samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Katika kile kinachoelezwa kuwa ni mkakati wa vyama vya siasa kusaka mtaji wa wanafunzi wa vyuo vikuu umoja wa wanawake wa ccm tanzania (UWccmT) jana jumapili uliandaa mkutano na wanafunzi wa kike wa vyuo vikuu vya mkoa wa dodoma uliofanyika katika ukumbi wa kilimani ili kupunguza nguvu ya chadema ambao nao walikuwa wameandaa kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani humo siku hiyo hiyo. UWccmT iliandaa magari kwa ajili ya kuwabeba wanafunzi kuelekea kilimani na baadaye kuwarudisha vyuoni. Dada mmoja kutoka udom aliyehudhuria mkutano huo anasema yeye alienda kwa ajili ya kula na kunywa na alitimiza adhma yake kama alivyokuwa amepang kwa kuwa ccm waliandaa mapochopocho kibao. Ajenda kubwa ya mkutano huo ilikuwa ni kuwasihi wanafunzi wasigome kwa kuwa wanasiasa hawatafukuzwa chuo bali ni wao ndio wataathirika. Kulikuwa pia na ajenda ya kuipasha chadema ambapo mtoa mada mmoja ambaye sikuweza kupata jina lake alimponda godbless lema na kusema ameishia kidato cha pili na kwamba alikuwa muosha magari hivyo wasomi hawapaswi kumsikiliza.(sina hakika kama kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya elimu na siasa). UWccmT waliwasihi akina dada hao wanunue kadi za ccm ambazo zinapatikana vyuoni lakin wanafunzi waliwauliza inakuwaje chadema wanagawa bure na wao wanauza, walijibiwa kuwa cha bure hakina thamani. Duru zinasema kwamba ccm waliamua kuandaa mkutano na wanafunzi wa kike kwa kuwa wao ni wepesi kushawishika ukilinganisha na wanaume. Mwezi novemba mwaka jana rais kikwete alipohudhuria mahafali ya kwanza ya chuo kikuu cha dodoma aliwataka wanafunzi.wasikubali kutumiwa na wanasiasa. Mkoa wa dodoma una vyuo vikuu 4 udom, st. John, mipango na cbe..