Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kilipokea jumla ya shilingi za kitanzania billion 2. 5 kama msaada wa ujenzi na uchimbaji wa visima 700.
Pesa hizo zilitolewa na mfanyabiashara Mustapha Sabodo a ajili ya majimbo 25 yanayoshikiliwa na wabunge wa chama hicho mwaka 2011 mwezi November.
Maswali yangu kwa wabunge wa CHADEMA na viongozi wetu ni haya machache tu
1. Viko wapi hivyo visima 700 vyenye thamani ya shilling billion 2.5 katika majimbo yetu 25 ya uchaguzi?
2. Mimi mbunge wangu ni mhe. Mnyika ningependa kujua visima hivyo vipo eneo gani haswa ukizingatia sisi wakazi wa ubungo tuna shida ya maji?
3. Wabunge wa CHADEMA tuleteeni idadi ya visima hivyo katika majimbo yenu na sehemu vilipochimbwa wananchi tufhamu
4. Kama hamna hivyo visima pesa hizo zilitumika katika eneo gani na mtuletee mchanganuao.
Tafadhali, nisitwe msaliti nataka kujua kwa sasabu jana tulikuwa na diwani wetu huku ubungo kilungule akashindwa kujibu hilo swali akataka aulizwe mbunge na viongozi wa kitaifa
Aliyekua mfadhili wa Chama, Mzee Sabodo alishawahi toa msaada wa mamilioni ya fedha kwa CHADEMA kusaidia jitihada za upatikanaji wa maji kwa uchimbaji wa visima katika majimbo yanayoongozwa na wabunge watokanao na chama hicho!
Kama mdau wa maendeleo ningependa kupata mrejesho toka kwa wapenda maendeleo wenzangu, kama kuna dalili zozote za matumizi sahihi ya fedha zilizotolewa kwa shughuli husika!
Napata mashaka kama kuna lolote limefanyika mpaka sasa! Kama lipo basi tungependa kuona tu visima vichache vilivyotokana na fedha zilizotolewa!
Visima 1236.
Swali jingine lipo au tufunge thread?
hivi ulivyoandika hata mtoto wangu anaweza.
nitafuatilia huu uzi hadi mwisho kama hamna majibu leo nitajua Tanzania upinzani umekufa rasimi.
Kwanza dr slaa alituahidi kuwa majimbo ya upinzani yatakuwa ya mfano,hilo sijaliona hadi leo
Thubutu nani wa kujenga visima hapo, ok kwa idadi hiyo mliyotupa tunakubali je location wapi vipo.
Du! Inaonesha tushalamba vihela vya Sabodo kama ndivyo!
Dogo umeambiwa Sabodo ndio serikali? Hili lakujenga visima waulize waliotawala zaidi ya miaka 50 wamejenga vingapi full stop!
mkuu Avanti huu uzi hatuwezi kupata majibu.wameshaanza kuogopa na pengine watakuita gamba au kijana wa zito
mkuu Avanti huu uzi hatuwezi kupata majibu.wameshaanza kuogopa na pengine watakuita gamba au kijana wa zito