Uwaziri wa Dr. Hussein Mwinyi ni halali?

Uwaziri wa Dr. Hussein Mwinyi ni halali?

Rio Tinto

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2014
Posts
777
Reaction score
452
Wadau kuna swali linaniumiza kichwa juu ya uteuzi wa Dr. Huseein Mwinyi kuwa Waziri katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Hussein Mwinyi ni mwakilishi toka Zanzibar ambapo Uchaguzi umefutwa...kwa tafsiri ya kisheria uwakilishi wake ni wa utata...itakuaje pindi uchaguzi utakaporudiwa na Dr. Hussein Mwinyi kushindwa kutetea kiti chake?

wajuzi wa sheria tunaomba muungozo wenu hapa maana waandishi wetu hawajui kuibua issues wao wana report events..
 
Nimejiuliza sana na mm ila sijapata majibu au labda kuna ufaham sina kuhusu hili
 
zanzibar walifuta uwakilishi lakini siyo wabunge.yeye amekuja kama mbunge
 
huyo ni mbunge wa bunge la muungano kwa iyo uchaguz wa zenji aumuhusu
 
Ko vituo vya muungano na uwakilishi vilikuwa tofauti???nisaidieni wenye kuelewa
 
Ko vituo vya muungano na uwakilishi vilikuwa tofauti???nisaidieni wenye kuelewa

Kituo Ni Kimoja,kadi Ya Kupigia Kula Ni Moja Tofauti Ni Masanduku Lakini Pia Wasimamizi Ni Wale Wa Zec
 
Wadau kuna swali linaniumiza kichwa juu ya uteuzi wa Dr. Huseein Mwinyi kuwa Waziri katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Hussein Mwinyi ni mwakilishi toka Zanzibar ambapo Uchaguzi umefutwa...kwa tafsiri ya kisheria uwakilishi wake ni wa utata...itakuaje pindi uchaguzi utakaporudiwa na Dr. Hussein Mwinyi kushindwa kutetea kiti chake?

wajuzi wa sheria tunaomba muungozo wenu hapa maana waandishi wetu hawajui kuibua issues wao wana report events..


Baada ya kufuatilia kwa umakinini kuhusu mambo ya Zanzibar nimeelewa kuwa: Wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015, uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Sheia ulisimamiwa na ZEC ya Jecha. Hata hivyo uchaguzi wa Rais wa Muungano na wabunge wa Muungano huko Zanzibar ulisimamiwa na ZEC kwa niaba ya NEC ya Lubuva. Jecha alipoamua kufanya mambo yake, alifuta uchaguzi wa Zanzibar tu (Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Sheia) na kuacha ule ulio chini ya NEC ya Lubuva. Basi baada ya sarakasi za Jecha, basi matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Muungano na wabunge wa Muungano huko Zanzibar yalihalalishwa na NEC na yale ya Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Sheia yaliharamishwa na Jecha. Hivyo basi Dr Hussein Mwinyi aliyekuwa anagombea kiti cha bunge la Muungano ni halali kwa kauri ya NEC. Hapo ndipo hadithi ya kupika nyama ya Kuku na ya Nguruwe chungu kimoja halafu baada ya kuivisha ukasema nyama ya kuku halali na nyama ya nguruwe ni haramu ikaanza. Wataalamu wa sheria na katiba wataweza fafanua zaidi.
 
Tunawaomba wanasheria wetu tumieni elimu yenu kutujuza watanzania tusiojua Sheria Kwa matukio ya kisheria.ZEC ilifuta uchaguzi Wa Zanzibar lakini tukashangaa kura za urais zilihesabiwa wakati wapiga kura ni wale wale ambao inasemekana kulikuwa Na dosari.Waziri Mkuu kathibitishwa Na bunge bila wabunge kutoka Zanzibar.Jana Mh.Magufuli kamwapisha Dr.Mwinyi kuwa Waziri Kwa kuwa in mbunge toka Zanzibar wakati Zanzibar uchaguzi ulifutwa.Swali he in halali Kwa Waziri Mkuu kuthibitishwa Na bunge bila wabunge Wa Zanzibar?Je ni halali Kwa Dr.Mwinyi kuwa Waziri wakati Zanzibar hakuna mbunge Kwa maana ya uchaguzi kufutwa? Tunaomba ufafanuzi wenu wanasheria wetu.
 
Wadau kuna swali linaniumiza kichwa juu ya uteuzi wa Dr. Huseein Mwinyi kuwa Waziri katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dr. Hussein Mwinyi ni mwakilishi toka Zanzibar ambapo Uchaguzi umefutwa...kwa tafsiri ya kisheria uwakilishi wake ni wa utata...itakuaje pindi uchaguzi utakaporudiwa na Dr. Hussein Mwinyi kushindwa kutetea kiti chake?

wajuzi wa sheria tunaomba muungozo wenu hapa maana waandishi wetu hawajui kuibua issues wao wana report events..
zec zanzibar ilifuta matokeo ya urais wa zanzibar wawakilishi na madiwan tu.ubunge na ya urais wa muungano hayatorudiwa. kwa hiyo mwinyi tayari yeye ni mbunge uchaguzi wao haurudiwi
 
yeye ni mbuge na siyo mwakilishi.wabunge wote wazanzibar waliochagulia hawan shida kwani matokeo yaok hayakufutwa ila wale wawaklishi na raisi wao ndiyo yalifutwa
 
Baada ya kufuatilia kwa umakinini kuhusu mambo ya Zanzibar nimeelewa kuwa: Wakati wa uchaguzi wa mwaka 2015, uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Sheia ulisimamiwa na ZEC ya Jecha. Hata hivyo uchaguzi wa Rais wa Muungano na wabunge wa Muungano huko Zanzibar ulisimamiwa na ZEC kwa niaba ya NEC ya Lubuva. Jecha alipoamua kufanya mambo yake, alifuta uchaguzi wa Zanzibar tu (Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Sheia) na kuacha ule ulio chini ya NEC ya Lubuva. Basi baada ya sarakasi za Jecha, basi matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Muungano na wabunge wa Muungano huko Zanzibar yalihalalishwa na NEC na yale ya Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Sheia yaliharamishwa na Jecha. Hivyo basi Dr Hussein Mwinyi aliyekuwa anagombea kiti cha bunge la Muungano ni halali kwa kauri ya NEC. Hapo ndipo hadithi ya kupika nyama ya Kuku na ya Nguruwe chungu kimoja halafu baada ya kuivisha ukasema nyama ya kuku halali na nyama ya nguruwe ni haramu ikaanza. Wataalamu wa sheria na katiba wataweza fafanua zaidi.


Issa michuzi alipost juzi mama mmoja mwanasheria akikata mzizi Wa fitna kuhusu NEC na ZEC. Google "tofauti kati NEC na zec" kisha msikilize Hugo mama. utaelewa
 
Kituo Ni Kimoja,kadi Ya Kupigia Kula Ni Moja Tofauti Ni Masanduku Lakini Pia Wasimamizi Ni Wale Wa Zec

Kituo kimoja, karatasi za kura za ububge na uraisi wa jmt zilikuwa na kama za huku ila na ukumbuke wazannzibar wanapiga kura 5 yaani ya rasi na wabunge wa jmt na 3 udiwan, baraza la wakilishi na urais smz na wanapaka wino vidole viwili
 
Umejiunga lini JF? mbona ufafanuzi umetolewa mara kibao tu kipindi ata uraisi wa jmt matokeo yake yanatangazwa?!! Yule ni mbunge wa jmt na si mjumbe wa baraza la wawakilishi zanzibar
 
huyo ni mbunge wa bunge la muungano kwa iyo uchaguz wa zenji aumuhusu
Mbunge wa Bunge la muungano maanake nini?
Kwani Zanzibar walisitisha uchaguzi ulio husu kitu gani,je,hii ina maana Wabunge wa Zamani wanaendelea na uwakilishi wa wananchi na wanaweza kuteuliwa kwenye nyadhifa mbali mbali ndani ya Serikali ya muungano au?

Binafsi naona kuna utata sana,ya nini kulazimisha mambo,kitu kingine huyu mtoto wa Mzee Mwinyi kwa nini anateuliwa kwenye Baraza la Mawaziri takribani awamu zote - je hii imekaaje kaaje ina maana hakuna Wazanzibari wengine zaidi yake - kwa nini hapewi shughuli nyingine za kufanya hata kama mnamjenga kwa lengo fulani sio lazima hawe Waziri wa kudumu hii haileti picha nzuri hata kidogo linapo kuja suala la Demokrasia, nalisema hili kwa nia njema tu,kama tumeweke kikomo cha term za Urais nchini kwa nini na Uwaziri husiwekewe kikomo akatafutiwa kazi nyingine ya kufanya.
 
Back
Top Bottom