Avanti
JF-Expert Member
- Aug 24, 2010
- 1,209
- 239
Angewahoji wenzake Mh. Zitto hili sijui ingekuwaje?
Anyway hebu tujibuni basi viongozi wetu, kuna visima vingapi? Vipo wapi?
Je, miradi yetu mingine(kama ofisi ya pale Mwenge) aliyotusaidia tuifanikishe imefikia wapi?
Jana wakati napost wengi wetu tulikuwa kwenye shamrashamra za sherehe za Uhuru. Labda leo Kurugenzi yetu ya Habari itajibu maswali haya!
============
SIMILAR CASES:
April 8, 2015
October 11, 2016:
Anyway hebu tujibuni basi viongozi wetu, kuna visima vingapi? Vipo wapi?
Je, miradi yetu mingine(kama ofisi ya pale Mwenge) aliyotusaidia tuifanikishe imefikia wapi?
Jana wakati napost wengi wetu tulikuwa kwenye shamrashamra za sherehe za Uhuru. Labda leo Kurugenzi yetu ya Habari itajibu maswali haya!
============
SIMILAR CASES:
April 8, 2015
Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) kilipokea jumla ya shilingi za kitanzania billion 2. 5 kama msaada wa ujenzi na uchimbaji wa visima 700.
Pesa hizo zilitolewa na mfanyabiashara Mustapha Sabodo a ajili ya majimbo 25 yanayoshikiliwa na wabunge wa chama hicho mwaka 2011 mwezi November.
Maswali yangu kwa wabunge wa CHADEMA na viongozi wetu ni haya machache tu
1. Viko wapi hivyo visima 700 vyenye thamani ya shilling billion 2.5 katika majimbo yetu 25 ya uchaguzi?
2. Mimi mbunge wangu ni mhe. Mnyika ningependa kujua visima hivyo vipo eneo gani haswa ukizingatia sisi wakazi wa ubungo tuna shida ya maji?
3. Wabunge wa CHADEMA tuleteeni idadi ya visima hivyo katika majimbo yenu na sehemu vilipochimbwa wananchi tufhamu
4. Kama hamna hivyo visima pesa hizo zilitumika katika eneo gani na mtuletee mchanganuao.
Tafadhali, nisitwe msaliti nataka kujua kwa sasabu jana tulikuwa na diwani wetu huku ubungo kilungule akashindwa kujibu hilo swali akataka aulizwe mbunge na viongozi wa kitaifa
October 11, 2016:
Aliyekua mfadhili wa Chama, Mzee Sabodo alishawahi toa msaada wa mamilioni ya fedha kwa CHADEMA kusaidia jitihada za upatikanaji wa maji kwa uchimbaji wa visima katika majimbo yanayoongozwa na wabunge watokanao na chama hicho!
Kama mdau wa maendeleo ningependa kupata mrejesho toka kwa wapenda maendeleo wenzangu, kama kuna dalili zozote za matumizi sahihi ya fedha zilizotolewa kwa shughuli husika!
Napata mashaka kama kuna lolote limefanyika mpaka sasa! Kama lipo basi tungependa kuona tu visima vichache vilivyotokana na fedha zilizotolewa!