Wanaohusika na midahalo kazi kwenu.
Mimi ningeshauri hoja hii ichukuliwe na Pascal Mayalla = Pasco = Pasco (wa JF) kwa kuanzia tu (kuhusu ile hoja yake ya kuchukua michango ya hapa JF kuanzishia midahalo ya kwenye Televisheni), au mnaonaje wakuu ...
Kama uliangalia midahalo ya 2010 iliyorushwa na tbc toka jimboni arumeru east ilishiriki na hapo ndo nilipata kumfahamu nasary kwa mara ya kwanza nafikiri ni vyema mdahalo ukawepo na najua utakuwepo kwani hata nzega ulikuwepo, wagombea tutawaona kwa hoja.
mdahalo wa wagombea Arumeru ili wananchi tuwapime vizuri uwezo wao
wewe ni mpiga kura wa arumeru?
Chadema, kimeomba kufanyika mdahalo wa wagombea wote wa ubunge wa jimbo la Arumeru Mashariki ili kutoa fursa kubwa kwa wapigakura wa jimbo hilo na Watanzania kwa ujumla, kuwafahamu.
Meneja Mwenza wa kampeni wa Chadema, Vincent Nyerere, alitoa ombi hilo jana katika mikutano ya kampeni ya chama hicho, katika Kijiji cha Kikatiti na Maleu, wakati mgombea ubunge wa chama hicho, Nassari akiomba kura.
Nyerere ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini, alisema uchaguzi wa Jimbo la Arumeru Mashariki unasura ya kitaifa, hivyo ni busara kutoa fursa kwa Watanzania wengi kuwajua wagombea, sera zao na nini wamejipanga kuwafanyia wakazi wa jimbo hilo.
"Sisi Chadema tunataka wagombea wengine wakubali hasa CCM ambao wamekuwa wakikacha midahalo ili tutowe fursa kwa Watanzania kuwajua wagombea wao kwani kipindi cha kampeni ni kifupi sana, hivyo hakitowi nafasi wagombea kujulikana,"alisema Nyerere.
My take: Naunga mkono hoja -Mdahalo utasaidia sana wapiga kura kuwaelewa wagembea na mambo wanayoyasimamia.