Uwepo Mdahalo wa Wagombea Arumeru

Sasaa nasari utampambanisha na sioi kweli?kama baba ake sioi mwenyewe alikua ana hemeshwa itakua mwanae?magamba wameshindwa tu kukubari wameona aibu kua kama cuf kiufupi wana sindikiza 2 hapo nikama baka na azam
 
C.c.m uwa hawataki kusikia mambo ya midahalo,hamkumbuki 2010 walikataa kabisa hayo mambo kuanzia ngazi ya urais mpaka diwani!na ndio yaliyosababisha Tido kutoongezewa mkataba tbc
 
Wanaohusika na midahalo kazi kwenu.

Mimi ningeshauri hoja hii ichukuliwe na Pascal Mayalla = Pasco = Pasco (wa JF) kwa kuanzia tu (kuhusu ile hoja yake ya kuchukua michango ya hapa JF kuanzishia midahalo ya kwenye Televisheni), au mnaonaje wakuu ...
 
Mimi ningeshauri hoja hii ichukuliwe na Pascal Mayalla = Pasco = Pasco (wa JF) kwa kuanzia tu (kuhusu ile hoja yake ya kuchukua michango ya hapa JF kuanzishia midahalo ya kwenye Televisheni), au mnaonaje wakuu ...

kwakweli pascal ni mtu sahihi kwa hii kazi ngoja tuwasiliane nae .
 
Kama uliangalia midahalo ya 2010 iliyorushwa na tbc toka jimboni arumeru east ilishiriki na hapo ndo nilipata kumfahamu nasary kwa mara ya kwanza nafikiri ni vyema mdahalo ukawepo na najua utakuwepo kwani hata nzega ulikuwepo, wagombea tutawaona kwa hoja.
 
huyu wakimkumbusha msiba tu atalia, nape na mukama hawawezi kukubali bado wanakumbuka igunga walipo danganya ujenzi wa daraja na ahadi kibao za magufuli, hivi arumeru nako kuna njaa kama igunga?
 
Kama uliangalia midahalo ya 2010 iliyorushwa na tbc toka jimboni arumeru east ilishiriki na hapo ndo nilipata kumfahamu nasary kwa mara ya kwanza nafikiri ni vyema mdahalo ukawepo na najua utakuwepo kwani hata nzega ulikuwepo, wagombea tutawaona kwa hoja.

kweli tutajua nani anatufaa.
 
Kama jana alishindwa kujieleza kweli nasari ataweza mdahalo ? Labda tumwangalie nae sioi jumatatu .
 
Naomba vyombo vya habari watuandalie mdahalo wa wagombea Arumeru ili wananchi tuwapime vizuri uwezo wao
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Hei! CCM hawatokubali mdahalo ndugu yangu kwa sababu wanaelewa udhaifu wao! Hivi huoni Sioi hana mvuto wale haiba ya siasa? anasukumwa tu na mafisadi kwa kukidhi matakwa yao! Embu ona mtu kama mzee Mkapa anafanya mambo ya aibu na kupoteza sifa zake.
 
Wee mzee wa kutoga masikio ataongea nini...kiswahili chenyewe shidaa....ehehehe labda akasaidiwe na vuvuzela Nape
 
Sioi ataburuzwa vibaya. Jamaa hana mvuto kabisa. Ongea yake inaonesha si mwanasiasa mkomavu analazimisha
 
Chadema, kimeomba kufanyika mdahalo wa wagombea wote wa ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ili kutoa fursa kubwa kwa wapigakura wa jimbo hilo na Watanzania kwa ujumla, kuwafahamu.

Meneja Mwenza wa kampeni wa Chadema, Vincent Nyerere, alitoa ombi hilo jana katika mikutano ya kampeni ya chama hicho, katika Kijiji cha Kikatiti na Maleu, wakati mgombea ubunge wa chama hicho, Nassari akiomba kura.

Nyerere ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, alisema uchaguzi wa Jimbo la Arumeru Mashariki unasura ya kitaifa, hivyo ni busara kutoa fursa kwa Watanzania wengi kuwajua wagombea, sera zao na nini wamejipanga kuwafanyia wakazi wa jimbo hilo.

"Sisi Chadema tunataka wagombea wengine wakubali hasa CCM ambao wamekuwa wakikacha midahalo ili tutowe fursa kwa Watanzania kuwajua wagombea wao kwani kipindi cha kampeni ni kifupi sana, hivyo hakitowi nafasi wagombea kujulikana,"alisema Nyerere.

My take: Naunga mkono hoja -Mdahalo utasaidia sana wapiga kura kuwaelewa wagembea na mambo wanayoyasimamia.
 
Thubutu nani atasimama na JO, magamba wanajijua hawana say zaidi ya kutukana na kuhonga, mgombea wa ccm ataongea nini?
 
Chadema, kimeomba kufanyika mdahalo wa wagombea wote wa ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ili kutoa fursa kubwa kwa wapigakura wa jimbo hilo na Watanzania kwa ujumla, kuwafahamu.

Meneja Mwenza wa kampeni wa Chadema, Vincent Nyerere, alitoa ombi hilo jana katika mikutano ya kampeni ya chama hicho, katika Kijiji cha Kikatiti na Maleu, wakati mgombea ubunge wa chama hicho, Nassari akiomba kura.

Nyerere ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, alisema uchaguzi wa Jimbo la Arumeru Mashariki unasura ya kitaifa, hivyo ni busara kutoa fursa kwa Watanzania wengi kuwajua wagombea, sera zao na nini wamejipanga kuwafanyia wakazi wa jimbo hilo.

"Sisi Chadema tunataka wagombea wengine wakubali hasa CCM ambao wamekuwa wakikacha midahalo ili tutowe fursa kwa Watanzania kuwajua wagombea wao kwani kipindi cha kampeni ni kifupi sana, hivyo hakitowi nafasi wagombea kujulikana,"alisema Nyerere.

My take: Naunga mkono hoja -Mdahalo utasaidia sana wapiga kura kuwaelewa wagembea na mambo wanayoyasimamia.

Dalili za kushindwa hizo. Watanzania wameshagundua midahalo inakuwa ikiongozwa na wafuasi wa vyama fulani fulani kwa malengo ya kutoa upendelea fulani na ndiyo maana unakuta katika midahalo hiyo washiriki wengi wanakuwa wamevalia sare za vyama hivyo cha ajabu zaidi hata kiongozi wa mdahalo anakuwa naye yuko katika Gwanda.
Tukiacha hayo, mbona CDMA wanajisifu kuwa mgombea wao amezaliwa Arumeru na kukulia hapo sasa wanataka wananchi wamfahamu kuhusu nini? Acheni kutafuta ushindi wa mezani na Rose Kitwangi.
 
Back
Top Bottom