Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam wafunguliwa

CPU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
3,863
687
Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Nyerere - Julius Nyerere International Airport (JNIA) umefunguliwa rasmi tena leo Feb 17, 2011 mchana saa saba na dk 4 baada ya kufungwa muda mfupi ilipotua ndege ya Shirika ya Swiss jana saa tatu usiku. Uwanja huo ulifungwa kutokana na milipuko ya mabomu kambi ya jeshi Ukonga jijini Dar es Salaam

Mabomu hayo pia yaliruka na kuingia mpaka ndani ya uwanja huo na kuharibu baadhi ya maeneo yanayotumika kupitia ndege, yaani TAXWAY pamoja na RUNWAY ambapo vipande vipatavyo kumi vya mabomu vilionekana ktk runway ya uwanja huo.


111.jpg

Ndege ya shirika la Ndege la Afrika ya Kusini, South African Airways kama ilivyokutwa leo Feb 17, 2011 majira ya saa Kumi jioni, ambapo ilishindwa kuendelea na safari

222.jpg


Ndege ndogo ndio zilianza kuruka baada ya kuruhusiwa kuruka leo Feb 17, 2011 mchana saa nane.





333.jpg


Ndege ya shirika la Ndege la Switzerland, Swiss Airways kama ilivyokutwa leo Feb 17, 2011 ambapo mpaka saa 12 jioni ilikuwa haijaondoka



Hata hivyo ktk tukio hilo la aina yake, jana usiku abiria waliokuwa ktk ndege hiyo ya Swiss waligoma kushuka ktk ndege hiyo kutokana na kupata hofu ya milipuko ya mabomu ambapo baadhi walisema ni bora wafie humo humo ndani ya ndege. Wakati abiria hao wakigoma kushuka, abiria wengine waliokuwa wanasubiri kuondoka walitaharuki na kuanza kukimbilia ndani ya ndege ya Swiss bila ya kuruhusiwa.

Ndege hiyo pia ilinusurika kupigwa na milipuko hiyo ya mabomu ambapo ilitua upande wa pili wa runway ya uwanja huo wa ndege kuelekea upande ambapo mabomu yalikuwa yanalipuka.

Picha za maeneo ya yaliyochimbika ktk uwanja huo nitawaletea muda si mrefu

All News by CPU
 
Kwa kuongezea ni kwamba hakuna mabomu yatakayolipuliwa zaidi kutokana pia na eneo kuwa karibu na uwanja wa ndege wa Dar
 
Hivi Kumbe walikuwa wanayalipua wenyewe nyama hawa?

Hapana! Kuna taarifa zilizagaa kwamba kuna mengine yapo hayajalipuka, ndo watu wakaambizana kwamba yatalipuliwa na wanajeshi. Sasa zoezi hilo haliwezi kufanyika kwa sababu mojawapo ikiwa ni unyeti wa kuwepo uwanja wa kimataifa wa ndege karibu
 
CPU nakukubali kwa taarifa moto moto, bora tuendele kubeba box tu huku umangani manake nchi hata haieleweki inaongozwaje na wanajeshi bado wamelala usingizi
 
CPU nakukubali kwa taarifa moto moto, bora tuendele kubeba box tu huku umangani manake nchi hata haieleweki inaongozwaje na wanajeshi bado wamelala usingizi

Nitaendelea kuwamwagia bila kuficha mambo yote yanayojiri tena kwa picha nikibahatika kufika maeneo husika ya habari zenyewe

CPU camera yako Kiwangoi sana! Shukrani

Mchungaji una uwezo mkubwa sana wa kusoma vitu. Ni kamera ya simu huwezi amini
 
Kwa kuongezea ni kwamba hakuna mabomu yatakayolipuliwa zaidi kutokana pia na eneo kuwa karibu na uwanja wa ndege wa Dar
kwa hiyo watalipua lkambia ganii tena? Arusha nini? tujuzane mapema wandugu
 
kwa hiyo watalipua lkambia ganii tena? Arusha nini? tujuzane mapema wandugu

Kaka haya mabomu yanalipuka yenyewe kutokana na kukaa muda mrefu bila kutumika wala kuondolewa, hayalipuliwi
 
Kusema la ukweli Tanzania tutazidi kuwa nyuma miaka nenda miaka rudi..nimekuwa nikisikiliza vyombo vya habari this morning eti JWTZ
wanajitetea kuwa hayo mabomu yalipaswa kuwa discarded 20 years ago na yamelipuka kutokana na chumba cha kuhifadhiwa kukosa umeme kwa hiyo lile joto ndo limeactivate....jamani hiyo sababu hata mtoto wa kindergated hawezi amini..where are going jamani watanzania??kwanini tunazidi kurudishana nyuma tuuu..nikifikiria nchi yangu hasira zanipanda looh.
 
Ivuga mimi nilidhani wewe teja la JF kumbe hata bness mwendo mdundo. Yaani umeshaona opportunity tayari loh!
 
Ivuga mimi nilidhani wewe teja la JF kumbe hata bness mwendo mdundo. Yaani umeshaona opportunity tayari loh!

Jamaa nilifikiri kaishia msimbazi tu, kumbe ni mjasiliamali
 
Hivi zoezi la Kuyaharibu huwa linafanyikaje....maana yamelipuka hivi tu zahama je kuyaharibu si itakuwa bara!
 
Hivi zoezi la Kuyaharibu huwa linafanyikaje....maana yamelipuka hivi tu zahama je kuyaharibu si itakuwa bara!

Unajua saa hizi kuna hofu ya kulipuka mabomu zaidi ktk magala ya silaha Lugalo, Ngerengere n.k. kama inavyodaiwa na baadhi ya watu. Sasa hilo ghala namba 23 ambalo halijalipuka itakuwaje???
Si nalo linaweza kulipuka wakati wowote??? Hizo kamati sijui mabaraza ya Usalama yataweza vp kuzuia ghala lililobaki lisilipuke???? Mi nahisi nalo litalipuka wakati wowote tu
 
Kama ni hiyo habari tutegemee milipuko zaidi katika kambi yeyote kwani tatizo la umeme ni la nchi nzima kambi gani itapona?Wananchi wahame karibu na makambi ya jeshi,joto litaongezeka na yatalipuka maana bado tuna mgao na viyoyozi havifanyi kazi,take care
 
Back
Top Bottom