
 
Na huko nasikia Mwinyi anauza vijivisiwa10 kwa waarabu sijui mtakimbilia wapi mkirudi wote zenji kakisiwa kanazama
 
Mbona hata mbeya inaburuzwa na muungano?? Miaka 60 ya uhuru hatujapata raisi kutokea mbeya au Iringa au Arusha
 
Muungano ulikuwa na umuhimu kwenye miaka ya 60 sio sasa

Ni muda wa tanganyika kuvunja huu udanganyifu hawa wapemba waliyokwapua ardhi yetu kwa mahekari warudi kwao
 
Mbona hata mbeya inaburuzwa na muungano?? Miaka 60 ya uhuru hatujapata raisi kutokea mbeya au Iringa au Arusha
umeongea ukweli mtupu, Mbeya inaburuzwa tu na muungano wa CCM, sioni jitihada za serikali za maendeleo kwa wananchi wa Mbeya.kama wameshindwa wawaache wana Mbeya wajiongoze tu.
 
Hakuna muungano kuna uvamizi wa majeshi ya Tanganyika yaliyopelekwa na Nyerere Zanzibar.
 
Nyinyi Wazanzibari kama vipi jitengeni tu. Kiukweli Watanganyika tulio wengi hata hatuoni umuhimu wenu kwenye Muungano. Na siamini kama kuna Mtanganyika anaye ulilia huu Muungano, ukiondoa ccm ambao wananufaika kisiasa.

Kila siku ni kulalamika tu na kunung'unika!
Yaani ni watu msiotosheka, wala kuridhika kwa chochote! Muda wote ni kulia lia tu!
I hope itatokea siku mtaishi kivyenu, na sisi tutaishi kivyetu.

God bless Tanganyika.
Pia Jussa kumbuka haya
Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi znz,

Ajira za serikali Znz ni za Wazanzibr pekee,

Mtanganyika hawezi kugombea nafasi yoyote ya kisiasa Znz, hata ujumbe wa mtaa, (sheha)

Ukitaka kwenda Znz lazima uwe na kitambulisho, lkn mpemba au muunguja anaweza kwenda popote Tanganyika na kumiliki ardhi na biashara yoyote bila tatizo,
Mzanzibar anaweza kuwa Rais wa JMT, lakini Mtanganyika hawezi kuwa Rais wa Zanzibar, hapa namaanisha mwenye jina kama Mapunda, John, au Mwakyoma,

Rai yangu ni muungano uboreshwe kuondoa maunguniko kama haya ya kina Jussa Ismail,
 
Pia Jussa kumbuka haya
Mtanganyika hawezi kumiliki ardhi znz,

Ajira za serikali Znz ni za Wazanzibr pekee,

Mtanganyika hawezi kugombea nafasi yoyote ya kisiasa Znz, hata ujumbe wa mtaa, (sheha)

Ukitaka kwenda Znz lazima uwe na kitambulisho, lkn mpemba au muunguja anaweza kwenda popote Tanganyika na kumiliki ardhi na biashara yoyote bila tatizo,
Mzanzibar anaweza kuwa Rais wa JMT, lakini Mtanganyika hawezi kuwa Rais wa Zanzibar, hapa namaanisha mwenye jina kama Mapunda, John, au Mwakyoma,

Rai yangu ni muungano uboreshwe kuondoa maunguniko kama haya ya kina Jussa Ismail,
Jamaa chakwao chakwao juzi kati nilikuwa moro ndani ndani huko kwenye mashamba ya mpunga wamejazana kibao wananunua matani na matani ya mchele wala hamna anae wagasi sasa nenda kwao uone.
 
Hapana asiejua kwamba Zanzibar inatawaliwa na inabururwa na Tanganyika. Kwa miaka sitiini yote ya Muungano...
Mpuuzi huyu Jussa, wanasiasa wa Tanganyika wangekuwa hawana nia njema na Zanzibar wasingewaruhusu kwa moyo mmoja waingie ndani ya ukumbi wa bunge la Dodoma na wakawa na uhuru wa kutoa maamuzi kama walionao sasa.
 
Hapana asiejua kwamba Zanzibar inatawaliwa na inabururwa na Tanganyika. Kwa miaka sitiini yote ya Muungano, ndio kwanza Rais aliepo madarakani hivi sasa ndio mzaliwa wa Zanzibar, lakini waliomzunguka ndio walewale, wao ni wengi mmno, wameshaota mizizi minene ndani ya CCM na Serikali zake, anapotumia nguvu zake wao hutumia wingi wao na hujuma zao dhidi yake.

Wapo wenye chuki na uadui kwanini Mzanzibari awe Rais wa Tanzania! Chuki na uadui huu umo ndani na nje ya CCM! Wanasahau kwamba Zanzibar ni nchi kamili iliyoungana tu na Tanganyika ikapatikana Tanzania! Tokea Mwanzo wa Muungano, hapana Mzanzibari aliewahi kuwa kiongozi Mkuu wa Taasisi kuu yoyote ya Muungano, sio Mkuu wa Jeshi, wala Mkuu wa Polisi, wala Mkuu wa Uhamiaji, na wala usiseme hizo taasisi nyengine.

Sisi Wazanzibari kipa umbele chetu sio Muungano wala Utanzania, kwa sababu tunajua wazu kwamba hizi ni njama tu na mbinu za kuumaliza Uzanzibari. Sisi Wazanzibari kipa umbele chetu ni Zanzibar yenye mamlaka kamili. Hapana asiejua kwamba CCM Tanganyika ni waanzilishi na ni wasimamizi dhulma na ukandamizaji kwa Wazanzibari. Na kinachosikitisha ni kuwaona CCM Zanzibar wameridhia hayo kwa sababu tu ya maslahi yao binafsi wanayoyapata ndani yake.

Wazanzibari kuishi Tanganyika sio lazima pawepo na Muungano, na Watanganyika wanaoishi Zanzibar pia sio lazima pawepo na Muungano. Watanganyika wapo kila nchi duniani wanaishi vizuri tu na wala hapana Muungano baina ya Tanganyika na nchi hizo, na kwa Wazanzibari ndio hivyohivyo. Kilicho bora zaidi na ni faida kwa pande zote mbili ni kuwa na Muungano ambao hauna upendeleo wala malalamiko.

Hata hivyo, mimi siungi mkono na wala sipendi kuona chuki na ugomvi baina ya Watanganyika na Wazanzibari. Mwenyezi Mungu atunusuru tusije tukaja kupigana na kuuwana. Kuepusha hayo, ipo haja ya kuoneshana ubinaadamu na kuwekeana heshima za mila na tamaduni za pale ulipo. Hapana haja ya kudhalilishana wala kudobogoana. Lakini tatizo ni mifumo ya kisiasa ya CCM na Serikali zake, au labda niseme kuwa wanasiasa wengi wa Tanganyika hawana nia njema na Zanzibar.

Ismail Jussa
21/08/2022
Makunduchi Unguja
Hivi nyie mna matatizo ya akili??itakuwa mna matatizo ya akili sio bure.Hivi zanzibar si mna serikali yenu,rais wenu,bunge lenu,baraza la mawaziri lenu na nchi yenu??Sasa mnatutaka nini watanganyia au mnataka mtunyonye damu??Yaani nynyi mna roho za kutolizika ndo maana kila siku kulalamika.Wazanzibar ni marais Tanganyika tuchukulia poa,wazanzibar ni mawaziri Tanganyika hata kwa mambo yasiyokuwa ya muungano(Waziri Mbarawa) tumechukulia poa,tunakulaga wote madini ya tanganyika miaka yote mmepata mafuta zanzibar mmekimbia mbio kama wehu ili mule wenyewe ambacho ni ujinga tu.Sasa tumewachoka tunakoelekea mbwai itakuwa mbwai kila mtu aishi kwakwe.
 
Jamaa chakwao chakwao juzi kati nilikuwa moro ndani ndani huko kwenye mashamba ya mpunga wamejazana kibao wananunua matani na matani ya mchele wala hamna anae wagasi sasa nenda kwao uone.
Ni walalamishi sana,
Sehemu yenye watu milioni na nusu Bunge la ina wabunge wengi kuliko Mwanza yenye watu zaidi ya milion tatu,

Na wanalipwa sawa na mbunge kawe yenye watu zaidi ya milioni,
 
Watanganyika tumekaa kimya Sana kwa muda juu ya chokochoko zenu na Sasa mnavuka redline kwanza huwa nashangaa kitu gani kinacho wafanya mjione watu special Sana enyi Wala ulojo?

Chuki zenu za wazi kwa watanganyika ni udini ulio zaa ubaguzi na mwisho mkatengeneza makundi ndani ya nchi yenu wenyewe sijui huyu mkaskazini sijui huyu mkusini ujinga tu umewajaa.

Kwanza hamchangii chochote kwenye muungano rudini kwenu.
 
Ni walalamishi sana,
Sehemu yenye watu milioni na nusu Bunge la ina wabunge wengi kuliko Mwanza yenye watu zaidi ya milion tatu,

Na wanalipwa sawa na mbunge kawe yenye watu zaidi ya milioni,

Wana haki, asilimia zaidi ya 90 zanzibar ni waislamu, sasa unategemea asiekua muislamu ajichomeke mule! Kumbuka zanzibar ina rais wake, na ni nchi na sio mkoa ama jiji.
 
Back
Top Bottom